Utumiaji wa makampuni ya consultants katika miradi ya maji ni upigaji na matumizi mabaya ya fedha za Umma

Kuna tetesi nimesikia wizara ya maji inataka kusaini mikataba na makampuni ya consultants kwa ajili ya usanifu wa miradi ya maji na usimamizi wake.

Je inakuaje serikali itumie hizi kampuni wakati inaweza tumia wataalam wa ndani?

Inakuaje serikali iwe tayari kulipa kampuni ya consultants mabilioni ya pesa wakati kazi hiyo inaweza fanyika kwa gharama ndogo kwa kutumia wataalam wa ndani?

Yani mradi wa kijiji kimoja unaajiri kampuni isanifu kweli?

NB: Nashauri hiyo mikataba ya consultants mnayotaka kusaini mwaka huu msisaini kama kweli mnajali fedha za umma wa watanzania!!
Lakini kingine mara nyingi wadhamini ndiyo huwa wanaweka sharti la uwepo wa Consultant kwa ajili ya kudhibiti baadhi ya mambo fulani. Haya tumeona sana.
 
Kwani wataalamu wa ndani hawawezi kuwa consultants? Mbona Mayanga construction ilifanya consultancies nyingi ikiwemo ujenzi wa Chato airport na hukulalamika?
Mayanga ni contractor (mjenzi) na sio consultant (mtaalam mshauri).

Kuna tofauti kati ya consultant na contractor.
 
Wewe ndo jitathmin mkuu, wataala wa ndani maana yake ni ma engineer waajiriwa wa serikali, wapo wanashinda whatsap tu hawana kaxi
Sio tu hawana kazi mbaya zaidi unaenda kumpa consultant asanifu kamradi kakuhudumia kata moja mwisho wa siku unaua morali ya watumishi wako.
 
Lakini kingine mara nyingi wadhamini ndiyo huwa wanaweka sharti la uwepo wa Consultant kwa ajili ya kudhibiti baadhi ya mambo fulani. Haya tumeona sana.
Hii oda ilitoka juu, maana mikoa na wilaya walikua na option ya kukataa lakini sijui ikatokea nini mpaka wale walio kataa wakajikuta imewabidi wakubali.

Haikua ni sharti la mikopo bali ni "amri toka juu".
 
Miradi ni hii midogo ya vijiji viwili vitatu. Hata hiyo mikubwa mbona imefanywa na mainjinia wa serikali kwa miaka nenda rudi? Why now?

Mbaya zaidi hata kamradi kadogo wanapewa na wanatakiwa kulipwa mabilioni ya pesa kukasanifu kazi ambayo hata mwanafunzi aliyemaliza chuo anaweza fanya tena gharama ndogo kabisa!
Mkuu sema tu utakuwa umenyang'anywa tonge mdomini. Utaratibu wa kutumia consultants kwenye miradi ni utaratibu wa dunia nzima.

Pili nadhani hujui maana ya wataalamu wa ndani. Tunaposema wataalamu wa ndani hatuna maana walio ajiriwa serikalini, bali tuna maanisha wa Tanzania. Sisi wataalamu wote bila kujari tunafanyaka kazi private sector, tumejiajiri, au tumeajiriwa serikalni...wote ni wa Taaalamu wa ndani. Tuna nafasi sawa katika kujenga Taifa letu.

Hivyo serikali natumia watu wake kelele ya nini?

Kama unaona ma consultant wanafaidi basi acha kazi serikalini ufungue consulting firm.
 
Mkuu sema tu utakuwa umenyang'anywa tonge mdomini. Utaratibu wa kutumia consultants kwenye miradi ni utaratibu wa dunia nzima.

Pili nadhani hujui maana ya wataalamu wa ndani. Tunaposema wataalamu wa ndani hatuna maana walio ajiriwa serikalini, bali tuna maanisha wa Tanzania. Sisi wataalamu wote bila kujari tunafanyaka kazi private sector, tumejiajiri, au tumeajiriwa serikalni...wote ni wa Taaalamu wa ndani. Tuna nafasi sawa katika kujenga Taifa letu.

Hivyo serikali natumia watu wake kelele ya nini?

Kama unaona ma consultant wanafaidi basi acha kazi serikalini ufungue consulting firm.

Kwa hiyo kwa akili yako fupi unaona ni sawa kulipa bilions kwa kitu unachopata na umekua ukikipata kwa ubora uleule kwa less than 50million?

NB: Mimi sio mtumishi wa serikali, na kama ningekua nisingeeza ruhusu ujinga kama huu.
 
Nadhani mtoa hoja hajui umuhimu wa consults na hajui wanapatikana kwa njia gani.

Huwezi kusema tu kwamba mradi wa kijiji kimoja consultant analipwa mabilioni ya pesa. Wakati wa kuomba kazi consultants wanaandika technical proposal na financial proposal zao. Team ya client ambao ni wahandisi, watu wa ugavi na kada zingine wanapitia proposal hizo wakianza na technical kisha financial na kupata consultant wanayemhitaji kwa vigezo vya ubora wa kazi, wataalam alionao na gharama. Ukiona bei ya chini ya Ma-consultant wote walioomba imeangukia kwenye mabilioni licha ya mradi kuwa wa kijiji kimoja, basi jua kuna changamoto ya ku-design mradi huo na hivyo utahitaji aina ya wataalam wengi na muda mwingi. Mwisho wa siku wenye kufanya maamuzi ni wale wa serikalini kwa niaba ya client.

Ni ukweli usiopingika kwamba miradi mingi lazima iwe na team ya kuanda mfano
1. Engineers kadhaa kwa levels na kada tofauti
Mfano Water engineer, electromechanical engineer kama si mradi wa gravity
2. Hydrologists au Geo-hydrologist kama utalazimika kustudy chanzo
3. Land Surveyor
4. Quantity surveyor
5. CAD technician
6. Environmental expert
7. Social expert
8. Engineer mkuu atakaye fanya QA ya kazi

Watu wote hawa huwezi kuwakuta kwa pamoja kwenye ofisi ya wilaya ruwasa. Pale mara nyingi utakuta
1. Engineer 1
2. Technicians 2 akibahatika
3. Social expert au environmental expert
kwa pamoja wana simamia vijiji vyote vya wilaya yao. Ukienda mkoani ni vilevile. Ni nadra sana kuwakuta hao wengine niliowataja kwenye eneo moja. Ukiwa na miradi inayoendelea vijiji kadhaa wilayani, na mkoani kwa nchi nzima utakuta kila engineer yupo busy na miradi yake, hii habari kwa kuunda team ya pamoja utawatoa wapi watu wa kutoshereza. Timu tu za procurement ilibidi ifanyiwe HQ kabla ya kuhamishiwa kwenye kanda na mikoani na wakati mwingine kwenye mamlaka. Wahasibu wa kila wilaya hawajapatikana inabidi mkoa ndo uhudumie wilaya zote. Unapata wapi ujasiri wa kuamini wilaya inaweza kujitegemea kusanifu mradi wake huku ukijua hawana resources za kutosha na ikiwa ni miradi ya vijiji kila wilaya/mkoa hamuwezi kuazimana.

Ushauri wangu
1. Fanya internal assessment ujiridhishe ikiwa uwezo huo upo. Usi-assume kwamba mradi wa kijiji ni kulaza tu mabomba ya maji. Kuna vitu vingi vya kustudy na ku-consider wakati wa design ili mradi wako uwe endelevu. Miradi mingi ya Force Account ilikosa ubora kwasababu ya kutokuwa na human resource za kutosha kila mmoja kupitia kwa eneo lake wakati wa design na kuhakikisha usimamizi unakuwa madhubuti wakati wa ujenzi.
2. Wakati wa kutafuta consultant hakikisha mnakuwa na baseline ya gharama na kuhakikisheni mmetoa details za kutosha kwenye tender documents.

Kumbuka engineer wa wilaya ndo wasimamizi wa kazi zote za maji wilayani. Ikiwa yupo mmoja tu na huyo ukam-keep busy na design si shughuli zingine za usimamizi na administration zitasimama!
 
Nadhani mtoa hoja hajui umuhimu wa consults na hajui wanapatikana kwa njia gani.

Huwezi kusema tu kwamba mradi wa kijiji kimoja consultant analipwa mabilioni ya pesa. Wakati wa kuomba kazi consultants wanaandika technical proposal na financial proposal zao. Team ya client ambao ni wahandisi, watu wa ugavi na kada zingine wanapitia proposal hizo wakianza na technical kisha financial na kupata consultant wanayemhitaji kwa vigezo vya ubora wa kazi, wataalam alionao na gharama. Ukiona bei ya chini ya Ma-consultant wote walioomba imeangukia kwenye mabilioni licha ya mradi kuwa wa kijiji kimoja, basi jua kuna changamoto ya ku-design mradi huo na hivyo utahitaji aina ya wataalam wengi na muda mwingi. Mwisho wa siku wenye kufanya maamuzi ni wale wa serikalini kwa niaba ya client.

Ni ukweli usiopingika kwamba miradi mingi lazima iwe na team ya kuanda mfano
1. Engineers kadhaa kwa levels na kada tofauti
Mfano Water engineer, electromechanical engineer kama si mradi wa gravity
2. Hydrologists au Geo-hydrologist kama utalazimika kustudy chanzo
3. Land Surveyor
4. Quantity surveyor
5. CAD technician
6. Environmental expert
7. Social expert
8. Engineer mkuu atakaye fanya QA ya kazi

Watu wote hawa huwezi kuwakuta kwa pamoja kwenye ofisi ya wilaya ruwasa. Pale mara nyingi utakuta
1. Engineer 1
2. Technicians 2 akibahatika
3. Social expert au environmental expert
kwa pamoja wana simamia vijiji vyote vya wilaya yao. Ukienda mkoani ni vilevile. Ni nadra sana kuwakuta hao wengine niliowataja kwenye eneo moja. Ukiwa na miradi inayoendelea vijiji kadhaa wilayani, na mkoani kwa nchi nzima utakuta kila engineer yupo busy na miradi yake, hii habari kwa kuunda team ya pamoja utawatoa wapi watu wa kutoshereza. Timu tu za procurement ilibidi ifanyiwe HQ kabla ya kuhamishiwa kwenye kanda na mikoani na wakati mwingine kwenye mamlaka. Wahasibu wa kila wilaya hawajapatikana inabidi mkoa ndo uhudumie wilaya zote. Unapata wapi ujasiri wa kuamini wilaya inaweza kujitegemea kusanifu mradi wake huku ukijua hawana resources za kutosha na ikiwa ni miradi ya vijiji kila wilaya/mkoa hamuwezi kuazimana.

Ushauri wangu
1. Fanya internal assessment ujiridhishe ikiwa uwezo huo upo. Usi-assume kwamba mradi wa kijiji ni kulaza tu mabomba ya maji. Kuna vitu vingi vya kustudy na ku-consider wakati wa design ili mradi wako uwe endelevu. Miradi mingi ya Force Account ilikosa ubora kwasababu ya kutokuwa na human resource za kutosha kila mmoja kupitia kwa eneo lake wakati wa design na kuhakikisha usimamizi unakuwa madhubuti wakati wa ujenzi.
2. Wakati wa kutafuta consultant hakikisha mnakuwa na baseline ya gharama na kuhakikisheni mmetoa details za kutosha kwenye tender documents.

Kumbuka engineer wa wilaya ndo wasimamizi wa kazi zote za maji wilayani. Ikiwa yupo mmoja tu na huyo ukam-keep busy na design si shughuli zingine za usimamizi na administration zitasimama!
Miradi ya maji imekua ikisanifiwa na mainjinia kutoka wilayani, mikoani na wizarani kwa miaka zaidi ya 10! Why today?

Pia hao wataalam ulio wasema unataka kutu aminisha serikalini hakuna?

Yani hakuna masaveya? Hakuna VAD technicians? Hakua hydrogeologists? Hakuna wataalam wa mazingira nk nk? Mkuu uko serious?
 
Back
Top Bottom