Upigaji wa Fedha za Umma mamlaka zimeshindwa kuzisimamia au wapigaji wanashirikiana na mamlaka?

MKWEAMINAZI

JF-Expert Member
May 28, 2023
930
1,299
Hakika inaogopesha na kusikitisha sana kuona jinsi fedha za umma ambazo ni kodi za masikini wananchi wanazolipa kwa kukamuliwa na fedha za mikopo tunazokopa toka nje zinavyoliwa na wajanja watendaji wa umma.

Tumemshuhudia Mh. Waziri Mkuu Mzee Majaliwa katika ziara zake akipambana na ufisadi mkubwa unaofanywa katika halmashauri zetu, ufisadi ambao inaonekana unaanzia Hazina unakuja TAMISEMI kisha halmashauri. Hazina wanatuma fedha zisizo na maelezo kwenda halmashauri kupitia TAMISEMI ambao nao hawaulizi hazina kwanini hizi fedha hazina maelezo!

Ushauri kwa serikali

1. Huu mtandao ni mkubwa wahusika wamejipanga mtandao unawahusu Hazina, TAMISEMI na Halmashauri zote.

2. Ajira za kuteua ma-DED na ma-DAS kutoka UVCCM zinachangia sana Halmashauri kushindwa kusimamia fedha na miradi mbalimbali ajira zitangazwe watumishi waliopo popote na wananchi wengine waombe ili kupata watendaji wenye sifa na uwezo wa kusimamia fedha na miradi tukiendelea kuteuana kiitikadi huu upigaji hautakoma.

Vile vile tunauliza ni hatua gani zimekwishachukuliwa kwa waliotajwa katika report ya CAG au sio lazima?

576809861.jpg
20230428_142210.jpg
millardayo_1680111897952155.jpg
bavicha.tz_168097986085523.jpg
 
Watanzania wengi ni wezi ukiwakabidhi ofisi tu kama hauna sheria nzuri umekwisha..
Umasikini na malezi ndio sababu..
 
Hakika inaogopesha na kusikitisha sana kuona jinsi fedha za umma ambazo ni kodi za masikini wananchi wanazolipa kwa kukamuliwa na fedha za mikopo tunazokopa toka nje zinavyoliwa na wajanja watendaji wa umma.

Tumemshuhudia Mh. Waziri Mkuu Mzee Majaliwa katika ziara zake akipambana na ufisadi mkubwa unaofanywa katika halmashauri zetu, ufisadi ambao inaonekana unaanzia Hazina unakuja TAMISEMI kisha halmashauri. Hazina wanatuma fedha zisizo na maelezo kwenda halmashauri kupitia TAMISEMI ambao nao hawaulizi hazina kwanini hizi fedha hazina maelezo!

Ushauri kwa serikali

1. Huu mtandao ni mkubwa wahusika wamejipanga mtandao unawahusu Hazina, TAMISEMI na Halmashauri zote.

2. Ajira za kuteua ma-DED na ma-DAS kutoka UVCCM zinachangia sana Halmashauri kushindwa kusimamia fedha na miradi mbalimbali ajira zitangazwe watumishi waliopo popote na wananchi wengine waombe ili kupata watendaji wenye sifa na uwezo wa kusimamia fedha na miradi tukiendelea kuteuana kiitikadi huu upigaji hautakoma.

Vile vile tunauliza ni hatua gani zimekwishachukuliwa kwa waliotajwa katika report ya CAG au sio lazima?

View attachment 2760819View attachment 2760823View attachment 2760825View attachment 2760827
Huez tenganisha CCM na upigaj+ufisadi!! Ishi humo
 
Tuko Vibaya Tumevurugwa Watu Mpaka Wanachukua Makusanyo Ya Miezi Miwili Bhalaa
Kuchota Mpaka Wenyewe Waliolala Wameamka
Babu Jinga
 
Hakika inaogopesha na kusikitisha sana kuona jinsi fedha za umma ambazo ni kodi za masikini wananchi wanazolipa kwa kukamuliwa na fedha za mikopo tunazokopa toka nje zinavyoliwa na wajanja watendaji wa umma.

Tumemshuhudia Mh. Waziri Mkuu Mzee Majaliwa katika ziara zake akipambana na ufisadi mkubwa unaofanywa katika halmashauri zetu, ufisadi ambao inaonekana unaanzia Hazina unakuja TAMISEMI kisha halmashauri. Hazina wanatuma fedha zisizo na maelezo kwenda halmashauri kupitia TAMISEMI ambao nao hawaulizi hazina kwanini hizi fedha hazina maelezo!

Ushauri kwa serikali

1. Huu mtandao ni mkubwa wahusika wamejipanga mtandao unawahusu Hazina, TAMISEMI na Halmashauri zote.

2. Ajira za kuteua ma-DED na ma-DAS kutoka UVCCM zinachangia sana Halmashauri kushindwa kusimamia fedha na miradi mbalimbali ajira zitangazwe watumishi waliopo popote na wananchi wengine waombe ili kupata watendaji wenye sifa na uwezo wa kusimamia fedha na miradi tukiendelea kuteuana kiitikadi huu upigaji hautakoma.

Vile vile tunauliza ni hatua gani zimekwishachukuliwa kwa waliotajwa katika report ya CAG au sio lazima?

View attachment 2760819View attachment 2760823View attachment 2760825View attachment 2760827
Niliwahoji vijana wapatao 10 wa Chuo kikuu kuhusu hali hii na siasa kwa jumla nchini. Inasikitisha mtazamo na msimamo wao. Wote kumi wanamuunga mkono Rais Samia pamoja na CCM ktk hatua za kupambania uchumi anazochukuwa. Hawawaelewi kabisa Chadema na Sauti ya Watanzania akina mzee Dr. Slaa na wenzake; wanasema wote ni wale wale tu wale wale wanatafuta "kupiga", ati, mbona Nchi iko vizuri tu!
Hao ndio wasomi wetu, product ya akina profesa Mkumbo, Paramagamba, etc.
Nikawahoji juu ya "upigaji" uliokithiri Serikalini na taasisi zake:
1. Wote hawakuonesha kujali wala kusikitishwa na hali hiyo.
2. 8 walipongeza "upigaji" na "wapigaji" kuwa ndiyo akili na hekima, kwamba, "likiwaka anika, likizima anua", kwamba, ponda mali kufa kwaja kwani maisha yenyewe haya ni mafupi.
Nchi za Afrika bado tuna safari ndefu ya kwenda na lazima kwa hali ya uchuni ilivyo sasa huko "majuu", lazima watarudi kututawala na kututumikisha maana viongozi wetu inaonesha wazi walikwishainua mikono na kusalimu amri.
 
Back
Top Bottom