Uwanja wa ndege Kisongo jijini Arusha hauna hadhi

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,851
15,265
Uwanja mdogo wa ndege kisongo ambao mara nyingi hutumika na watalii wanaokodi ndege ndogo kwenda kutalii katika hifadhi za taifa na sehemu za serengeti, ngorongoro na sehemu nyingine zenye vivutio vya utalii, hauna kabisa hadhi ya kuitwa uwanja wa ndege kwa maisha ya kileo. Maana muonekano ni ule ule wa kizamani.

Nyasi na majani., kiwanja hichi cha Ndege ambacho hutumika na ndege ndogo za watalii na abiria Wa ndani ya nchi, Nyasi na majani yamejitoea hovyo ndani ya uwanja na hakuna mpangilio maalum unaonekana wa ukataji wa Nyasi hizo bali ni ule wa hovyo hovyo na sehemu nyingine ndani ya uwanja huo nyasi na majani hazijakatwa bali zimeachwa zijiotee vyovyote vile.

Taa hasa upande unaongalia barabarani maana uwanja huu upo kando ya barabara hii ya kisongo kuelekea monduli na kuelendelea, ni barabara kubwa na muhimu kwani ndio inayotumika na Mabasi yanayoenda Mwanza, singida Dodoma na Pia ndio bara bara kuu inayopitisha watalii kwenda hifadhini lakini ukiangalia vizuri eneo hilo ni giza Mida ya usiku.

Mabango, Kwa hadhi ya kuitwa uwanja mdogo wa kitalii kulipaswa kabisa pembeni ya uwanja na hata kwenye uzio huo ambao unaangalia barabarani basi wengeweka mabango yenye picha yanyoonyesha wanyama wanaopatikana hifadhini, na hata vivutio mbalimbali vilivyopo katika hifadhi zetu ingependeza na kuvutia zaidi na kufanya uwanja kuwa katika hadhi yake.

Pia majengo yaliyomo ndani ni ya kizamani na hayana muonekano mzuri
 
Huo uwanja ulikuwa ni kwa ajili ya ndege ndogo zinazofanya shughuli za kilimo,kama kunyunyiza dawa za kuua wadudu kwenye mashamba nk,nadhani hadi leo pana bango limeandikwa Kilimo anga,pale karibu na control tower,kulikuwa na mpango wa kukiboresha kiwanja kile kwa hadhi ya kimataifa ila baadaye serikali iliona hakuna sababu ya kuwa na viwanja viwili vikubwa kwenye eneo lisilozidi hata kilometa 100,kwani pia kufanya hivyo kungeathiri uchumi wa kilimanjaro na miji midogo midogo ya njiani ambayo inanufaika na uwepo wa kilimanjaro international airport,hivyo uwanja wa arusha uliachwa ubaki kwa shughuli ndogo ndogo kama za utalii nk, ila hivi ninavyoandika hapa shughuli za uboreshaji wa uwanja huo zinaendelea,kama ndugu mtoa mada huna chuki binafsi na mkoa wa arusha au uwanja wake wa ndege utakubaliana na mimi kuwa uboreshaji wa kile kiwanja ulianza muda mrefu tu,runway iliongezwa urefu kwa zaidi ya nusu,eneo lote la uwanja lilizungushiwa fence,barabara ya kuingilia uwanjani ilihamishwa kutoka ile ya zamani iliyokuwa ikipita kwenye geti la magereza ambayo haikuwa na hadhi kabisa,ya sasa ni nzuri sana,yenye lami safi,na taa za kutosha,kuhusu kuweka taa za barabarani upande huu wa barabara ya dodoma ni jambo lisilo na umuhimu mkubwa kwa sasa,kwanza kumbuka kuwa eneo lile lilikuwa ni eneo la madhamba ya kahawa na ngano hadi miaka michache iliyopita,uwanja una taa za kutosha na zilizowekwa kwa mpangilio maalum, na pia si eneo la makazi ya watu,ndege pale huwa zinatua kati ya asubuhi hadi jioni tu,ni nadra sana ndege kupaa au kutua usiku pale,mengine jiongeze mkuu
 
Huo uwanja ulikuwa ni kwa ajili ya ndege ndogo zinazofanya shughuli za kilimo,kama kunyunyiza dawa za kuua wadudu kwenye mashamba nk,nadhani hadi leo pana bango limeandikwa Kilimo anga,pale karibu na control tower,kulikuwa na mpango wa kukiboresha kiwanja kile kwa hadhi ya kimataifa ila baadaye serikali iliona hakuna sababu ya kuwa na viwanja viwili vikubwa kwenye eneo lisilozidi hata kilometa 100,kwani pia kufanya hivyo kungeathiri uchumi wa kilimanjaro na miji midogo midogo ya njiani ambayo inanufaika na uwepo wa kilimanjaro international airport,hivyo uwanja wa arusha uliachwa ubaki kwa shughuli ndogo ndogo kama za utalii nk, ila hivi ninavyoandika hapa shughuli za uboreshaji wa uwanja huo zinaendelea,kama ndugu mtoa mada huna chuki binafsi na mkoa wa arusha au uwanja wake wa ndege utakubaliana na mimi kuwa uboreshaji wa kile kiwanja ulianza muda mrefu tu,runway iliongezwa urefu kwa zaidi ya nusu,eneo lote la uwanja lilizungushiwa fence,barabara ya kuingilia uwanjani ilihamishwa kutoka ile ya zamani iliyokuwa ikipita kwenye geti la magereza ambayo haikuwa na hadhi kabisa,ya sasa ni nzuri sana,yenye lami safi,na taa za kutosha,kuhusu kuweka taa za barabarani upande huu wa barabara ya dodoma ni jambo lisilo na umuhimu mkubwa kwa sasa,kwanza kumbuka kuwa eneo lile lilikuwa ni eneo la madhamba ya kahawa na ngano hadi miaka michache iliyopita,uwanja una taa za kutosha na zilizowekwa kwa mpangilio maalum, na pia si eneo la makazi ya watu,ndege pale huwa zinatua kati ya asubuhi hadi jioni tu,ni nadra sana ndege kupaa au kutua usiku pale,mengine jiongeze mkuu
Kama umesoma mada hapo juu utakubaliana na mimi kuwa niliyoyaandika na uliyoandika wewe ni tofauti, hiyo runaway Nimeona imeongezwa lakini hapo juu sikulizungumzia hilo,

Pili unavyosema swala la taa upande wa barabarani hauna tija kwa sasa na magari ya mikoani na ya watalii yanapita hapo muda wote hizo taa zitakuwa na umuhimu kipindi gani sehemu muhimu kama hiyo.

Ukiwa eneo hilo huwezi kuona bango lolote la muhimu kama nilivoeleza hapo juu,.
Watalii wanaleta pesa za kigeni nchini hata kama ni uwanja mdogo wa ndege lakini uwekwe katika hadhi basi ya kuvutia maana pale ni sawa na shambani
 
watu wa utalii kuna maeneo mnafanya mambo ya hovyo sana, ukiangalia Mbuga ya Ruaha, kweli mbuga maarufu kama ile hakuna barabara ya lami ?? yaani kuanzia mbele kidogo tu ya Iringa (kalenga) mpaka unafika mbugani hakuna lami ? !! kweli mko ''serious'' kazi kusema utalii unaingiza 80% ya fedha za kigeni lakini uwekezaji 0%. haya ukifika pale Ruaha sijui ndo mnaita Bandaz na Cottage, zile nyumba wanazopumzika wafanyakazi, zinasikitisha kwa kweli, yaani nyumba zimejengwa kwa mabati afu joto kama lote, hata mandhara haikisi ule usemi kwamba 80% ya fedha za kigeni ni utalii, kwa jinsi mtu ukiona yale mazingira - hatuko serious !!
 
watu wa utalii kuna maeneo mnafanya mambo ya hovyo sana, ukiangalia Mbuga ya Ruaha, kweli mbuga maarufu kama ile hakuna barabara ya lami ?? yaani kuanzia mbele kidogo tu ya Iringa (kalenga) mpaka unafika mbugani hakuna lami ? !! kweli mko ''serious'' kazi kusema utalii unaingiza 80% ya fedha za kigeni lakini uwekezaji 0%. haya ukifika pale Ruaha sijui ndo mnaita Bandaz na Cottage, zile nyumba wanazopumzika wafanyakazi, zinasikitisha kwa kweli, yaani nyumba zimejengwa kwa mabati afu joto kama lote, hata mandhara haikisi ule usemi kwamba 80% ya fedha za kigeni ni utalii, kwa jinsi mtu ukiona yale mazingira - hatuko serious !!
Ukiangalia private sekta imeboreshwa na zinazidi kuboreshwa kila leo lakini kwa upande wa serikali kila kitu lazima kipigiwe kelele
 
Huo uwanja ulikuwa ni kwa ajili ya ndege ndogo zinazofanya shughuli za kilimo,kama kunyunyiza dawa za kuua wadudu kwenye mashamba nk,nadhani hadi leo pana bango limeandikwa Kilimo anga,pale karibu na control tower,kulikuwa na mpango wa kukiboresha kiwanja kile kwa hadhi ya kimataifa ila baadaye serikali iliona hakuna sababu ya kuwa na viwanja viwili vikubwa kwenye eneo lisilozidi hata kilometa 100,kwani pia kufanya hivyo kungeathiri uchumi wa kilimanjaro na miji midogo midogo ya njiani ambayo inanufaika na uwepo wa kilimanjaro international airport,hivyo uwanja wa arusha uliachwa ubaki kwa shughuli ndogo ndogo kama za utalii nk, ila hivi ninavyoandika hapa shughuli za uboreshaji wa uwanja huo zinaendelea,kama ndugu mtoa mada huna chuki binafsi na mkoa wa arusha au uwanja wake wa ndege utakubaliana na mimi kuwa uboreshaji wa kile kiwanja ulianza muda mrefu tu,runway iliongezwa urefu kwa zaidi ya nusu,eneo lote la uwanja lilizungushiwa fence,barabara ya kuingilia uwanjani ilihamishwa kutoka ile ya zamani iliyokuwa ikipita kwenye geti la magereza ambayo haikuwa na hadhi kabisa,ya sasa ni nzuri sana,yenye lami safi,na taa za kutosha,kuhusu kuweka taa za barabarani upande huu wa barabara ya dodoma ni jambo lisilo na umuhimu mkubwa kwa sasa,kwanza kumbuka kuwa eneo lile lilikuwa ni eneo la madhamba ya kahawa na ngano hadi miaka michache iliyopita,uwanja una taa za kutosha na zilizowekwa kwa mpangilio maalum, na pia si eneo la makazi ya watu,ndege pale huwa zinatua kati ya asubuhi hadi jioni tu,ni nadra sana ndege kupaa au kutua usiku pale,mengine jiongeze mkuu
mtoa mada amecomment kwa chuki ule uwanja wameuboresha sana na sasa hivi umetanuliwa kiasi cha ndege mpya za Air Tanzania zinatua pale
 
Back
Top Bottom