Kwanza,nyinyi mnasemwa kama vijana mnaotumika na makundi ya Urais 2015. Hivyo,nyinyi UVCCM,si wamoja. BAVICHA hawana makundi na wamebaki wamoja.
Tena,BAVICHA inathubutu hata kufanya mikutano ya hadhara kupitia viongozi wao. Wanahutubu na kusikilizwa. UVCCM mko nyuma. Mnaogopa au kukosa kitu gani. Semeni msaidiwe. Shirikini mikutano na midahalo.
Mabaraza ya Vijana vyamani ni chemchem ya kuzalisha viongozi waliopikwa wakapikika. Si mahali pa kukaa ofisini bila tija. Kukaa bila ya kufanya kazi inayostahili.
Binafsi,sijaiona tena UVCCM ya Nchimbi. Ilikuwa moto. Hii imepoa na inazidiwa ujanja na BAVICHA. Thubutuni kuhutubia na kutangaza sera za chama chetu kwa vijana. Isifikie wasemaji wa vijana nchini wawe BAVICHA.
Punguzeni au muache kabisa woga na utegemezi. BAVICHA wanawazidi ujanja. Msikubali.
Uvccm ya makonda iko bize kutukana wazee. Kuwaundia njama za kuwapiga na kula njama za kuteka watu. Mwenyekiti sadifa kazeeka mpaka shingo imegoma kupinda, katibu wake mapunda ni zigo linalosubiri pesa za mafisadi wagombea urais, vijana wa uvccm waliobaki ni watoto wa vigogo ambao muda mwingi wako nje wanakula bata. Hawa wezi wa simu,watekaji, wapigaji wa wastaafu watazungumza nini mbele ya vijana wenye akili?