John John Msakuzi
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 279
- 99
Akiongea na waandishi wa Habari Mkuu wa Mkoa wa Tabora anasema Serikali ya Awamu ya Sita imetoa TZS 52.8 bilioni kwa ruzuku ya mbolea, mbegu na miradi ya umwagiliaji ili kuongeza tija na usalama wa chakula.
Skimu za umwagiliaji nazo zimeongezeka kutoka 25 mwaka 2020 hadi 46 mwaka 2025 na eneo la umwagiliaji kutoka ekari 16,453.25 hadi 37,560.25. Vyama vya umwagiliaji vimeongezeka kutoka 10 hadi 23, na upatikanaji wa mbolea kutoka tani 34,109 mwaka 2020|2021 hadi tani 61,504 mwaka 2024|2025.
Kutokana na hayo, uzalishaji wa tumbaku umeongezeka kutoka kilo 29,829,742 mwaka 2021 hadi kilo 62,964,460 mwaka 2025. Matumizi ya Mbolea yameongezeka kutoka Tani 30 hadi 60,000 wakati uzalishaji wa Tumbaku nao ukiongezeka kutoka Tani 30,000 hadi 60,000