Fanto
JF-Expert Member
- Mar 23, 2012
- 211
- 83
Katika kikao kinachoendelea cha Bunge letu tukufu, Utoro wa baadhi ya Wah wabunge wetu ulisababisha shughuli za bunge kuahirishwa kwa sababu idadi ya waliohudhuria isingeruhusu kupitisha maamuzi. Mpaka sasa sijasikia watoro hawa wakichukuliwa hatua yoyote kwa kosa hilo. Je ni udhaifu wa Kanuni, Miongozo na Taratibu (walizojiwekea wenyewe)? Je mimi mwajiri wao (mpiga kura) nisubiri mpaka 2015 ili niwaadhibu? Naomba Mwanajamvi yeyote mwenye uelewa mpana na maswala ya Bunge anisaidie. Nimechoka kuibiwa kodi kibao ninazolipa.