Uwezo Duni TBS Unaligharimu Taifa

Hamatan

JF-Expert Member
Nov 10, 2020
3,183
7,645
Leo hii Tanzania imejaa bidhaa nyingi zenye ubora duni zilizotengenezwa China na ndani ya Tanzania, na kwa kiasi kidogo toka India na Thailand.

Leo hii, ni rahisi sana kuikunja nondo ya 16mm iliyotengenezwa Tanzania kuliko nondo ya 12mm iliyotengenezwa Kenya. Mathalani, ukienda dukani kutaka kununua nondo ya 6mm, utaulizwa unataka 6mm nene (imetengenezwa Kenya) au nyembamba (imetengenezwa Tanzania). Unajiuliza, hivi unene wa 6mm unawezaje kuwa na unene wa aina mbili? Ni sawa na mtu akuulize kama unataka kilo moja nyepesi na kilo moja nzito!!

Leo hii, siyo ajabu ukaingia dukani kununua kiatu kilichotengenezwa China, ukavaa asubuhi, jioni kikawa kimechanika.

Kwenye vifaa vya umeme na machinery, huko nako ni balaa. Kila duka zimejaa bidhaa za China, na kwa kukadiria, zaidi ya 70%, zina ubora hafifu kabisa. Mwaka 2017 nilinunua safety boot nchini Australia iliyotengenezwa China (made in China Australian standard) kwa Australian dola 100 (sawa kama U$80 au shilingi 170,000). Mwakajana nilinunua safety boot Dar iliyotengenezwa nchini China kwa shilingi 120,000. Ile ya Australia, mpaka leo, hakuna kilichobadilika, ni kama mpya, LAKINI ile ikiyotengenezwa China hukohuko lakini nikanunulia Dar, nilivaa miezi 4 tu, sole ilibanduka, na haikufaa tena. Huu ni mfano mdogo.

Kilicho dhahiri ni kuwa China inafahamika kwa kutengeneza bidhaa nyingi zenye ubora duni, na chache zenye ubora mzuri ambazo zinapelekwa kwenye mataifa ya watu wanaojitambua, na ambayo yana taasisi zenye uwezo mkubwa wa kupima na kudhibiti ubora.

Kilicho dhahiri hapa kwetu, TBS ni taasisi yenye ubora duni, itawezaji kudhibiti bidhaa zenye ubora duni? TBS ni duni kuanzia uwezo wa wataalam wake, vifaa na hata kimaadili. Wao wanachojali ni kulipwa pesa, ja siyo ubora.

Leo tuna mpaka bidhaa ndogo kama misumari ambayo ni ya kiwango duni kabisa. Misumari ambayo ukipiga kwenye ubao, kama ni hard wood, una uhakika wa zaidi ya 90% lazima utapinda au utashindwa kuingia kabisa.

Pendekezo:
Kwa kuwa taasisi yetu ya viwango haina kiwango, EAC iwe na taasisi moja tu ya kudhibiti viwango, ambayo itakuwa na wataalam wenye uwezo, nyenzo na maadili. Kwa bidhaa ambazo uwezo wa EAC kutambua ubora, ni mdogo, tuyaombe mataifa yenye uwezo kama Australia, tutumie viwango vyao. Mathalani bidhaa zitakazoruhusiwa kuingia nchini zilizotengenezwa China ziwe ni zile zenye label "Made in China Austrakia and EAC standards".

Taifa na watu wake tunapoteza pesa nyingi, tunapata hasara kubwa kwa kuingiza nchini bidhaa zenye ubora duni. Unaweza kununua bidhaa ya kiwango kizuri kwa shilingi 100,000 ikadumu kwa miaka 5, lakini unaweza kununua bidhaa yenye ubora duni kwa shilingi 50,000 halafu ikadumu kwa miezi 3 tu, ni bidhaa ipi inaendana na tjamani ya fedha yako? Watanzania tunaibiwa sana, na mataifa kama China kwa kuwa dampo la bidhaa duni, zisizofaa kuwafikia wateja. Hasara kubwa tuliyo nayo ni kuwa na shirika la viwango kama TBS lisilokuwa na viwango.
 
Uchumi bora utokomeza bidhaa duni

Mtu akiwa na uchumi mzuri atanunua bidhaa bora

Umaskini ndio zao la bidhaa duni Mchina anakutengezea kutokana na bei yako

Mfano bila Mchina kuwepo hata simu za mkononi hapa 80% tusingekua nazo

TBS inapaswa uwe wewe mwenyewe mkuu si ajabu wewe ndio mnunuzi wa feki
 
Leo hii Tanzania imejaa bidhaa nyingi zenye ubora duni zilizotengenezwa China na ndani ya Tanzania, na kwa kiasi kidogo toka India na Thailand.

Leo hii, ni rahisi sana kuikunja nondo ya 16mm iliyotengenezwa Tanzania kuliko nondo ya 12mm iliyotengenezwa Kenya. Mathalani, ukienda dukani kutaka kununua nondo ya 6mm, utaulizwa unataka 6mm nene (imetengenezwa Kenya) au nyembamba (imetengenezwa Tanzania). Unajiuliza, hivi unene wa 6mm unawezaje kuwa na unene wa aina mbili? Ni sawa na mtu akuulize kama unataka kilo moja nyepesi na kilo moja nzito!!

Leo hii, siyo ajabu ukaingia dukani kununua kiatu kilichotengenezwa China, ukavaa asubuhi, jioni kikawa kimechanika.

Kwenye vifaa vya umeme na machinery, huko nako ni balaa. Kila duka zimejaa bidhaa za China, na kwa kukadiria, zaidi ya 70%, zina ubora hafifu kabisa. Mwaka 2017 nilinunua safety boot nchini Australia iliyotengenezwa China (made in China Australian standard) kwa Australian dola 100 (sawa kama U$80 au shilingi 170,000). Mwakajana nilinunua safety boot Dar iliyotengenezwa nchini China kwa shilingi 120,000. Ile ya Australia, mpaka leo, hakuna kilichobadilika, ni kama mpya, LAKINI ile ikiyotengenezwa China hukohuko lakini nikanunulia Dar, nilivaa miezi 4 tu, sole ilibanduka, na haikufaa tena. Huu ni mfano mdogo.

Kilicho dhahiri ni kuwa China inafahamika kwa kutengeneza bidhaa nyingi zenye ubora duni, na chache zenye ubora mzuri ambazo zinapelekwa kwenye mataifa ya watu wanaojitambua, na ambayo yana taasisi zenye uwezo mkubwa wa kupima na kudhibiti ubora.

Kilicho dhahiri hapa kwetu, TBS ni taasisi yenye ubora duni, itawezaji kudhibiti bidhaa zenye ubora duni? TBS ni duni kuanzia uwezo wa wataalam wake, vifaa na hata kimaadili. Wao wanachojali ni kulipwa pesa, ja siyo ubora.

Leo tuna mpaka bidhaa ndogo kama misumari ambayo ni ya kiwango duni kabisa. Misumari ambayo ukipiga kwenye ubao, kama ni hard wood, una uhakika wa zaidi ya 90% lazima utapinda au utashindwa kuingia kabisa.

Pendekezo:
Kwa kuwa taasisi yetu ya viwango haina kiwango, EAC iwe na taasisi moja tu ya kudhibiti viwango, ambayo itakuwa na wataalam wenye uwezo, nyenzo na maadili. Kwa bidhaa ambazo uwezo wa EAC kutambua ubora, ni mdogo, tuyaombe mataifa yenye uwezo kama Australia, tutumie viwango vyao. Mathalani bidhaa zitakazoruhusiwa kuingia nchini zilizotengenezwa China ziwe ni zile zenye label "Made in China Austrakia and EAC standards".

Taifa na watu wake tunapoteza pesa nyingi, tunapata hasara kubwa kwa kuingiza nchini bidhaa zenye ubora duni. Unaweza kununua bidhaa ya kiwango kizuri kwa shilingi 100,000 ikadumu kwa miaka 5, lakini unaweza kununua bidhaa yenye ubora duni kwa shilingi 50,000 halafu ikadumu kwa miezi 3 tu, ni bidhaa ipi inaendana na tjamani ya fedha yako? Watanzania tunaibiwa sana, na mataifa kama China kwa kuwa dampo la bidhaa duni, zisizofaa kuwafikia wateja. Hasara kubwa tuliyo nayo ni kuwa na shirika la viwango kama TBS lisilokuwa na viwango.
Hii taasisi ina upungufu mkubwa wa rasilimali watu, Serikali ishutuke haraka.
 
Kwenye tairi za gari mchina ni mshenzi sana, nilifunga tairi nne zote mpya lakini aisee ndan ya wiki mbili zote chali, yaani tairi zinachanika zinatoa wire na upya wake

Ulizinunua sh ngapi😆😆😆😆
 
Kwenye tairi za gari mchina ni mshenzi sana, nilifunga tairi nne zote mpya lakini aisee ndan ya wiki mbili zote chali, yaani tairi zinachanika zinatoa wire na upya wake
Yanapotokea hayo, unafikiroa sana na kujiuliza, hivi kweli tuna serikali? Jukumu kubwa mojawapo la serikali ni kwalinda watu wake dhidi ya hujuma mbalimbali. Kuruhusu bidhaa duni kuingia nchini, ni kuruhusu wananchi wako waibiwe. Lakini pia ni kupoteza mapato ya nchi.

Pole sana. Wapo wengi wametokewa na hayo. Hapo umepata hasara ya fedha, lakini wengine wamepoteza mpaka maisha kwa ajali ambazo zingeweza kuzuilika.
 
Ni kweli kabisa tunaingia hasara kubwa kama walaji na wakati mwengine hata kuweka uhai wetu na vyombo vyetu rehani hususa ni kwenye vipuri vya magari na mitambo.

Kwa mwananchi wa kawaida hana uwezo wowote wa kujua kuwa bidhaa fulani inakidhi vigezo au la, bali hilo ni jukumu la serikali kuhakikisha bidhaa zisizo na ubora haziingii mtaani/kwenye soko kwa kuziteketeza au kurudisha kwa wazalishaji kama ilivyo kwa vipodozi.
 
Leo hii Tanzania imejaa bidhaa nyingi zenye ubora duni zilizotengenezwa China na ndani ya Tanzania, na kwa kiasi kidogo toka India na Thailand.

Leo hii, ni rahisi sana kuikunja nondo ya 16mm iliyotengenezwa Tanzania kuliko nondo ya 12mm iliyotengenezwa Kenya. Mathalani, ukienda dukani kutaka kununua nondo ya 6mm, utaulizwa unataka 6mm nene (imetengenezwa Kenya) au nyembamba (imetengenezwa Tanzania). Unajiuliza, hivi unene wa 6mm unawezaje kuwa na unene wa aina mbili? Ni sawa na mtu akuulize kama unataka kilo moja nyepesi na kilo moja nzito!!

Leo hii, siyo ajabu ukaingia dukani kununua kiatu kilichotengenezwa China, ukavaa asubuhi, jioni kikawa kimechanika.

Kwenye vifaa vya umeme na machinery, huko nako ni balaa. Kila duka zimejaa bidhaa za China, na kwa kukadiria, zaidi ya 70%, zina ubora hafifu kabisa. Mwaka 2017 nilinunua safety boot nchini Australia iliyotengenezwa China (made in China Australian standard) kwa Australian dola 100 (sawa kama U$80 au shilingi 170,000). Mwakajana nilinunua safety boot Dar iliyotengenezwa nchini China kwa shilingi 120,000. Ile ya Australia, mpaka leo, hakuna kilichobadilika, ni kama mpya, LAKINI ile ikiyotengenezwa China hukohuko lakini nikanunulia Dar, nilivaa miezi 4 tu, sole ilibanduka, na haikufaa tena. Huu ni mfano mdogo.

Kilicho dhahiri ni kuwa China inafahamika kwa kutengeneza bidhaa nyingi zenye ubora duni, na chache zenye ubora mzuri ambazo zinapelekwa kwenye mataifa ya watu wanaojitambua, na ambayo yana taasisi zenye uwezo mkubwa wa kupima na kudhibiti ubora.

Kilicho dhahiri hapa kwetu, TBS ni taasisi yenye ubora duni, itawezaji kudhibiti bidhaa zenye ubora duni? TBS ni duni kuanzia uwezo wa wataalam wake, vifaa na hata kimaadili. Wao wanachojali ni kulipwa pesa, ja siyo ubora.

Leo tuna mpaka bidhaa ndogo kama misumari ambayo ni ya kiwango duni kabisa. Misumari ambayo ukipiga kwenye ubao, kama ni hard wood, una uhakika wa zaidi ya 90% lazima utapinda au utashindwa kuingia kabisa.

Pendekezo:
Kwa kuwa taasisi yetu ya viwango haina kiwango, EAC iwe na taasisi moja tu ya kudhibiti viwango, ambayo itakuwa na wataalam wenye uwezo, nyenzo na maadili. Kwa bidhaa ambazo uwezo wa EAC kutambua ubora, ni mdogo, tuyaombe mataifa yenye uwezo kama Australia, tutumie viwango vyao. Mathalani bidhaa zitakazoruhusiwa kuingia nchini zilizotengenezwa China ziwe ni zile zenye label "Made in China Austrakia and EAC standards".

Taifa na watu wake tunapoteza pesa nyingi, tunapata hasara kubwa kwa kuingiza nchini bidhaa zenye ubora duni. Unaweza kununua bidhaa ya kiwango kizuri kwa shilingi 100,000 ikadumu kwa miaka 5, lakini unaweza kununua bidhaa yenye ubora duni kwa shilingi 50,000 halafu ikadumu kwa miezi 3 tu, ni bidhaa ipi inaendana na tjamani ya fedha yako? Watanzania tunaibiwa sana, na mataifa kama China kwa kuwa dampo la bidhaa duni, zisizofaa kuwafikia wateja. Hasara kubwa tuliyo nayo ni kuwa na shirika la viwango kama TBS lisilokuwa na viwango.
Unashauri nini waende shule ama mamlaka ivunjiliwe mbali?
 
Kwenye tairi za gari mchina ni mshenzi sana, nilifunga tairi nne zote mpya lakini aisee ndan ya wiki mbili zote chali, yaani tairi zinachanika zinatoa wire na upya wake
Mkuu ukiangalia manufacturering dates ya hizo tairi? Isije kuwa zilisha expire?
 
Umasikini wa watanzania ndio unafanya kuwepo na bidhaa duni sokoni, TBS hawawezi kukaza kwa 100% wanasiasa watawajia juu.

Fikiria TV zote madukani zingekuwa na bei za Samsung, LG n.k au simu zote zingekuwa na ubora na bei za iphones, watanzania wangapi wangeweza kumudu?

Kitu pekee ambacho TBS wanakizingatia kwa asilimia kubwa ni usalama / afya za watumiaji. Kwenye bidhaa suala la kudumu muda mrefu au la ni wewe na urefu wa mfuko wako.

Mwenye pesa kidogo nenda kariakoo kanunue tecno, kama zipo za kutosha nenda mlimani city kanunue iphone. The same kwa bidhaa nyingine zote.

Hata kwenye madawa ya binadamu (TMDA) fumula ni hiyohiyo, kuna paracetamol kutoka UK inauzwa 10,000 na kuna paracetamol ya zenufa inauzwa 100, ni wewe na wallet yako.

Nchi masikini hii ndugu, ebo!
 
Kwenye tairi za gari mchina ni mshenzi sana, nilifunga tairi nne zote mpya lakini aisee ndan ya wiki mbili zote chali, yaani tairi zinachanika zinatoa wire na upya wake
... Mkuu penda uhai wako na wapendwa na marafiki zako. Kuna bidhaa unaweza fumba macho lakini sio vitu kama tairi hasa endapo ni mtu wa long safari!

Sijawahi kuwaza kununua tairi mchina hata mara mmoja; sijui King Lion; dah! Nunua Yokohama ex Japan and the like miaka mifano mkataba!
 
Back
Top Bottom