Uwezo wa Malkia Elizabeth wa Uingereza

3squere

JF-Expert Member
Aug 2, 2011
925
181
Nguvu na uwezo alionao Malkia Elizabeth wa Uingereza...

1. Haitaji leseni ya gari, huendesha bila leseni

2. Husafiri bila passport nje ya nchi

3. Huwa anasherehekea siku ya kuzaliwa mara mbili, ile ya kweli 21 april na jumamosi ya jully

4. Ana mtunga mashairi wake maalumu.

5. Ana ATM mashine yake binafsi ya kutoa ela

6. Bila ruhusa yake hakuna muswada utapitishwa kuwa sheria

7. Ana uwezo wa kutolipa kodi

8. Ana uwezo wa kumuonya waziri yoyote, na hata kumwajibisha

9. Ni malkia wa Australia pia

10. Ukiacha ukuu wake katika UK na Australia pia anaongoza nchi zifuatazo Antigua and Barbuda, the Bahamas, Barbados, Belize, Canada, Grenada, Jamaica, New Zealand, Papua New Guinea, Saint Kitts and Nevis, Saint Lucia, Saint Vincent and the Grenadines, Solomon Islands, na Tuvalu.

11. Ni mwenyekiti wa kanisa la Anglikana

12. Ana uwezo wa kuivunja serikali ya Australia

13. Anakinga ya kutoshitakiwa

14. Anamiliki ndege aina ya swans, kongoro katika mto thames

15. Anauwezo wa kumteuwa spika kwa amri yake
 
Nguvu na uwezo alionao Malkia Elizabeth wa Uingereza...

1. Haitaji leseni ya gari, huendesha bila leseni

2. Husafiri bila passport nje ya nchi

3. Huwa anasherehekea siku ya kuzaliwa mara mbili, ile ya kweli 21 april na jumamosi ya jully

4. Ana mtunga mashairi wake maalumu.

5. Ana ATM mashine yake binafsi ya kutoa ela

6. Bila ruhusa yake hakuna muswada utapitishwa kuwa sheria

7. Ana uwezo wa kutolipa kodi

8. Ana uwezo wa kumuonya waziri yoyote, na hata kumwajibisha

9. Ni malkia wa Australia pia

10. Ukiacha ukuu wake katika UK na Australia pia anaongoza nchi zifuatazo Antigua and Barbuda, the Bahamas, Barbados, Belize, Canada, Grenada, Jamaica, New Zealand, Papua New Guinea, Saint Kitts and Nevis, Saint Lucia, Saint Vincent and the Grenadines, Solomon Islands, na Tuvalu.

11. Ni mwenyekiti wa kanisa la Anglikana

12. Ana uwezo wa kuivunja serikali ya Australia

13. Anakinga ya kutoshitakiwa

14. Anamiliki ndege aina ya swans, kongoro katika mto thames

15. Anauwezo wa kumteuwa spika kwa amri yake
mkuu kwahyo mtu mmoja anaongoza nchi zote hzo na kila nchi ina mpa mshaharA?
 
Inashangaza kwamba wazungu pamoja ukweli kwamba ni jamii iliyoelimika zaidi wanaweza kuruhusu ujinga kama huu kuendelea,kwamba ukoo mmoja unatawala nchi vizazi na vizazi!
kwako ndio unaona kama ujinga hiyo ni kama mila na desturi zao na kila jamii ina utamaduni wake na wana heshimu utamaduni wao. sio kama bongo hawajali wachakulia vitu easy tu
 
Mkuu unamengi Sana tudokeze kidogo kaka! Rip princess Diana

Princess Diana alikuwa mjamzito tayari, alipoanza mapenzi mazito na Dodi Al Fayad, mtoto wa tajiri wa asili ya kiarabu wa UK..

Camilla, ndio alisababisha yote haya ktk familia yake Diana na mumewe kusambaratika, baada ya Princess Diana kulalamika sana kwa Malkia, jinsi mumewe anamtesa kimapenzi anamuona kama house girl, na anachepuka kwa malove ya nguvu na Camilla, lakini Malkia alishindwa muonya mwanae Prince Charles.. Prince Charles mapenzi yalikolea kwa Camilla, jua Camilla, alikuwa mpenzi wa Charles kabla hajamuoa Princes Diana, mambo yalizidi kuwa mabaya ndani ya Kasri la Malkia, Diana Princess of Wales akaamua kuondoka, na kujitenga, bahati mbaya akiwa na hasira ya mapenzi na kama yuko confused hv, akaanza mapenzi na Dodi Al Fayed, na kushika UJAUZITO, huku akiwa ktk mapenzi na Dodi, Familia ya Malkia ilichukia sana sana, kuona familia hii wanaoichukulia ni takatifu kwa mila zao, Princess of Wales ana mimba ya mtu mwingine... Basi tena, ikatafutwa namna aibu kuu hii isiifikie Familia ya malkia, mipango ikapangwa, ikaonekana ni kumundolea uhai wake tu...

Basi 1997, ajali ikatengenezwa, Princess Diana na Dodi, walifariki ktk ajali ya gari Paris, France 1997 ikawa mwisho wa maisha yake duniani, Mungu ana mengi sana siku ya mwisho... ndio HIVYO SIKU YA MWISHO MUNGU ATALIPA KILA MTU KWA UJIRA ULIOFANYA DUNIANI..!!

Wenye dhambi, duniani ni watakatifu, walio wema
na wenye haki ktk dunia hii ndio WANAMALIZWA NA KUTEKETEZWA...!!
 
babaake dodi bado analalamika mpaka leo kuwa mwanae aliuliwa kwa makusudi

100%, yuko sahihi, na Dunia inajua huo ndio ukweli..!! Kifo cha Diana Princess of Wales, kiligusa sana nyoyo za watu duniani.. inaumiza sana..!! Kumbuka Diana akiwa msichana mbichi, mwanzoni hakutaka kabisa kuolewa ktk Familia ya Malkia, but kutokana na mashinikizo ya Malkia na wao ndio wenye nguvu UK, basi tena akakubali, ila Prince Charles atalipwa na Mungu, he is the source of all evils juu ya Diana... hata watoto wake wote wawili wa kiume William na Harry, wanajua huu ukweli.. leo ni watu wazima ila hawatasahau unyama aliofanyiwa mama yao.. na Charles asivyo na hata aibu akamuoa CAMILLA na sasa ni mkewe... na Malkia akaruhusu yote haya.. Inauma sana..!!
 
Diana alikuwa sahihi kukataa tangu mwanzo angeweka msimamo ingekuwa sawa ila baadae alipoingia kwenye mahusiano na yule mmisri ndipo alipoharibu maana kwa vyovyote mtoto angezaliwa angekuwa na sehemu katika ufalme jambo ambalo lingeleta shida kifupi unapoamua kuingia kwenye hizi familia kubwa jua kabisa utapoteza Uhuru kwa kiasi kikubwa na hutaishi unavyotaka bali wanavyotaka
 
babaake dodi bado analalamika mpaka leo kuwa mwanae aliuliwa kwa makusudi
Kwa kweli ilimuuma sana na alikuwa anasimamia haki ya mwanae mpaka america lakini imeshindikana.

Nilimuona (Mohamed Al Fayed siku moja Harrod's alikuwa na wasiwasi sana akipanda ngazi huku anaangalia nyuma akiwa na walinzi kibao, poor guy
 
Inashangaza kwamba wazungu pamoja ukweli kwamba ni jamii iliyoelimika zaidi wanaweza kuruhusu ujinga kama huu kuendelea,kwamba ukoo mmoja unatawala nchi vizazi na vizazi!

Waingereza hawachelewi.

Akitokea chizi mmoja akishawishi kuwe na referendum ya kuondoa utawala wa Malkia inawezekana.
 
Waingereza hawachelewi.

Akitokea chizi mmoja akishawishi kuwe na referendum ya kuondoa utawala wa Malkia inawezekana.
Hili halitawezekana kamwe mkuu...nakumbuka kuna kipindi cha Blair kulikuwa na chokochoko za familia hiyo ilipe kodi.. uliza walichoambiwa...kuna siri nzito na kubwa saana juu ya uzao ule.
 
Hili halitawezekana kamwe mkuu...nakumbuka kuna kipindi cha Blair kulikuwa na chokochoko za familia hiyo ilipe kodi.. uliza walichoambiwa...kuna siri nzito na kubwa saana juu ya uzao ule.

Inawezekana mkuu.
 
Namba 11 nimeipenda! Ipo siku Waanglicana huenda Mwenyekiti wao akawa wa dini /dhehebu jingine labda kama Malkia anazuiwa kuwa dini/dhehebu tofauti
 
Back
Top Bottom