UVCCM Arusha watoa tamko zito!

UVCCM Arusha watoa tamko zito!

Itatuchukuwa muda gani kugundua kwamba kiongozi wa nchi kisha pata tatizo la akili?
Je, ni nani anastahili kuamua kwamba afya ya Rais sasa hivi haimuruhusu kuendelela na kazi yake?

Sioni dalili kwamba sasa hivi kuna kiongozi wa nchi.

Ina maana pamoja na kikombe cha babu bado ubongo haujakaa sawa? Basi tumekwisha yaani TZ sasa imekuwa kama treni ambayo imeshatoka kwenye reli.Ukiangalia makamu naye ndiyo walewale.
 
Hawa vijana wa CCM nadhani kama akili zao hazitegei ilibidi wajiulize mambo ya msingi kama alivyowashauri Aloyce Kimaro kwamba:-

1.Wafanye tathmini ni kwanini vijana wengi nchi hii wapo CHADEMA? na wamekipa kisogo chama cha mazezeta na wao kama vijana wachukue lawama zao kwamba wamefanya jitihada gani kuwashawishi vijana nchini kuipenda na Kuishabikia CCM?

2.Pili ilitakiwa vijana hawa wafanye tathmini ni vijana wangapi kutoka UVCCM ambao waligombea uwakilishi au ubunge na kufanikiwa kupata ridhaa ya wananchi? na kama hakuna wa-source out tatizo ni chama ndio kina ukiritimba dhidi ya vijana au Jamii (Wananchi) hawawaamini tena vijana wa CCM
My Take:UVCCM imebaki story...kwani wameuza wenyewe uhuru wao kwa mafisadi kama alivyouza uhuru wake kijana mmoja aliyekuwa maarufu sana CDM..Waongeaji wote wa UVCCM na vizabizabina vyao kuna fisadi nyuma yake

1. Hussein Bashe..The former NMB Employee and Mzumbe President..anakiri kuwa Director wa Kampuni ya Rostam
2.Ridhiwani J Kikwete...The former IMMMA E mployee ni mtoto wa damu wa M.K.W.E.R.E mtu ambaye kila mtanzania anamlilia kwa kumsababishia maumivu haya ya kiuchumi.
3.Ole Millya...Huyu ni kama Tarishi wa ndani wa E.L Mtu ambaye yuko nyuma ya karibu kila ovu linalosababishwa na binadmu ktk nchi hii.

Wasalaaam.
 
Millya ndiye aliyeandika barua kwa aliyekua Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula kabla ya mwaka 2005 akilalamika kutishwa na Lowassa kuwa aache kumsaliti kwani yeye ni ndugu yake na anapaswa kumuunga mkono kama anataka mambo yake yanyooke. Millya alimwambia Mangula kwamba Lowassa alimwambia kwamba ameshakubaliana na Rais Mkapa kwamba JK atakua Rais na yeye (Lowassa) atakua Waziri Mkuu na Millya ataaibika. Lowassa akamsihi ajinge naye na asimsaliti.

Mazungumzo hayo yalifanyika nyumbani kwa Lowassa baada ya Millya na viongozi wenzake wa Dodoma, Kilimanjaro, Dar es Salaam na mikoa mingine kutoa matamko kumpinga Kikwete. Baadae ni Millya ambaye amekuja kumbana Lowassa na alionekana kama tishio kuelekea 2010 kabla ya kubwaga manyanga na kumwachia na hatimaye kumuunga mkono Lowassa. Je, Millya ametishwa tena? Na safari hii ameambiwa nani ni Rais na nani PM? Je, Millya hataki kupoteza tena kama alivyompinga JK? Ama 2005 alitumwa na Lowassa kumpinga JK kiana na sasa kazi iliisha na anapaswa sasa kuingia ndani tena?

Jamani kama unaamini kwamba hili tamko ni halali na Lowassa ameonewa, karibu sana utapata majibu humu

Mambo ya ndani ya Chama hayatuhusu sisi wengine, mipango yao ni yao kwani pilipili usizozia zinakuwashia nini?
Ninachokubaliana na tamko hili limetofautiana mno na matamko ya umoja wa vijana taifa na ya baadhi ya kanda. Tamko hili limetulia, hakuna matusi au dharau kama tulivyoshuhudia katika matamko yaliyotangulia.

Wamejitahidi kutoa tokuduku lao katika mambo ya msingi ambayo wewe na mimi tunayaelewa na ni rahisi kuelewa madai yako.

Wanajamii forums licha ya kushabikia vyama tuangalie ajenda zenye manufaa kwa taifa bila kuangalia sura na itikadi za mtu au chama, huo ndio ukomavu wa kisiasa.
 
"aCtion AND REACTION ARE EQUAL AND IN OPPOSITE DIRECTION"
action was against CDM on ukabila, now equal reaction are facing them.
Lets see what will happen, will they violate newton's third Law?
 
Back
Top Bottom