Uuzwaji holela wa dawa za Mitishamba udhibitiwe, nyingine ni hatari kwa afya ya binadamu!

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,848
15,252
Kumekuwa na ongezeko kubwa mtaani la uuzwaji wa dawa za mitishamba, dawa hizo hazina vipimo maalumu na wala haijulikani ni aina gani ya miti.

Mfano mzuri unakuta mmasai ameweka dawa kwenye galoni moja huku amebeba karatasi maalumu yenye aina za magonjwa karibu 200 ambayo yanatibika na dawa iliyopo kwenye galoni.

Dawa moja tu utaambiwa inatibu magonjwa kama vile presha, kusafisha damu,Kichwa, UTI. Uvimbe, malaria. Homa ya matumbo fungus, kisukari, tambazi. Ini nk

Ongezeka la dawa hizo zimekuwa kila mahala hadi kufikia wengine kufungua maduka ya dawa za asili lakini ukifuatilia wengi wa waliotibiwa kupitia dawa zao hawakupona wala kupata nafuu.

Serikali nayo imekuwa kimya ikiwaacha wananchi kufanya chochote bila uthibiti maalumu wa kuwaokoa raia wake. Badala ya dawa hizo kwenda kutibu tatizo inaenda kuanzisha tatizo lingine.
DSC_0867.JPG

Huko instagram nako kumegeuka serikali nyingine maana wasomi na wasio wasomi wanatafuta namna ya kuishi kwa kuuza dawa za kila aina ambazo hawana hata ujuzi nazo wao ni ilimradi pesa imeingia mfukoni wewe mgonjwa utajijua mwenyewe mbele ya safari.
 
Wapigaji wamegundua kitu. Wakitaka dawa zao za miti shamba zotoke kwa kasi wanatangaza kua zinaongeza nguvu za kiume.

Wamasai nao wameingia katika ujanja huo. Wenyewe maisha yao wana pilika nyinga. Wanatembea kwa miguu umbali mrefu na wanakula vitu natural. Wengi wao hasa vijana hawanaga viriba tumbo

Sasa badala kushauri watu juu ya life style yenye kuleta afya wao wanadanganya kuwauzia mitishamba😀😀😀
 
Kuna mtu alikula vile vimbegu vinavyouzwa na wamasai vya kupunguza unene,aliharisha mpk pulu akawa anairudisha na kidole kwa ndani.
Pole sana yaani mpaka ulikuwa unairudisha naniliu kwa vidiole siku nyengine niite Mimi niirudishe
 
Kuna jamaa yangu tunafanya kazi pamoja anapenda sana dawa za miti shamba, kuna moja nimeona ameinunua nikaona niisome maelezo yake daaah inatubu kila aina ya ugonjwa unaoujua.
 
Wapigaji wamegundua kitu. Wakitaka dawa zao za miti shamba zotoke kwa kasi wanatangaza kua zinaongeza nguvu za kiume.

Wamasai nao wameingia katika ujanja huo. Wenyewe maisha yao wana pilika nyinga. Wanatembea kwa miguu umbali mrefu na wanakula vitu natural. Wengi wao hasa vijana hawanaga viriba tumbo

Sasa badala kushauri watu juu ya life style yenye kuleta afya wao wanadanganya kuwauzia mitishamba😀😀😀
Wamasai wa sasa na wenyewe wamekuja kupenda pesa sana, halafu wanapenda kuuza hizo dawa huku wamevaa rubega zao ili waaminike kwa haraka
 
... uholela hadi kwenye mambo ya msingi kama afya za wananchi ni excellent indicator of absolute poverty of a society.

Hivi yale mabanda ya kujifukiza yaliyoenea nchi nzima miezi michache iliyopita bado yapo?
 
Huwa nashangaa yakitokea maoneshobyoyote

1. Sabasaba ndio hao wamejazana

2. Nanenane wamejazana wao

3. Maonesho ya biashara wao wamejaa

4. Maonesho ya afrika mashariki wamejaa

6. Syrian exhibition nao wapo
 
Back
Top Bottom