UTT AMIS vs DSE – Ni ipi bora kwa uwekezaji? Nisaidiane kufahamu

UTT AMIS vs DSE – Ni ipi bora kwa uwekezaji? Nisaidiane kufahamu

888I

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
445
Reaction score
553
Wakuu,
Nimekuwa nikijifunza kuhusu njia mbalimbali za uwekezaji hapa Tanzania, na nimekutana na majina mawili makubwa: UTT AMIS na DSE. Ningependa kuelewa tofauti zao, faida, na changamoto kabla sijafanya maamuzi.

Nimefahamu haya
1. UTT AMIS (Unit Trust of Tanzania – Asset Management and Investor Services)
Ni taasisi ya serikali inayosimamia mfuko wa pamoja wa uwekezaji (unit trust funds).

2. DSE (Dar es Salaam Stock Exchange)
Ni soko rasmi la hisa Tanzania.
Unanunua na kuuza hisa za makampuni yaliyosajiliwa, pamoja na hati fungani na bidhaa nyingine za kifedha.

Swali langu kwa wakuu wa JamiiForums:
Ni ipi kati ya hizi mbili imewasaidia zaidi kwenye malengo ya kifedha?
Je, kwa mtu anayeanza, ni UTT AMIS, au ni DSE?

Changamoto na hatari za kila upande ni zipi?
Ningependa kusikia maoni yenu, uzoefu wenu binafsi, na ushauri kwa mtu anayetaka kuanza safari ya uwekezaji...
 
Kwa bado ni kijana below 45 go for DSE nunua hisa za CRDB, Afriprise, Nicol and NMB but if you are above 45 go for UTT. Why nasema hivi? Hisa zina tabia ya kufluctuate sana…… unaweza kupata faida sana kuliko UTT na Bonds ila sometimes unaweza pata hasara kubwa au kupoteza mtaji. UTT ni sehemu isiyo na mawimbi makubwa so kama ni mtu usiyependa kashikashi go for it ila faida ni ndogo ~12% per year. Chaguo ni lako
 
Mkuu umeeleza kila kitu
Kwa bado ni kijana below 45 go for DSE nunua hisa za CRDB, Afriprise, Nicol and NMB but if you are above 45 go for UTT. Why nasema hivi? Hisa zina tabia ya kufluctuate sana…… unaweza kupata faida sana kuliko UTT na Bonds ila sometimes unaweza pata hasara kubwa au kupoteza mtaji. UTT ni sehemu isiyo na mawimbi makubwa so kama ni mtu usiyependa kashikashi go for it ila faida ni ndogo ~12% per year. Chaguo ni lak
 
Kwa bado ni kijana below 45 go for DSE nunua hisa za CRDB, Afriprise, Nicol and NMB but if you are above 45 go for UTT. Why nasema hivi? Hisa zina tabia ya kufluctuate sana…… unaweza kupata faida sana kuliko UTT na Bonds ila sometimes unaweza pata hasara kubwa au kupoteza mtaji. UTT ni sehemu isiyo na mawimbi makubwa so kama ni mtu usiyependa kashikashi go for it ila faida ni ndogo ~12% per year. Chaguo ni lako
Okay shukrani sana
 
Inategemea na uwezo wako wa kuhimili risks, ila kama unataka uwezekano wa kupata faida kubwa kwa muda mfupi, nunua hisa zinazofanya vizuri​
 
Nilifungua account UTT na M-Wekeza kote nikaweka kiwango sawa cha uwekezaji. UTT nilifungua Liquid. Baada ya mwezi M-Wekeza nilipata faida ya 42,000 na UTT nilipata 11,000.
 
Nilifungua account UTT na M-Wekeza kote nikaweka kiwango sawa cha uwekezaji. UTT nilifungua Liquid. Baada ya mwezi M-Wekeza nilipata faida ya 42,000 na UTT nilipata 11,000.
Inawezekana. Uliweka kwa muda gani maana riba za miezi zinatofautiana mpaka mwisho unapata wastani 10% 11% 12% 13% n.k
 
Kwa bado ni kijana below 45 go for DSE nunua hisa za CRDB, Afriprise, Nicol and NMB but if you are above 45 go for UTT. Why nasema hivi? Hisa zina tabia ya kufluctuate sana…… unaweza kupata faida sana kuliko UTT na Bonds ila sometimes unaweza pata hasara kubwa au kupoteza mtaji. UTT ni sehemu isiyo na mawimbi makubwa so kama ni mtu usiyependa kashikashi go for it ila faida ni ndogo ~12% per year. Chaguo ni lako
Nje ya mada mkuu, unaweza kuni recommend nisome vitabu gani ili nipate uelewa zaidi juu ya uwekezaji hass katika masoko ya Hisa kama DSE. Kutokana na Jibu lako nahisi unaweza kuwa na uelewa wa haya mambo. Asante.
 
Inawezekana. Uliweka kwa muda gani maana riba za miezi zinatofautiana mpaka mwisho unapata wastani 10% 11% 12% 13% n.k

Mwezi mmoja tu. Lengo lilikuwa kuwa na accounts zote mbili ndo kugundua kwingine napata faida zaidi
 
Mwezi mmoja tu. Lengo lilikuwa kuwa na accounts zote mbili ndo kugundua kwingine napata faida zaidi
Mwezi mmoja hautoshi kufanya tatmnini angalau mwaka mmoja ambapo kivyovyote nilazima UTT iwe juu kutokana na compound interest ya kila.siku
 
Nilifungua account UTT na M-Wekeza kote nikaweka kiwango sawa cha uwekezaji. UTT nilifungua Liquid. Baada ya mwezi M-Wekeza nilipata faida ya 42,000 na UTT nilipata 11,000.
uliweka sh ngap?
 
Kwa bado ni kijana below 45 go for DSE nunua hisa za CRDB, Afriprise, Nicol and NMB but if you are above 45 go for UTT. Why nasema hivi? Hisa zina tabia ya kufluctuate sana…… unaweza kupata faida sana kuliko UTT na Bonds ila sometimes unaweza pata hasara kubwa au kupoteza mtaji. UTT ni sehemu isiyo na mawimbi makubwa so kama ni mtu usiyependa kashikashi go for it ila faida ni ndogo ~12% per year. Chaguo ni lako
Kwenye bonds hasara kubwa au kupoteza mtaji vinatokeaje mkùu?
 
Nje ya mada mkuu, unaweza kuni recommend nisome vitabu gani ili nipate uelewa zaidi juu ya uwekezaji hass katika masoko ya Hisa kama DSE. Kutokana na Jibu lako nahisi unaweza kuwa na uelewa wa haya mambo. Asante.
Five rules for successful stock investing - Pat Dorsey
Just keep buying - Nick Migguel
Pia mfuatilie mtaalamu anaitwa Emillian Busara kuna mafundisho yake mengi youtube pia kuna vitabu ameandika
 
Five rules for successful stock investing - Pat Dorsey
Just keep buying - Nick Migguel
Pia mfuatilie mtaalamu anaitwa Emillian Busara kuna mafundisho yake mengi youtube pia kuna vitabu ameandika
Yule mzee yuko vzr.Me nataka nijilipue na CRDB Hisa zao ziko vzr.
 
Kuweni makini na hizo pesa zenu hasa kipindi hiki cha uchafuzi
 
Back
Top Bottom