A
Anonymous
Guest
Muonekano wa sehemu ya Dampo Bakhresa ulivyo wakati wa msimu huu wa kiangazi.
Kwa wakati huo asilimia kubwa ya eneo lilikuwa ni pori na hakukuwa na makazi ya watu karibu na eneo hilo la Dampo.
Miaka ilivyozidi kwenda, Vikindu na maeneo yake ya jirani (yaliyomo ndani ya Vikindu) yakawa yanakua, idadi ya watu ikaongezeka kutokana na mwingiliano wa shughuli mbalimbali.
Wakati huohuo, Dampo la Bakhresa lipo wazi, mvua ikinyesha maji yanatirirka kuelekea kwenye makazi ya watu hasa wa Kijiji cha Kazole ambacho ni moja ya vijiji vinachopatikana ndani ya Kata ya Vikindu.
Baadhi yetu Wanakijiji wa Kazole tukafanya mpango wa kukutana na uongozi wa Bakhresa kuwashauri kuwa wajenge uzio ili kuzuia maji yanayoenda kwenye makazi ya watu.
Hoja hiyo ikawa inapigwa danadana na imeendelea kupigwa danadana hadi leo, watendaji wa upande wa Bakhresa wakawa wanadai wao waliingia mkataba na Vikindu na sio Kijiji cha Kazole.
Ikumbukwe Kazole ilipewa hadhi ya kuwa Kijiji kinachojitegemea Mwaka 2014, lakini mikataba ya Dambo yote ilisainiwa Vikindu, hivyo hatuna cha kufanya.
Dambo ambalo ninalizingumzia hapa, sijui lina sumu gani au zinawekwa dawa gani kwa kuwa hakuna mdudu anayesogea kwenye taka hizo, zinaoza na kunuka lakini Wadudu hawasogei.
Sasa Watoto wa mtaani wanapita na kushikashika vitu kwenye Dampo hilo, hapo nadhani unaweza kufikiria kuhusu hatari kwa afya zao ikoje.
Kingine ni kuwa wakati wa msimu wa matunda kama maembe au machungwa au matunda mengine ambayo yanatumika zaidi kwenye viwanda, ndipo ambapo uchafu unakuwa mwingi, kuna wakati inafikia hadi lori 30 hadi 40 kwa siku zinazokuja kumwga taka hapo.
Maembe mabovu yanayotupwa huuzwa tena mtaani
Taarifa nyingine ni kuwa yale maembe na machungwa ambayo yanaonekana hayafai na kwenda kutupwa katika Dampo hilo, kuna baadhi ya watu ambao sio waaminifu wanayachukua yale ambayo yanaonekana kuwa na muonekano mzuri kisha kwenda kuuzwa mitaani kwa bei rahisi hasa mitaa ya Temeke.
Wito wetu
Wito wetu sisi Wananchi wa Kazole na maeneo ya Vikindu na jirani, tunaomba Serikali ifuatilie kinachoendelea, kwani tuna wakati mgumu wa afya zetu kutokana na Dampo hilo.
Pia wanaochukua matunda yanayotupwa na kwenda kuyauza mitaani Dar es Salaam na kwingineko wanahatarisha afya za walaji kwa kuwa matunda hayo si salama kwa afya na hayafai kuliwa.