Uwekezaji Singida washika kasi

Uwekezaji Singida washika kasi

Kanyunyu

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2012
Posts
335
Reaction score
495
Vijana wazawa wa Singida wameanza kurejea Nyumbani na kufanya uwekezaji mkubwa hasa Ujenzi wa nyumba za kuishi na hotel za kibiashara

REGENCY HOTEL AND RESORT ni Hotel ya kisasa kabisa iliyozinduliwa hivi karibuni na ni moja ya kazi nzuri iliyofanywa na mzalendo na mzawa wa Singida ndugu Raymond Nkingo ambae alienda kutafuta pesa nje ya mkoa wa Singida na Sasa amerudi kuwekeza Nyumbani kwa kujenga hotel ya kisasa kabisa yenye gorofa 9 , Regency Hotel ipo ufukweni mwa Ziwa Singida ikiwa na mandhari mazuri Sana

Uwekezaji wa hotel ni kichocheo kikubwa cha maendeleo mkoani Singida kwa kuwa itasaidia kutoa ajira kwa Vijana, kuvutia wageni na wadau kuwekeza mkoani Singida

Kwa miongo kadhaa wazawa wa Singida wamekuwa na msukumo mdogo kuwekeza Nyumbani, wengi waliofanikiwa kusoma na kupata fedha wamewekeza mikoa ya Arusha na Dar

Tunawakaribisha wadau wote kuja kuwekeza Singida kwani ni centre nzuri ya kibiashara hasa kuelekea mpango wa serikali kuhamia Dodoma

Singida ya jana, sio Singida ya Leo

#Transforming_Singida

1476333019404.jpg
 
Kweli mna kiu ya uwekezaji!
Mpaka huu mnausifia hivi!!!
Kweeeeli mna hamu muwekezewe!!!

Unataka kutuambia wawekezaji wa kichaga waliowekeza hapo singida miaka kibao walikuwa wanakosea maana walipaswa kuwekeza kwao Kilimanjaro.

Sijui mmelogwa na Mwigulu au Nyalandu?
 
Mkuu hizo ghorofa tisa singida sijaziona ,umeleta ka-uongo hapa
 
Mbona inaonekana jengo la goropha 3 tu?
 
Comrade Hon Mwigulu and others mnaitwa home mkawekeze wenzenu wana hamu na mjengo wa ghorofa 9
 
hahahhahahah we jamaa ni komedi kweli? yaani hiyo hotel moja tu kujengwa ndo unadai eti uwekezaji singida washika kasi. ignorant
 
Vijana wazawa wa Singida wameanza kurejea Nyumbani na kufanya uwekezaji mkubwa hasa Ujenzi wa nyumba za kuishi na hotel za kibiashara

REGENCY HOTEL AND RESORT ni Hotel ya kisasa kabisa iliyozinduliwa hivi karibuni na ni moja ya kazi nzuri iliyofanywa na mzalendo na mzawa wa Singida ndugu Raymond Nkingo ambae alienda kutafuta pesa nje ya mkoa wa Singida na Sasa amerudi kuwekeza Nyumbani kwa kujenga hotel ya kisasa kabisa yenye gorofa 9 , Regency Hotel ipo ufukweni mwa Ziwa Singida ikiwa na mandhari mazuri Sana

Uwekezaji wa hotel ni kichocheo kikubwa cha maendeleo mkoani Singida kwa kuwa itasaidia kutoa ajira kwa Vijana, kuvutia wageni na wadau kuwekeza mkoani Singida

Kwa miongo kadhaa wazawa wa Singida wamekuwa na msukumo mdogo kuwekeza Nyumbani, wengi waliofanikiwa kusoma na kupata fedha wamewekeza mikoa ya Arusha na Dar

Tunawakaribisha wadau wote kuja kuwekeza Singida kwani ni centre nzuri ya kibiashara hasa kuelekea mpango wa serikali kuhamia Dodoma

Singida ya jana, sio Singida ya Leo

#Transforming_Singida

View attachment 417107
Mbona huo uongo ghorofa tisa zinafika hizo , hii ghorofa tisa kwa biashara gani ya kuwalaza watu hapo Singida
 
Mbona huo uongo ghorofa tisa zinafika hizo , hii ghorofa tisa kwa biashara gani ya kuwalaza watu hapo Singida
Hapo kuna Underground gorofa sita. hivi kufanya idadi ya Tisa
 
Singida Hamna gorofa Tisa tafadhali bado ni mkoa ulionyuma sana hapa tz kimaendeleo
 
Back
Top Bottom