Uwanja wa ndege wa Dar wafungwa (KIA)

Uwanja wa ndege wa Dar wafungwa (KIA)

UFUNUO WA TANZANIA

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2013
Posts
471
Reaction score
166
Nipo KIA nimeambiwa uwanja wa ndege wa Dar umefungwa na hivyo tumeshindwa kuondoka hadi ufunguliwe. Hatujaambiwa sababu ni nini?
Kama kuna mwana JF yupo hapo JNIA atujuze kwa nini umefungwa?
Au kuna taarifa za kiintelejensia?

Baada ya nusu saa tuliruhusiwa kuondoka kama saa 7 na dk 20 mchana. Nashukuru wote waliotoa majibu juu ya kilichokuwa kimejili dar. Kweli bila JF maisha hayatakuwa ya furaha hapa TZ.
 
We waulize hao waliosema umefungwa kwa sababu zipi? kisha rudi hapa na majibu sahihi.
 
Nimetua hapo saa 5 asbh, huduma zote zinaendelea hapo.
 
Labda fire trucks hayana maji, au Police walienda Arusha kuongeza nguvu
 
Nipo KIA nimeambiwa uwanja wa ndege wa Dar umefungwa na hivyo tumeshindwa kuondoka hadi ufunguliwe. Hatujaambiwa sababu ni nini?
Kama kuna mwana JF yupo hapo JNIA atujuze kwa nini umefungwa?
Au kuna taarifa za kiintelejensia?

Hizo ni taarifa za kitaalam haujafungwa ila kuna ndege ndogo imetua pembeni mwa njia Ingawa Hakuna majeruhi yeyote. nafikiri ndo mana mmeambiwa msubiri kidogo.
 
kwa nini usiwaulize hao waliosema umefungwa kwa sababu gani??
 
Nimetua hapo saa 5 asbh, huduma zote zinaendelea hapo.
 
Nipo KIA nimeambiwa uwanja wa ndege wa Dar umefungwa na hivyo tumeshindwa kuondoka hadi ufunguliwe. Hatujaambiwa sababu ni nini?
Kama kuna mwana JF yupo hapo JNIA atujuze kwa nini umefungwa?
Au kuna taarifa za kiintelejensia?

KIA ni uwanja wa kimataifa, km walitoa taarifa ya kufungwa kwa JK NYERERE INT.AIRPORT, walipaswa kutoa na sabab za kufungwa, na kam walijisahau ulipaswa kuuliza! Pole kwa kucheleweshwa! Vuta subira!
 
Kwa huduma zetu sio ajabu kufungwa na kasha kufunguliwa uwanja wandege na mkaambiwa baadaye chanzo!! Kama treni ya reli ya kati tuu-unaahirisha, unarudisha nk. bila ULAZIMA SAANA kuwataarifu watumiaji wa huduma zako!!! Tuna mambo Tanzania......
 
takribani kama dakika 50 hivi kuna ndege ndogo imeacha njia na kushuka pembeni mwa njia ya ndege. kwa sasa kila kitu kiko shwari.
 
ulifungwa kwa sababu nimewasiri leo hivo niliitaj ulinzi wa kutosha.asanten kwa kuvumilia. mnaweza kuendelea na safari sasa
 
Dsm inatakiwa kuwa na viwanja viwili. Kiwanja cha sasa kibakie kwa matumizi ya ndege za ndani na nchi jirani. Uwanja mpya na wa kisasa ujengwe Bagamoyo ama Kibaha. Ni aibu kutua ktk kakiwanja kalioko sasa. Tunaliabisha jina la Mwl. JK Nyerere!
 
Dsm inatakiwa kuwa na viwanja viwili. Kiwanja cha sasa kibakie kwa matumizi ya ndege za ndani na nchi jirani. Uwanja mpya na wa kisasa ujengwe Bagamoyo ama Kibaha. Ni aibu kutua ktk kakiwanja kalioko sasa. Tunaliabisha jina la Mwl. JK Nyerere!

Wewe ni mkweere?
 
Ni mambo ya kawaida ktk aviation industry.
Nijuavyo JNIA kuna runways 2, imekuwaje hadi kufunga kiwanja kabisa?, au ndege hiyo imeapatia tatizo kwenye intersection ya hizo runways?
Kama ndivyo, basi wafikirie juu ya Parallel runways, zitasolve matatizo madogo kama hayo.
 
Back
Top Bottom