Utengenezaji wa Sabuni za Aina Mbalimbali: Fahamu Mahitaji, Mchakato wa Uzalishaji na Masoko

Nkoboiboi

JF-Expert Member
Oct 9, 2010
243
63


Tafadhali wana JF wenzangu,

Anayeweza kunifundisha kutengeneza sabuni naomba tuwasiliane haraka. Nina soko kubwa.


WADAU WENGINE WENYE KUHITAJI KUFAHAMU BIASHARA HII
WanaJF,

Naitaji kuanza kutengeneza sabuni za kufulia kama B 29, Star ya Uganda, Komesha n.k, mimi niko Mwanza na tatizo litakalonikwamisha ni soko sababu mwanzo ni mgumu. Naomba niwasilishe kwenu kwa maoni na ushauri zaidi.
Heshima kwenu wadau.

Naomba masada wenu kama kuna yeyote anayejua jinsi ya kutengeneza JASIMINI ile ya kusafishia chooni.

Natanguliza shukrani.


MICHANGO YA WADAU MBALIMBALI



 
Upo wapi? Una mtaji kiasi gani? Je, unataka kutengeneza ya maji au kipande,je ni medicated soap au ya kawaida?

Unatarajia kutengeneza kwa machine au mkono? Miimi nilikuwa na kiwanda cha sabuni, tatizo ni mali ghafi kwa Dar-es-Salaam. Kuna mtaalam wa sabuni anaweza kutengeneza sabuni.
Tafadhali wana JF wenzangu anayewezakunifundisha kutengeneza sabuni naomba tuwasiliane haraka. Nina siko kubwa
 
Tafadhali wana jf wenzangu anayewezakunifundisha kutengeneza sabuni naomba tuwasiliane haraka. Nina siko kubwa

Muzeiya karibu sana katika ukumbi wa ujasiliamali katika nyanja hiyo niko bomba ile mzuri waweza kinipata kwa {safariwafungo@yahoo.com} tuwasiliane tuweze fanya kazi mzee, na kwa wale wenye kutaka ku-invest in manufacturing industry and the like please let work together I have a huge exposure academically and in experience wise!
 
Kutengeneza sabuni ni kupata malighaafi kama Alkali, mafuta, n.k Kama uko serious nitakupa formula zote

Mkuu nakubariana na wewe kwa kiasi fulani, ila kuhusu kumpa mtu formula that is not a good idea, kwasababu hizo malighafi zinautofauti mkubwa wa ubora wake kulingana na source yako kwa wakati huo ni ipi au imehifadhiwa vipi, hii ni kwa uchache tu, kimsingi unapoamua kujikita katika bzness is better product yako ikawa consistence within the market, kwasababu ndicho wanacho hitaji walaji.

Sasa kama kuna variation katika malighafi ni ndoto kuwa na consistence katika product yako. Jamani hizi ni fani za watu hivyo ni vyema zikachukuliwa kwa umakini zaidi. Sasa nini kinatakiwa kufanywa, ni kuwawezesha wajasiliamali wawe nauwezo wa kufanya formula project, cost estimation na vitu kama determination of selling price, sasa kwa yule aliye tayari na mkaribisha tufanye kazi and to experience the difference!
 
Mzee wazo lako tamu sanaaa! Upo mkoa gani? Mi ninaweza kukusaidia katika maswala mawili matatu(capital,sehemu ya kutengenezea, tena ipo mjini kabisa, na maswala ya matangazo) kama soko tayari unalo sio tabu. Kama upo tayari niwe biz partner wako nicheki hapa: Charleschami@yahoo.com.
 
Well, one can search more of such soap making formulas online as well but get to know that these are reactive so be careful during its making process.
 
Mimi ni mtumishi wa uma, nimejaliwa kupata mtaji kidogo, nataka nianzishe kiwanda kidogo cha kutengeneza sabuni. Je, ni vitu gani vinahitajika na soko lipo la bidhaa hiyo? Hapa Tz.
 
Mimi ni mtumishi wa uma, nimejaliwa kupata mtaji kidogo, nataka nianzishe kiwanda kidogo cha kutengeneza sabuni. Je, ni vitu gani vinahitajika na soko lipo la bidhaa hiyo? Hapa TZ
Ndugu Mjasiriamali matarajiwa!

Biashara yeyote ni upatikanaji wa "soko" - yaani wanunuzi. Ni kazi yako kufanya utafiti wa kuwepo kwa "soko". Wengine hawatakusaidia sana. Pili, unataka kutengeneza sabuni ya aina gani? - Kwa maana kulingana na matakwa ya "soko" lako! Sabuni ya maji, unga, manukato (na ya aina gani?) na maswali mengi. Je, unaijua stadi ya utengenezaji sabuni? Kama la.

Soma vitabu, ingia kwenye websites kama - "Instructables" au tembelea watengenezaji sabuni wadogo na wakubwa! Nipigie tafadhali - 0784360034

Nakutakia mafanikio mema.

RA
 
Mimi nataka kujikita ktk utengenezaji wa sabuni za miche na za kuogea ila sina utalaamu, nimesikia sido wanafundisha, pia nataka kujua machine za kutengeza sabuni zinapatikana wapi.
 
Mkuu nina uzoefu wa kutengeneza sabuni za miche. Soko lipo kubwa mmno kwani viwanda havikidhi mahitaji ndio sababu bado tuna import sabuni.

Machine ya kutengeneza sabuni - Ploder ni milioni 7, ya kukata chips milioni 1, na clutcher ya kupikia sabuni ni around 3millioni, ila unaweza kuanzia kupika ktk mapipa ya lita200 (siyo kazi rahisi kutumia mapipa) hivyo unahitaji around milioni11 kwa ajili ya equipment.

Tatizo ni Malighafi. mafuta ya kutengeneza sabuni yanatoka nje ya nchi, hivyo yanaagizwa na viwanda vikubwa, viwanda vidogo wananunua kwa dili kutoka kwa madalali.

Kuna mafuta ya mise yanatoka Mbeya, na Kigoma haya ni rahisi ila kama upo Dar gharama ya usafiri ni kubwa.

Competitors
Sabuni ya kiwanda kidogo huwa na ubora zaidi ktk maji ya chumvi/kisima ambayo ndio maji yanayotumika na Watanzania wengi, sabuni za viwanda vikubwa huwa zimechujwa sana (highly refined and processed oils) hivyo hazifai ktk maji ya visima.

Watengeneza sabuni za mikono kutoka kigoma huwa wanamwaga sabuni nyingi ktk soko la DAr ,wanarudi a month later kuchukua pesa, hivyo jiandae kushindania nao.

Viwanda vikubwa sabuni zao zinapendwa mjini e.g Dar, Arusha na Mwanza ambako kuna maji ya bomba,hivyo tarajia soko la mikoani na vijijini, ili uwafikie hawa wateja inabidi uunde distribution network ya whole sellers, pale manzese kuna maduka ya wapemba ya whole sale ukiwapelekea mzigo wanakulipa hapo hapo, wao huwa wanawauzia watu wanaopeleka bidhaa za maduka mikoani. e.g pruduct yangu nilikuwa siioni madukani in Dar es Salaam. Nilipodadisi nikagundua ipo very popula in Kibaigwa Dodoma. So niki-supply mzigo jamaa wanaotoka Dodoma hawanunui kitu kingine zaidi hiyo sabuni.

Kama utafungua kiwanda mitaani na siyo ktk industrial zone e.g Pugu Road, EPZA jinpange kupambana na TFDA. Bora ya TBS, Afisa biashara, TRA, mwenyekiti wa serikali za mtaa.

Packaging ya product yako ni muhimu sana,ndiyo maana wachina wanauza vitu vyao kwa wingi wao wanajua packaging and presentation nzuri za quality.

Kwa sabuni ya mche ni kutengeneza mabox nenda Pugu Road kiwanda kinaitwa Commercial Printers wao wanabei nzuri na ni wazoefu kwa ajili ya SME s wenye viwanda vidogo watakufanyia design ya box, inabidi uende na miche yako ili wawe na uhakika wa vipimo vya carton.

Kwa ushauri zaidi wa michanganuo ya biashara na faida muone BABALAO atakushauri vizuri zaidi mpaka jinsi ya kupata mkopo.
 
Kuna hawa jamaa wa Tanzania Business Creation Company wanatoa semina kwa wajasiriamali wanaotaka kumiliki viwanda vidogo vidogo. Mafunzo wanayotoa ni pamoja na utengenezaji wa:

Sabuni za kufulia na kuogea
Sabuni za maji
Shampoo za kila aina
Dawa za viatu
Bleaching agent
Petrolleam jelly etc.
 
thanks,je hizi semina wanazotoa ni kiasi gani kuattend?
 
Mkuu dawa za viatu ndo nini? Hawa jamaa ni Waswahili wenzetu au Wachina?

 
Mkuu dawa za viatu ndo nini? Hawa jamaa ni waswahili wenzetu au wachina?

Kweli Wachina kiboko. Kumbe kuna mpaka mayai ya Kichina. Watu wamenunua egg chops na kababu zilizotegenezwa na mayai ya kichina pale royal bakery kawe matokeo yake matumbo yamewauma na wameendesha vibaya sana.
 

mkuu new mzalendo umetoa ushauri mzuri sana kwa huyu ndg yetu. Kweli unauzoefu ktk eneo hilo. Big up bro.
 
Mkuu dawa za viatu ndo nini?
Hawa jamaa ni waswahili wenzetu au wachina?

Kaka hiyo no shoe polish. Inavyoelekea ni waswahili wenzetu na ni mradi wa kanisa liitwalo Word Alive Church lililopo Sinza Mori.

Wanauza mtambo wa kutengeneza sabuni za miche unaotoa miche 150 pamoja na mishumaa 500 kwa siku. Pia watakuunganisha na watengenezaji mitambo wa China na kukusaidia kuagiza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…