Utata wa dhehebu lako katika kufunga ndoa

Utata wa dhehebu lako katika kufunga ndoa

Mkuu ngoja nikupe ufafanuzi mzuri hapa, halafu utaelewa vizuri Concept kati ya Ndoa na Imani.

1/Ndoa ni taasisi ya Kiimani kwa 100%. Huwezi kuitenganisha ndoa na imani yako. Mitazamo yote ya ndoa iliyopo leo duniani imetafsiriwa kutoka kwenye maandiko ya kiimani. Kuanzia kwenye Uhindi, Ukristo, Uislamu nk.

2/Ndoa ni mapatano baina ya watu wawili tu, na patano hilo linaweza kuhalalishwa kisheria, kiimani au Kijamii. Sasa vijana waliochumbiana wenyewe, waamue wao wenyewe kwanza wanataka kuhalalisha(kuubariki) uhusiano wao wa kindoa katika misingi ipi ya kiimani. Kama wameshindwa kuafikiana katika hilo sasa, usitegemee kama wataweza kuishi kwenye ndoa kwenye uhalalisho huo. Ni vyema wakajiuliza kama kuna ulazima wa wao kuishi pamoja(kuoana)

3/Imani yako ni zaidi ya ndoa yako, hivyo hupaswi kuilazimisha Imani yako iifuate ndoa yako maana haiwezekani, ila unaweza kuilazimisha ndoa yako ifuate imani yako maana inawezekana.
Nimekuelewa vizuri sana ndugu na asante sana kwa maelezo mazuri.
Kuna kitu nimeongeza kutoka kwenye maelezo yako
 
The Spirit of Prophecy consistently counsels against marriage between “the believer and the unbeliever” and further cautions against uniting with fellow Christians who have “not accepted the truth for this time.”—5T 364. Marriages are more likely to endure, and family life to fulfill the divine plan, if husband and wife are united and are bound together by common spiritual values and lifestyles. For these reasons the Church strongly discourages marriage between a Seventh-day Adventist and a member of another religion and strongly urges its pastors not to perform such marriages.

The Church recognizes that it is the prerogative of each individual member to make the final decision relative to the choice of a marriage partner. However, it is the hope of the Church that if the member chooses a partner who is not a member of the Church, the couple will realize and appreciate that the Seventh-day Adventist pastor, who has covenanted to uphold the principles outlined above, should not be expected to perform the marriage.

Hii ni sehemu ya maelezo ya kanuni ya kanisa la Waadventista Wasabato. Hapo hakuna ndoa itakayofungwa kwa kifupi tu
Umeeleweka ndugu, asante kwa ufafanuzi mzuri,
nahisi ndio sababu huyo binti amekataa mwanzo mwisho kufunga ndoa nje ya dhehebu lake la kisabato.
Ila kwa upande mwingine naona ni kama kifungo kwa wasabato na sheria zao hizo zenye utata
 
Leo ni mara ya kwanza kuingia kwenye hili jukwaa wadau, nategemea ushauri wa maana juu ya hili jambo.

Iko hivi kuna kijana wangu anaomba ushauri kuhusu tatizo linalomsumbua yeye ni mkristo wa dhehebu la KKKT na ana mchumba wake ni msabato, sasa mda unazidi kwenda kijana anataka kufunga ndoa.

Kijana akatoa wazo kwa binti kwamba ndoa inatakiwa ifungwe kanisani KKKT na baada ya ndoa binti ataendelea na dhehebu la kisabato.

Sasa binti amegoma kabisa, binti nae kasema hawezi kufunga ndoa KKKT anataka ndoa ifungwe kanisani sabato na baada ya ndoa kamruhusu kijana aendelee na dhehebu la KKKT.
Sasa ubishano upo kwenye wapi ndoa ifungwe kati ya Kanisani KKKT au sabato, na imefika hatua kwamba endapo mmoja atakataa kukubali mawazo ya mwenzie wanasema bora mahusiano yaishe.

Sasa wadau mnaushauri gani ili kuweza kuwanusuru huyu kijana pamoja na huyo mchumba wake.
Nimewashauri kuhusu ndoa ya kiserikali, ila wote hawako tayari kwa ndoa ya kufungwa serikalini.

Je mnamshauri nini huyu kijana na mchumba wake ili waweze kufanikisha mipango yao ya kufunga ndoa pamoja?
Dini hizi...

Kama wote wanaona imani zao ni kali kuliko hitaji lao la kuwa pamoja nadhani kila mmoja aifuate imani yake.
 
Y aani sisi wasabato
Mtu yeyot e a siye msabato ni asiyeamini.
Biblia inatuonya kufunga nira na wasioamini wakiwamo kkkt
Rc na wato to wake.
Ufinyu wa mawazo hamna tofauti na mafarisayo ambao Yesu alikua anawashushua...ng'ombe akianguka shimoni sabato hamumtoi??..
Dini yenyewe mpo wachache af mnataka uoe wa dini yako subutuu
 
Kutumia biblia siyo sababu..

Mosi....Wasabato hawaamini Utatu Mtakatifu
Wasabato wanapinga ufufuko wa Yesu...Ref, kitabu cha Mama EGW nabii wao kinachoitwa Investigative Judgement....

Pili Wasabato wana biblia yao mpya inajulikana kama "the clear Word Bible"
Ahhhhh hapa sasa unapotosha umma na huwezi kubaki salama,kama hujui wasabato kaa kimya..
Eti hawaaamini utatu na ufufuo sasa nini maana ya mkristo,..SMH...nawajua kuliko unavyodhani ila sina mood ya kutoa maelezo tu
 
Ndoa ni hiari ya muoaji na mwolewaji,hiari ya wazazi ama walezi na kutolewa mahari/engagement.... Kanisani na ukumbini ni mbwembwee...
 
Am nothing to do with dini mm ni mkristu ila aktokea bint wakislam anataka nibadl din nabadl, after al "dini zmeletwa na wazungu" cc tunakomalia dini wkt waletaji hata habar hawana
 
Ufinyu wa mawazo hamna tofauti na mafarisayo ambao Yesu alikua anawashushua...ng'ombe akianguka shimoni sabato hamumtoi??..
Dini yenyewe mpo wachache af mnataka uoe wa dini yako subutuu
Sisi sio kama mafarisayo
Ungefafanua maana ya ng'mbe kuanguka Shimoni. Kuitunza sabato ni Amri si ombi.
Wasabato tupo wengi sana. Ni tamaa tu zinapeleka watu nje.
Hata Samson alioa nje, alichokutana nacho nawe unakijua
 
Waende kwa mkuu wa wilaya ndoa ni ile ile wala hakuna jipya la kufungia kanisani
 
Huko kanisani kwao sijui wanalishwaga nini maana ukimtongoza atataka uache dhehebu lako, ufuate usabato wake.
afu kibaya zaidi wanaamini wenzao wana dhambi then wao pekee ndo wenye haki mbele za Mungu.......wamesahau kwamba tunahesabiwa haki kwa neema kwa njia ya imani.
 
Kwa kuwa wote ni waumini wa biblia takatifu nawaambia kabisa hapo hakuna uchumba wala nini. Wameongozwa na matamaa yao ya kimwili sasa wanajua wazi kuwa hakuna popote watapata suluhisho. Si mchungaji wa KKKT au Sabato ataifunga hiyo ndoa.
Kwa kuwa wote wanaiamini biblia takatifu wasome 2 Kor. 6 : 14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa.....
Kati yao ni nani anaamini sawa sawa na mwenzake?? Hakuna. Basi hawatafanikiwa bali wanapotezeana muda.
Wazo la kimwili; Kijana ajitahidi amtotoe huyo binti. Atalainika tu
 
Kwa kuwa wote ni waumini wa biblia takatifu nawaambia kabisa hapo hakuna uchumba wala nini. Wameongozwa na matamaa yao ya kimwili sasa wanajua wazi kuwa hakuna popote watapata suluhisho. Si mchungaji wa KKKT au Sabato ataifunga hiyo ndoa.
Kwa kuwa wote wanaiamini biblia takatifu wasome 2 Kor. 6 : 14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa.....
Kati yao ni nani anaamini sawa sawa na mwenzake?? Hakuna. Basi hawatafanikiwa bali wanapotezeana muda.
Wazo la kimwili; Kijana ajitahidi amtotoe huyo binti. Atalainika tu
Daah hapo mwisho kweli umetoa wazo la kimwili
 
Imeandikwa

Mwanamume atamwacha baba na mama yake ataambatana na mkewe

Ugumu uko wapi mwambie afuate ushauri wa Mungu huotena bora wote wa mwelekeo mmoja majumba tofauti tuu
Sidhani kama huu mstari ulimaanisha ulichotaka kutuaminisha hapa.

Kuondoka huku ni kusignify kuacha kutegemea wazazi. Hiyo ni sign ya kwanza ya mwanaume aliye tayari kwa ndoa na si kumfuata mkewe...naamini ndiyo maana Biblia ikatumia neno 'kuambatana'.

Kwako mtoa mada: ushauri wa kwanza, mwambie huyo kijana ajiunge huku JF tumshauri vyema itamsaidia na maswali ya nyongeza aliyonayo tutamjibu kinagaubaga.
 
Kwa kukushauri tu, mwambie atafute mtu wa KKKT au dhehebu lolote la Kikristo, Ndoa na Msabato ni pasua kichwa, Msabato hachangamani na Mkristo yoyote, nimeshuhudia mateso makubwa ya ndoa a Msabato na Mkristo (Catholic, KKKT, Mlokole) Kuoa ni mara moja tu na ukikosea ni kila kitu
Umempa ushauri mzuri kabisa. Wakati mwingine hatutakiwi kuruhusu mioyo itutawale tutumie na brain pia
 
Back
Top Bottom