UVCCM Mbeya wapinga maamuzi ya BASATA kumfungia msanii Wema Sepetu kwa muda usiojulikana

wogakuria

JF-Expert Member
Aug 15, 2018
743
1,223
*UMOJA WA VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA MBEYA-UVCCM UNAPINGA MAAMUZI YA BASATA KUMFUNGIA MSANII WEMA SEPETU KWA MUDA USIOJULOKANA.*

Akinukuliwa na moja ya chombo cha habari alipoulizwa kuhusu maoni ya UVCCM kufuatia Wema Sepetu kufungiwa na BASATA kwa kile kinachoitwa kusambaza picha na video za utupu mtandaoni, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya bwana Mashango ameeleza kwamba wamesikitishishwa sana na kitendo cha BASATA kumfungia Wema Sepetu ikiwa tayari ameshajutia na kuomba msamaha kwa jamii na mamlaka husika juu ya picha na video zilizoeneoa mtandaoni zikimuonesha akiwa mtupu.

"Kuna haja gani ya kumuadhibu mtu ambaye ametambua makosa na kuomba msamaha, tumefundishwa kusamehana inapolazimu". Ameeleza Mashango
Ameeleza kwamba sehemu kubwa ya wasanii ni vijana na wamekuwa sehemu ya ushindi wa CCM 2015 ,na kwa hivyo wanapoonewa na mamlaka yoyote UVCCM itaendelea kuwatetea kwa kadri ya uwezo wake.
"CCM imewakosea wasanii mara kadhaa wakati wa chaguzi lakini hawajawahi iadhibu kama wanavyoadhibiwa na BASATA" aliongeza Mashango.
Mashango ameeleza kwamba watawasilisha maoni yao kwa uongozi wa UVCCM Taifa ili Serikali iingilie na kuzuia manyanyaso kwa wasanii yanafanywa na BASATA.
Imetolewa na ofisi ya Katibu -UVCCM MBEYA.
Adia Rashid.
 
Wacha mimi nikae msitari wa mbele niishuhudie hii movie
giphy-1.gif
 
Hata Mimi nimeahangazwa na hatua ya BASATA, lakini nimeshangazwa zaidi na shina la CCM lililomfukuza uanachama Wema wakati kwa ccm mambo haya ni poa tu, hakuna tatizo. Kuna mmoja alikuwa anashinda uchi mitandaoni na baada ya picha zake nzuri za utupu kuonekana hadi IKULU akazawadiwa Ukuu wa Wilaya. Kwanini Wema iwe dhambi na Dc iwe sifa? UV CCM Mbeya mko sahihi, teteeni vijana.
 
Safari hii naye awe mkali afungue kesi ya zile Trillioni moja na nukta kadhaa.
 
Huyu ndio mwenyekiti wa vijana wa chama fulani ngazi ya mkoa hebu fikiria hawo wafuasi wakoje? Kama mwenyekiti anawaza hivi eti kwa kisingizio cha ushindi, hebu fikiria huyu ndio kiongozi wa nchi si yupo tayari kufanya upuuzi kwa kisingizio cha ushindi?
Tukiambiwa hawa vijana bado sana kupewa majukum tuelewe mbona wamewanguusha vijana wenzao.
Halafu hata katibu wao mkuu ashasema hawahitaji wasanii tena kwenye kampeni za uchaguzi.
 
Back
Top Bottom