Utetezi wa Simbachawene unaeleweka ukiwa ni mtu wa umri fulani

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,608
Jana niliwasikiliza mawaziri wakiitetea serikali ambaye ni mwajiri wao katika hili suala zima la tozo zinazotesa wananchi.

Sikutegemea kipya kusema ukweli kutoka kwa Dr Mwigulu Nchemba zaidi ya kujenga hoja nyingi za aina ya maisha aliyokulia, anajiweka mbali na dhana ya utajiri unaosemekana ameupata katika awamu ya sita baada ya kukabidhiwa dhamana ya uwaziri.

Kusema amekulia katika familia ya watoto 11 na kusema kachunga ng'ombe ni kujaribu tu kujishusha mbele ya macho na akili za wanaomsikiliza.

Utetezi ulionifanya nifikirie kwa kina ni ule uliotolewa na waziri wa mambo ya ndani Mheshimiwa Simbachawene. Yeye angalau alikuja na hoja zenye uungwana na zisizo na chembechembe ya mtu aliyelewa madaraka.

Pale aliposema kuwa ipo tofauti ya Awamu ya kwanza na ya pili na miaka hii ya sasa, aliweza kujenga hoja ya kueleweka. Kwamba kuna ongezeko kubwa la watu kitaifa. Na hao watu peke yake ni changamoto kuweza kutimiza mahitaji yao yote kama serikali.

Enzi zile tunasoma shule ya msingi na sekondari. Kulikuwa na utaratibu wa kuwalisha chakula cha mchana wanafunzi, nakumbuka miaka ile pale forodhani wanafunzi wa sekondari walikuwa wanapata chakula pale pale shuleni. Hapo hujaongelea utaratibu wa madaftari na vitabu kugawiwa bure.

Hayo yaliwezekana kutoka na uchache wa idadi ya watu wa Tanzania nzima kwa wakati ule, rasilimali angalau zilionekana kwenda sambamba na watu waliozitumia. Mtu akimaliza chuo kikuu ajira zinamsubiri tena za uhakika.

Leo hii huwezi ukayafanya haya bila ya kuleta maneno na kutokueleweka miongoni mwa wanajamii hao hao. Tupo wengi na tunazidi kuongezeka idadi, siku zote wingi wa watu huja na faida ya taifa kuwa na uhakika wa rasilimali watu na humo ndimo wamo wataalam wa sekta mbalimbali na wateja wa biashara mbalimbali kubwa.

Lakini wingi wa watu hujaa na changamoto za rasilimali zisizotosha kutakiwa ziyaguse maisha ya kila mtu, vita ya kimawazo ndio huanzia hapo.

Hivyo sio haki kusema kuwa sisi tumekuwa maskini kulinganisha na awamu za kwanza na ya pili, hapana. Ukweli ni kwamba teknolojia zimepiga hatua na maisha yamerahisishwa sana kulinganisha na miongo iliyopita. Mtihani ni namna kila mmoja wetu anavyoweza kuguswa na huo urahisishwaji wa maisha kulingana na maendeleo ya kiteknelojia.


Serikali hata ikijitahidi kuhakikisha uwepo wa ajira mpya laki moja kila mwaka, kama kwa mwaka huo mmoja wanaoingia katika soko la ajira wakiwa wakihitajika kitaaluma ni laki tano, hapo wapo watu laki nne wanaotakiwa kuumiza vichwa ili waweze kuwa na maisha angalau yenye kufanana na yale ya binadamu wa kisasa.

Kama upo uwezekano wa kukuza sekta zisizo rasmi kupitia ujenzi na uimarishaji wa vyuo vya VETA, na hilo lifanyike kwani ndilo litakalopunguza ukosefu wa ajira angalau kati ya wale laki nne wanaobakia mtaani basi laki mbili na nusu wawe na maarifa mengine ya kupambana wenyewe mtaani.

Huwa naziangalia filamu za kinigeria, namna zinavyovutia na kuwa na ujumbe unaoishi siku zote. Nollywood wametengeza mastaa wa viwango vya kidunia, wanasifika kila mahali sinema zao zinapouzwa. Ukichunguza wale watengeneza filamu na waigizaji utagundua wengi wao ni watu waliokosa kazi rasmi za serikalini na kuamua kupambana kwa kujiajiri wenyewe.

Kwa Taifa lenye kufanya sensa ili kujua idadi ya watu wake, ambao kwa habari zisizo rasmi wanaweza kuzidi milioni 60, wasio na ajira wataendelea kuongezeka. Hivyo sekta kama filamu na zenyewe zipewe kipaumbele na wizara husika.

Kisiwe ni kipaumbele cha kisiasa, la hasha. Wenye kuweza kufaidika na sekta ya filamu ni wengi, wenye elimu za vyuo vikuu na wasio na kazi kama Nigeria kwa hapa Tanzania ni wengi pia. Serikali inajipangaje kuitumia sanaa ya uigizaji katika kupungua hii changamoto ya ajira. Hilo ni swali linaelekezwa kwa wizara yenye dhamana ya utamaduni na masuala ya sanaa.

Pia kuna suala la serikali kuutazama mpira wa miguu, una fursa nyingi sana zimejificha japokuwa baadhi yetu tunautazama tukiwa na mtazamo hasi. Samuel Eto'o amestaafu rasmi soka miaka kama kumi imepita lakini mpaka kesho ni balozi maalum ya mashirika makubwa ya UN, pamoja na Kanu na Drogba. Hawa watu wameingiza pesa nyingi kiasi gani katika mzunguko wa kiuchumi huko katika mataifa wanayotoka?.

Zipo habari za Obi Mikel nyota wa zamani wa Nigeria ambaye inadaiwa malori mengi yanayofanya biashara huko Lagos na Abuja mmiliki ni yeye, ametoa ajira kwa wanigeria wangapi?. ameingiza pesa kiasi gani katika mzunguko mzima wa Nigeria?. Nilimuelewa sana Mheshimiwa Rais SSH aliposema upo mpango wa kujenga academy pale Tanganyika Packers Kawe kuliko kupaacha pakichakaa tu. Ni sekta yenye kutengeneza mzungiko mpana sana wa pesa kama ikitiliwa maanani na kutochukuliwa poa tu.

Niliweza kumuelewa Waziri Simbachawene, kwamba maisha ya sasa yamerahisishwa sio kama yale ya simu za mezani za kuzungusha, sasa hivi unatumia vidole kwa kugusa tu kioo cha simu unakuwa umeshawasiliana na jamaa zako wa Marekani na Canada.

Nilimuelewa aliposema ipo changamoto ya mtu mmoja mmoja, ndio hivi vilio vya tozo kwa raia asiye na kipato halafu hicho hicho kidogo anachopata anapoamua kuweka benki au kumtumia rafiki yake anaona kinakatwa kodi.

Wingi wetu na ongezeko la watu huja na neema nyingi tu lakini huja pia na changamoto halisi. Niliweza kuielewa vizuri hoja ya Mheshimiwa Simbachawene.
 
Mimi sijakuelewa ww uliyemwelewa chawene.

Swali ni je?

Tulipo kuwa idadi ndogo miaka ya nyuma Serikali iliweza kutuhudumia, sasa tumeongezeka sana inashindwaje kutuhudumia?

Watu walioongezeka ni tegemezi wasozalisha chochote?

Serikali imeongeza au imepunguza makusanyo ya Kodi Kwa idadi ya wananchi walioongezeka?

Kwamba unataka kusema Idadi ya watu kuwa wengi Serikali inashindwa kuwafikia kuwatoza Kodi?

Au Tuigawe Nchi ktk majimbo Ili tuisimamie vizuri kukusanya mapato na kuhudumia wananchi?

Au wingi wa wananchi umesababisha mapato kuwa mengi kiasi kwamba viongozi wanakwapua na hawafikiki kumulikwa wakiziiba?

We umeona hoja ndugu?
 
..kiongozi au mtawala anatakiwa atatue au atoe majibu ya changamoto za wakati ambao yuko ktk uongozi.

..Simbachawene alitakiwa atoe ufumbuzi wa matatizo, na sio kutoa hoja za kujaribu kuyahalalisha kwa kulinganisha na hali ya kiuchumi wakati anakua.

..Viongozi tulionao sasa hivi wanatumia vitendea kazi bora kuliko viongozi wa awamu ya 1, 2, na 3. Wakati wa Nyerere kulikuwa hakuna ma-V8, cell phones, computers, etc etc.

..Kama viongozi wa sasa hivi wanatumia vitendea kazi bora zaidi, na wana elimu, maarifa, taarifa, etc kuliko awamu zilizopita basi wanatakiwa kuwa na majibu ya uhakika kutatua changamoto za zama hizi.
 
Mhm
 

Attachments

  • 20220902_174946.jpg
    20220902_174946.jpg
    53.1 KB · Views: 7
Bora hata wewe uliyemuelewa, mimi ndo sijakuelewa tu ulichoandika!
 
Jana niliwasikiliza mawaziri wakiitetea serikali ambaye ni mwajiri wao katika hili suala zima la tozo zinazotesa wananchi.

Sikutegemea kipya kusema ukweli kutoka kwa Dr Mwigulu Nchemba zaidi ya kujenga hoja nyingi za aina ya maisha aliyokulia, anajiweka mbali na dhana ya utajiri unaosemekana ameupata katika awamu ya sita baada ya kukabidhiwa dhamana ya uwaziri.

Kusema amekulia katika familia ya watoto 11 na kusema kachunga ng'ombe ni kujaribu tu kujishusha mbele ya macho na akili za wanaomsikiliza.

Utetezi ulionifanya nifikirie kwa kina ni ule uliotolewa na waziri wa mambo ya ndani Mheshimiwa Simbachawene. Yeye angalau alikuja na hoja zenye uungwana na zisizo na chembechembe ya mtu aliyelewa madaraka.

Pale aliposema kuwa ipo tofauti ya Awamu ya kwanza na ya pili na miaka hii ya sasa, aliweza kujenga hoja ya kueleweka. Kwamba kuna ongezeko kubwa la watu kitaifa. Na hao watu peke yake ni changamoto kuweza kutimiza mahitaji yao yote kama serikali.

Enzi zile tunasoma shule ya msingi na sekondari. Kulikuwa na utaratibu wa kuwalisha chakula cha mchana wanafunzi, nakumbuka miaka ile pale forodhani wanafunzi wa sekondari walikuwa wanapata chakula pale pale shuleni. Hapo hujaongelea utaratibu wa madaftari na vitabu kugawiwa bure.

Hayo yaliwezekana kutoka na uchache wa idadi ya watu wa Tanzania nzima kwa wakati ule, rasilimali angalau zilionekana kwenda sambamba na watu waliozitumia. Mtu akimaliza chuo kikuu ajira zinamsubiri tena za uhakika.

Leo hii huwezi ukayafanya haya bila ya kuleta maneno na kutokueleweka miongoni mwa wanajamii hao hao. Tupo wengi na tunazidi kuongezeka idadi, siku zote wingi wa watu huja na faida ya taifa kuwa na uhakika wa rasilimali watu na humo ndimo wamo wataalam wa sekta mbalimbali na wateja wa biashara mbalimbali kubwa.

Lakini wingi wa watu hujaa na changamoto za rasilimali zisizotosha kutakiwa ziyaguse maisha ya kila mtu, vita ya kimawazo ndio huanzia hapo.

Hivyo sio haki kusema kuwa sisi tumekuwa maskini kulinganisha na awamu za kwanza na ya pili, hapana. Ukweli ni kwamba teknolojia zimepiga hatua na maisha yamerahisishwa sana kulinganisha na miongo iliyopita. Mtihani ni namna kila mmoja wetu anavyoweza kuguswa na huo urahisishwaji wa maisha kulingana na maendeleo ya kiteknelojia.


Serikali hata ikijitahidi kuhakikisha uwepo wa ajira mpya laki moja kila mwaka, kama kwa mwaka huo mmoja wanaoingia katika soko la ajira wakiwa wakihitajika kitaaluma ni laki tano, hapo wapo watu laki nne wanaotakiwa kuumiza vichwa ili waweze kuwa na maisha angalau yenye kufanana na yale ya binadamu wa kisasa.

Kama upo uwezekano wa kukuza sekta zisizo rasmi kupitia ujenzi na uimarishaji wa vyuo vya VETA, na hilo lifanyike kwani ndilo litakalopunguza ukosefu wa ajira angalau kati ya wale laki nne wanaobakia mtaani basi laki mbili na nusu wawe na maarifa mengine ya kupambana wenyewe mtaani.

Huwa naziangalia filamu za kinigeria, namna zinavyovutia na kuwa na ujumbe unaoishi siku zote. Nollywood wametengeza mastaa wa viwango vya kidunia, wanasifika kila mahali sinema zao zinapouzwa. Ukichunguza wale watengeneza filamu na waigizaji utagundua wengi wao ni watu waliokosa kazi rasmi za serikalini na kuamua kupambana kwa kujiajiri wenyewe.

Kwa Taifa lenye kufanya sensa ili kujua idadi ya watu wake, ambao kwa habari zisizo rasmi wanaweza kuzidi milioni 60, wasio na ajira wataendelea kuongezeka. Hivyo sekta kama filamu na zenyewe zipewe kipaumbele na wizara husika.

Kisiwe ni kipaumbele cha kisiasa, la hasha. Wenye kuweza kufaidika na sekta ya filamu ni wengi, wenye elimu za vyuo vikuu na wasio na kazi kama Nigeria kwa hapa Tanzania ni wengi pia. Serikali inajipangaje kuitumia sanaa ya uigizaji katika kupungua hii changamoto ya ajira. Hilo ni swali linaelekezwa kwa wizara yenye dhamana ya utamaduni na masuala ya sanaa.

Pia kuna suala la serikali kuutazama mpira wa miguu, una fursa nyingi sana zimejificha japokuwa baadhi yetu tunautazama tukiwa na mtazamo hasi. Samuel Eto'o amestaafu rasmi soka miaka kama kumi imepita lakini mpaka kesho ni balozi maalum ya mashirika makubwa ya UN, pamoja na Kanu na Drogba. Hawa watu wameingiza pesa nyingi kiasi gani katika mzunguko wa kiuchumi huko katika mataifa wanayotoka?.

Zipo habari za Obi Mikel nyota wa zamani wa Nigeria ambaye inadaiwa malori mengi yanayofanya biashara huko Lagos na Abuja mmiliki ni yeye, ametoa ajira kwa wanigeria wangapi?. ameingiza pesa kiasi gani katika mzunguko mzima wa Nigeria?. Nilimuelewa sana Mheshimiwa Rais SSH aliposema upo mpango wa kujenga academy pale Tanganyika Packers Kawe kuliko kupaacha pakichakaa tu. Ni sekta yenye kutengeneza mzungiko mpana sana wa pesa kama ikitiliwa maanani na kutochukuliwa poa tu.

Niliweza kumuelewa Waziri Simbachawene, kwamba maisha ya sasa yamerahisishwa sio kama yale ya simu za mezani za kuzungusha, sasa hivi unatumia vidole kwa kugusa tu kioo cha simu unakuwa umeshawasiliana na jamaa zako wa Marekani na Canada.

Nilimuelewa aliposema ipo changamoto ya mtu mmoja mmoja, ndio hivi vilio vya tozo kwa raia asiye na kipato halafu hicho hicho kidogo anachopata anapoamua kuweka benki au kumtumia rafiki yake anaona kinakatwa kodi.

Wingi wetu na ongezeko la watu huja na neema nyingi tu lakini huja pia na changamoto halisi. Niliweza kuielewa vizuri hoja ya Mheshimiwa Simbachawene.
Hapana kabisa, hoja ya mh. Simbachawene siyo ya mashiko. Kushindwa kuhudumia wananchi maana yake mipango mibovu.
 
Ongezeko la watu linaenda sambamba na ongezeko la shughuli za kiuchumi na ongezeko la mapato ya serikali. Hoja yako ingekuwa sahihi kama makusanyo ya serikali yangebaki kiwa vile vile huku idadi ya watu ikiongezeka.

Wakati wa Nyerere kodi kwa mwezi ilikusanywa kiasi gani na sasa ni kiasi gani? Barabara za lami zilikuwa Km ngapi na sasa ni km ngapi?

Utetezi wa ongezeko la watu hauna mantiki. Kiuhalisia watu wanapoongozeka ndo maisha yanatakiwa kuwa rahisi. Kilichopo.l sasa hivi ni. Labda kilichopo sasa hivi ni.
1. Serikali kushindwa kutumia watu wake. Kwa maana watu wengi hawazalishi. Hii inatokana na uongozi mbovu, mipango mibovu, ukosefu wa mbinu mpya za kuongeza ajira n.k.
2. Wizi wa fedha za serikali na matumizi mabaya ya fedha za umma. Serikali imeshindwa ku control matumizi na kuelekeza fedha zinazo kusanywa kwenye mambo ya msingi.
 
samahani kwa lugha hii, "kuna wakati nakuta najisemea tu inawezekana mimi sina akili au hawa watu ndio hawana akili"

inamaana Serikali ilikuwa inaamini idadi ya watu itabaki ile ile ya 1961 wakati tunapata uhuru.?

Ina maana serikali haijua birth na death rate kwa watu wake na kuforecast in every 20yrs kuanzia leo na kujipanga?
 
Wakati huo pato la taifa lilikuwa asilimia ngapi? Na je, miradi iliendeshwa kwa namna gani? Maana leo hii mikopo kila kona, mara nchi imefunguliwa na bado wananchi wanakatwa tozo! Ardhi inabinafsishwa! Wageni kila siku wanapishana ikulu! Faida ya hayo yote ni nini?

Argument ya huyo mheshimiwa ni ya hovyo kabisa. Haina mashiko. Ni mawazo ya kizamani sana. Wale wanaopenda kusema enzi zetu tulitembea umbali mrefu kutafuta huduma, mara oh, tulipanga foleni kupata bidhaa!
Hayo hayana uhusiano na tozo!
 
Kama wingi wa watu unaleta umasikini, China yenye watu zaidi ya bilioni moja wangekuwa mafukara wa kutupwa.
 
Sasa Kama tupo wengi China na India wasemeje?
Shida ya viongozi wa chama Twawala ni kujiona wao,jamaa na ndugu zao ndiyo wenye akili sana ya kuongoza nchi,hawapendi mawazo mapya.
Kazi ya kiongozi ni kutatua matatizo siyo kuyaainisha
Sasa wanafanya sensa za nini?maana sensa ndiyo inatoa mwelekeo wa nature ya Demography kama tuna au tutakuwa na wazee wengi kuliko vijana kwa maana ya nguvu kazi lakini kwa Tanzania asilimia kubwa ya nguvu kazi ni vijana,sasa kinachotakiwa ni kuwawezesha ili wajiendeleze.
Mifuko ya mikopo mingi mpaka time ya uwezeshaji Wananchi kiuchumi ipo lakini wanafanya kazi gani,zaidi ya kula mishahara ya bure na kuleta uchawi tu kwa vijana wanaotaka kujikwamua na umasikini!!
Ata sasa uliza tu vijana wanaojishughulisha na ujasiriamali kuwa ni wangapi wamepewa mikopo ya 10% za halmashauri?ukiwakuta Basi wengi ni makada wa chama Twawala maana ndiyo wanaopewa kipaombele Kama ambavyo kwenye sensa tumeshuhudia.
*Yaanina sisi watanzania tumekaa tunaamini eti tuna Mawaziri wenye akili wa kutukomboa na umaskini,the likes Mwigulu(Mr Burundi), TaifaGas Kipara,Nape,Bashungwa,Ridhiwan nk.🤣🤣🤣🤣
MUNGU ATUSAIDIE SANA WATANZANIA
 
Cha ajabu wao wameshindwa kuepuka matumizi yasio ya lazima ,wanafuja tu
 
Mimi sijakuelewa ww uliyemwelewa chawene.

Swali ni je?

Tulipo kuwa idadi ndogo miaka ya nyuma Serikali iliweza kutuhudumia, sasa tumeongezeka sana inashindwaje kutuhudumia?

Watu walioongezeka ni tegemezi wasozalisha chochote?

Serikali imeongeza au imepunguza makusanyo ya Kodi Kwa idadi ya wananchi walioongezeka?

Kwamba unataka kusema Idadi ya watu kuwa wengi Serikali inashindwa kuwafikia kuwatoza Kodi?

Au Tuigawe Nchi ktk majimbo Ili tuisimamie vizuri kukusanya mapato na kuhudumia wananchi?

Au wingi wa wananchi umesababisha mapato kuwa mengi kiasi kwamba viongozi wanakwapua na hawafikiki kumulikwa wakiziiba?

We umeona hoja ndugu?
Tulipokuwa idadi ndogo serikali iliweza kufika kwa watu ilivyoweza tofauti na sasa. Ili kila mtu aipate keki ya taifa kile kinachozalishwa kinatazamwa uwiano wake kwa kulinganisha na wale wanaokitumia.

Watu wanaoongezeka kwa mapenzi ya Mungu, Huwezi kuweka uwiano sawa kati ya wanaoongezeka na uwezo wao wa kuzalisha kumbuka kuwa kuzaliwa na kukua mpaka kufika umri wa kuzalisha mali ni mchakato wa kisayansi.

Wanaozaliwa na kuwa wazalishaji mali, hakuna anayejua uwiano wao utakuwa vipi watakapofika umri wa kuwa wazalishaji. Kuna watu wanapotea na madawa ya kulevya kabla hata hawakafika umri wa kuzalisha!.

Majimbo kuwepo sio suluhisho la matatizo haya ya sasa, ukiigawa nchi utaleta ukabila na chuki za kikanda. Yale yale yanayoitesa Nigeria ya sasa, watatokea wajinga wanaoteswa na njaa na kuanza kuhubiri udini na sera za kikanda zenye kuongeza hasira na mitazamo hatari ya watu kujigawa na kuchukiana.


Maendeleo ya teknolojia yana faida ya nchi kufikiwa lakini huko serikali inapofika walipo watu inakutana na changamoto zinazotokana na ongezeko la idadi ya watu lisilo na uwiano sawa na wanachotakiwa wakipate.

Wingi wa watu ni changamoto nzuri kwani ukitumika vizuri unazo faida zenye kuweza kudumu miaka na miaka.
 
Wakati huo pato la taifa lilikuwa asilimia ngapi? Na je, miradi iliendeshwa kwa namna gani? Maana leo hii mikopo kila kona, mara nchi imefunguliwa na bado wananchi wanakatwa tozo! Ardhi inabinafsishwa! Wageni kila siku wanapishana ikulu! Faida ya hayo yote ni nini?

Argument ya huyo mheshimiwa ni ya hovyo kabisa. Haina mashiko. Ni mawazo ya kizamani sana. Wale wanaopenda kusema enzi zetu tulitembea umbali mrefu kutafuta huduma, mara oh, tulipanga foleni kupata bidhaa!
Hayo hayana uhusiano na tozo!
Tozo zinazotwa na ili serikali ipunguze mzigo wa huduma kwa wananchi. Ili serikali iwe na wigo mpana wa mapato halali.

Changamoto za sasa ni nyingi kulinganisha na miaka ile ya awamu ya kwanza. Mwaka 1982 kutoka Dar mpaka Tanga ilikuwa ni zaidi ya saa kumi na mbili ndani ya basi la Yarabi Salama leo hii ni saa tatu tu umeshafika.

Nchi imefunguka kimaendeleo lakini ni maendeleo yanayokutana na mahitaji mapana ya watu hivyo uwezo ule wa 1982 wa kuhudumia watu hao hao hauwezi kufanana na wa leo hii mwaka 2022 miaka 40 baadae.

Tozo zinauma lakini ndio kujitegemea kwenyewe huko. Mawaziri wetu walikuwa wakinyanyasika sana kwenda kuomba omba pesa za kuendesha nchi kila siku huko Ulaya na Marekani, kuamua kuja na tozo au kodi ni kupunguza kero ya matusi waliyokuwa wakikutana nayo kila wanapokwenda kuomba kwa wazungu.

Kuna muda unafika ni lazima tujitegemee, upo uchungu wa kufanya hivyo lakini ni kulinda pia heshima ya taifa letu.
 
..kiongozi au mtawala anatakiwa atatue au atoe majibu ya changamoto za wakati ambao yuko ktk uongozi.

..Simbachawene alitakiwa atoe ufumbuzi wa matatizo, na sio kutoa hoja za kujaribu kuyahalalisha kwa kulinganisha na hali ya kiuchumi wakati anakua.

..Viongozi tulionao sasa hivi wanatumia vitendea kazi bora kuliko viongozi wa awamu ya 1, 2, na 3. Wakati wa Nyerere kulikuwa hakuna ma-V8, cell phones, computers, etc etc.

..Kama viongozi wa sasa hivi wanatumia vitendea kazi bora zaidi, na wana elimu, maarifa, taarifa, etc kuliko awamu zilizopita basi wanatakiwa kuwa na majibu ya uhakika kutatua changamoto za zama hizi.
Easier said than done brother Jokakuu.
 
Hapana kabisa, hoja ya mh. Simbachawene siyo ya mashiko. Kushindwa kuhudumia wananchi maana yake mipango mibovu.
Tangu tupate uhuru haijawahi kutokea tukawa na mipango mizuri. Tunaona shida kulipa hizi tozo lakini ndio uhalisia wenyewe wa maisha.
 
Tozo zinazotwa na ili serikali ipunguze mzigo wa huduma kwa wananchi. Ili serikali iwe na wigo mpana wa mapato halali.

Changamoto za sasa ni nyingi kulinganisha na miaka ile ya awamu ya kwanza. Mwaka 1982 kutoka Dar mpaka Tanga ilikuwa ni zaidi ya saa kumi na mbili ndani ya basi la Yarabi Salama leo hii ni saa tatu tu umeshafika.

Nchi imefunguka kimaendeleo lakini ni maendeleo yanayokutana na mahitaji mapana ya watu hivyo uwezo ule wa 1982 wa kuhudumia watu hao hao hauwezi kufanana na wa leo hii mwaka 2022 miaka 40 baadae.

Tozo zinauma lakini ndio kujitegemea kwenyewe huko. Mawaziri wetu walikuwa wakinyanyasika sana kwenda kuomba omba pesa za kuendesha nchi kila siku huko Ulaya na Marekani, kuamua kuja na tozo au kodi ni kupunguza kero ya matusi waliyokuwa wakikutana nayo kila wanapokwenda kuomba kwa wazungu.

Kuna muda unafika ni lazima tujitegemee, upo uchungu wa kufanya hivyo lakini ni kulinda pia heshima ya taifa letu.

..Mimi sikuelewi unaposema awamu hii ina changamoto nyingi kuzidi awamu ya kwanza / mwaka 1982.

..Usafiri ni nafuu. Mawasiliano ni ya kasi zaidi. Vitendea kazi na teknolojia ni ya kisasa kushinda wakati. Hata lIfe expectancy ni kubwa zaidi.

..Yote hayo niliyoyataja yanaelekeza kwamba kila mtu ktk nafasi yake anatakiwa kuzalisha au kufanya kazi kwa tija na viwango vya juu kuliko zamani.

..Binafsi sitegemei Waziri wa fedha Mwigulu Nchemba alalamike kwamba wizara yake ina wakati mgumu kawa wakati wa Amir Jamal, au Kighoma Malima, waliokuwepo wakati tunafunga mikanda miaka ya 1980.

..Kama Mwigulu, Simbachawene, na wengine wanaona majukumu yao ni magumu au changamoto zimewaelemea, basi wawapishe wengine.
 
Back
Top Bottom