Millya ndiye aliyeandika barua kwa aliyekua Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula kabla ya mwaka 2005 akilalamika kutishwa na Lowassa kuwa aache kumsaliti kwani yeye ni ndugu yake na anapaswa kumuunga mkono kama anataka mambo yake yanyooke. Millya alimwambia Mangula kwamba Lowassa alimwambia kwamba ameshakubaliana na Rais Mkapa kwamba JK atakua Rais na yeye (Lowassa) atakua Waziri Mkuu na Millya ataaibika. Lowassa akamsihi ajinge naye na asimsaliti.
Mazungumzo hayo yalifanyika nyumbani kwa Lowassa baada ya Millya na viongozi wenzake wa Dodoma, Kilimanjaro, Dar es Salaam na mikoa mingine kutoa matamko kumpinga Kikwete. Baadae ni Millya ambaye amekuja kumbana Lowassa na alionekana kama tishio kuelekea 2010 kabla ya kubwaga manyanga na kumwachia na hatimaye kumuunga mkono Lowassa. Je, Millya ametishwa tena? Na safari hii ameambiwa nani ni Rais na nani PM? Je, Millya hataki kupoteza tena kama alivyompinga JK? Ama 2005 alitumwa na Lowassa kumpinga JK kiana na sasa kazi iliisha na anapaswa sasa kuingia ndani tena?
Jamani kama unaamini kwamba hili tamko ni halali na Lowassa ameonewa, karibu sana utapata majibu humu