Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Tetesi za kuahirisha uchaguzi huu zinazidi kushika kasi kwa sababu ya mazingira yafuatayo:-
1) CCM hawapo tayari kushiriki uchaguzi huu baada ya kufahamu wapigakura wanaghadhabu kubwa na ya muda mrefu dhidi yao kutokana na utendaji wao duni. Uzoefu wa mwaka 1995 wa Mkoa wa Dar-Es-Salaam unawahamasisha CCM kuishinikiza NEC kuahirisha chaguzi hii.
Mwaka 1995, NEC iliahirisha chaguzi ile kutokana na uzembe wa makusudi wa NEC yenyewe katika kusambaza vifaa vya kupigia kura na ilifanya hayo yote kwa manufaa ya CCM. Uchaguzi uliporudiwa mahudhurio yalikuwa kiduchu kutokana na wapigakura kuchoshwa na usumbufu tajwa na CCM ilipeta.
2) Tetesi za TRA kukamata kura haramu za "NDIYO" kwa JK hata kabla ya makabrasha ya NEC kuwasili nchini na kusambazwa yanaleta picha ya kuwa "mtihani" umevuja na dawa ni kuurudia tu. Yaani zoezi zima lianze upya na makaratasi yenye NEMBO tofauti yakachapishwe upya. Hii itahitaji muda zaidi wa maandalizi yasiyopungua mwezi mmoja hivi na chaguzi itakuwa imeahirishwa.
Bila ya kufanya hivyo imani ya wapigakura ya kuwa uchaguzi huu ulikuwa ni huru na wa haki hautakuwepo kwa sababu hatujui ni kiasi gani ya kura haramu za kumbeba JK tayari zimo nchini na hazijashikwa na hivyo kuharamisha uhalali wa uchaguzi huu.
3) Ili kuwapooza viongozi wa kikristu ambao walilalamikia NEC kuichagua siku ya Jumapili ambayo ni siku ya ibada katika kupiga kura sasa itakuwa ni sababu sindikizi ya kuahirisha uchaguzi. NEC watachagua siku nyingine ya kati ya Jumatatu hadi Alhamisi ili kudai imezingatia malalamiko hayo!
4) Madai ya wanafunzi wa vyuo vikuu kutOshiriki chaguzi hii nayo yatatumika na NEC kama sababu nyingine sindikizi katika kuahirisha uchaguzi huu.
Zote hizi ni njama za NEC na CCM katika kutuchaguliwa viongozi ambao hatuwataki kabisa...............................CHAGUA DR. SLAA..CHAGUA CHADEMA......KUJIHAKIKISHIA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.............
1) CCM hawapo tayari kushiriki uchaguzi huu baada ya kufahamu wapigakura wanaghadhabu kubwa na ya muda mrefu dhidi yao kutokana na utendaji wao duni. Uzoefu wa mwaka 1995 wa Mkoa wa Dar-Es-Salaam unawahamasisha CCM kuishinikiza NEC kuahirisha chaguzi hii.
Mwaka 1995, NEC iliahirisha chaguzi ile kutokana na uzembe wa makusudi wa NEC yenyewe katika kusambaza vifaa vya kupigia kura na ilifanya hayo yote kwa manufaa ya CCM. Uchaguzi uliporudiwa mahudhurio yalikuwa kiduchu kutokana na wapigakura kuchoshwa na usumbufu tajwa na CCM ilipeta.
2) Tetesi za TRA kukamata kura haramu za "NDIYO" kwa JK hata kabla ya makabrasha ya NEC kuwasili nchini na kusambazwa yanaleta picha ya kuwa "mtihani" umevuja na dawa ni kuurudia tu. Yaani zoezi zima lianze upya na makaratasi yenye NEMBO tofauti yakachapishwe upya. Hii itahitaji muda zaidi wa maandalizi yasiyopungua mwezi mmoja hivi na chaguzi itakuwa imeahirishwa.
Bila ya kufanya hivyo imani ya wapigakura ya kuwa uchaguzi huu ulikuwa ni huru na wa haki hautakuwepo kwa sababu hatujui ni kiasi gani ya kura haramu za kumbeba JK tayari zimo nchini na hazijashikwa na hivyo kuharamisha uhalali wa uchaguzi huu.
3) Ili kuwapooza viongozi wa kikristu ambao walilalamikia NEC kuichagua siku ya Jumapili ambayo ni siku ya ibada katika kupiga kura sasa itakuwa ni sababu sindikizi ya kuahirisha uchaguzi. NEC watachagua siku nyingine ya kati ya Jumatatu hadi Alhamisi ili kudai imezingatia malalamiko hayo!
4) Madai ya wanafunzi wa vyuo vikuu kutOshiriki chaguzi hii nayo yatatumika na NEC kama sababu nyingine sindikizi katika kuahirisha uchaguzi huu.
Zote hizi ni njama za NEC na CCM katika kutuchaguliwa viongozi ambao hatuwataki kabisa...............................CHAGUA DR. SLAA..CHAGUA CHADEMA......KUJIHAKIKISHIA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.............