Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Kama nilivyosema jana jioni; Uvumilivu siku zote huwa una kikomo chake. Hatuwezi tena kuendelea kujificha kwenye kivuli cha kile kinachoitwa amani ni tunda la roho wakati roho zetu zikiwa na huzuni kila tuamkapo.
Wale wanaoitangaza hii Amani; ukiwatazama kwenye kwapa zao, wameficha Visu na Mapanga. Nchi gani hii ya kidemokrasia.
Ninachoweza kusema; hata hiyo Demokrasia ya Kenya, Uhuru wa Bunge lake na Mahakama ama ule wa Vyombo vya habari uliopo Kenya hivi sasa; haukupatikana kwenye sahani kama kipande cha Mkate. Kuna watu wali-sacrifice maisha yao kwa ajili ya watoto na wajukuu wao, leo hii Wakenya wanaishi raha mstarehe.
Ikumbukwe kuwa; Wakenya walichoshwa na udharimu uliokuwa unafanywa na KANU enzi zile na wakaamua kwa gharama yoyote ile kuidai Katiba Mpya iliyowasaidia kuundwa kwa Tume huru ya Uchaguzi hatimaye dhamira yao ya kuing'oa KANU ikatimia.
Muda na wakati wa kuonyeshana meno na CCM na Watu wake haupo tena; hawa walishadhamiria kung'ang'ania madaraka na hawatakuwa tayari kuona wanawekwa benchi kwa hii kitu inaitwa Uchaguzi.
Sisi tufanye siasa kupitia haya majukwaa ya chaguzi ndogo; lakini tutambue kwamba, dhamira ya CCM ni dhamira hasi iliyojaa uovu ndani yake.
Wale wanaoitangaza hii Amani; ukiwatazama kwenye kwapa zao, wameficha Visu na Mapanga. Nchi gani hii ya kidemokrasia.
Ninachoweza kusema; hata hiyo Demokrasia ya Kenya, Uhuru wa Bunge lake na Mahakama ama ule wa Vyombo vya habari uliopo Kenya hivi sasa; haukupatikana kwenye sahani kama kipande cha Mkate. Kuna watu wali-sacrifice maisha yao kwa ajili ya watoto na wajukuu wao, leo hii Wakenya wanaishi raha mstarehe.
Ikumbukwe kuwa; Wakenya walichoshwa na udharimu uliokuwa unafanywa na KANU enzi zile na wakaamua kwa gharama yoyote ile kuidai Katiba Mpya iliyowasaidia kuundwa kwa Tume huru ya Uchaguzi hatimaye dhamira yao ya kuing'oa KANU ikatimia.
Muda na wakati wa kuonyeshana meno na CCM na Watu wake haupo tena; hawa walishadhamiria kung'ang'ania madaraka na hawatakuwa tayari kuona wanawekwa benchi kwa hii kitu inaitwa Uchaguzi.
Sisi tufanye siasa kupitia haya majukwaa ya chaguzi ndogo; lakini tutambue kwamba, dhamira ya CCM ni dhamira hasi iliyojaa uovu ndani yake.