Kweli kabisa, kama ule wa Morogoro ni airstrip tu imeota majani wafanyakazi huwa wanafyeka kwa kwanja na kupitisha ufagio kabla ndege haijatua, na ndege zake ni vile vidogo vibajaji. Iringa pale Nduli hali ni hiyohiyo. Shinyanga pale Ibadakuli, Bukoba na Mtwara vyote havikaribii hiyo Chato Airport. Hata Songwe Airport ambayo inapokea ndege kila siku asubuhi na jioni nimeambiwa ni ndogo kuliko hiyo Chato.
Kilichonishangaza, licha ya ukubwa wa Chato airport, Tanzania Airports Authority (TAA) haijaiorodhesha katika tovuti yake kivyovyote.
Tovuti ya TAA
Tanzania Airports Authority imeorodhesha airports zilizoko nchini katika categories 3: international airports, domestic entry and exit, na airstrips. Chato airport haijaorodheshwa. Wanajua sababu.