Utata Siku ya ufufuo

Utata Siku ya ufufuo

Akirudi ndio ufufuo unatokea au uliambiwaje hasa ?

Na upi uhusiano uliopo kati ya Yesu na ufufuo ?

''Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.” Ufu. 22:12. “Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko,… nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza… na hivyo tutakuwa na Bwana milele.” 1 Thes. 4:16,17. “Sote tutabadilika, kwa dakika moja, kufumba na kufumbua,… na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu… Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa. Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika…” 1 Kor. 15:51-53.

Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti hitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.” Ufu. 21:4. “Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu.” Ufu. 20:6
 
kwa mungu siku elfu moja ni sawa na siku moja unabii unasema ivo kwaiyo izo siku elfu zilizo pita kwake anaona kama siku mbili tatu ivi kwaiyo ufufuo upo na uzima wa milele upo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sijai pata ng'ombe wala wanyama na madudu wakijadiliana masuala hayo isipokua sisi binadamu, natunapumua vile. si tutulie tuishi maisha yetu bila wasi

Sent using Jamii Forums mobile app
Haya maswali ndo yanasababisha uongo mwiiingi pale binadamu anapoanza kutafuta kabla ya kuzaliwa alikua wapi na akifa ataenda wapi
 
Hiv ni kweli siku ya ufufuo ipo au ni tricky tu ya kutufariji pindi tunapofiwa na ndugu na jamaa ili tuamini ipo siku tutaonana nao paradiso na kama kweli ipo? Maana watu wamefariki miaka zaidi ya Ma elfu iliyopita ila hatujawahi kusikia habari za ufufuo wao au inakuaje? Maana kila siku watu wanazidi kuzaliana na kufa.
Na hata mkionana na ndugu zako siku hiyo hawatotufaa
 
Yaan mtu afe halafu afufuke tena amebaki mifupa mitupu, halafu nyama na sura zirudi tena

Wewe ulishawahi kuona nani amekufa na akafufuka tokea hizo stori zimenza mpk leo hatujaona chochote watu wanakufa na kuzaliwa hakuna anayefufuka tokea miaka hiyo ambao muhamad au yesu alisema
Kama mungu ameweza kukuumba kutokana na ugali(carbohydrate) maharage(protein) ndo zkatengeza mbegu za kiume na kike zkaungana ukawa mwanadamu kamili ukawa na kaili ya kujiunga jamiiforum
ATASHINDWAJE KUKUFUFUA MZIMAMZIMA.
 
Hakuna cha ufufuo wala kwenda motoni au mbinguni;ukishakufa ndio mwisho wako unakuwa umefikia,ila watu wanajipa matumaini ya ufufuo au kwenda mbinguni ili wasiogope kifo.Kwa hiyo kuleni bata mkiwa wazima
 
Hiv ni kweli siku ya ufufuo ipo au ni tricky tu ya kutufariji pindi tunapofiwa na ndugu na jamaa ili tuamini ipo siku tutaonana nao paradiso na kama kweli ipo? Maana watu wamefariki miaka zaidi ya Ma elfu iliyopita ila hatujawahi kusikia habari za ufufuo wao au inakuaje? Maana kila siku watu wanazidi kuzaliana na kufa.
Lipo Tumaini kwa hao waaminio.

Ulimwengu tuliopo unao Muda.na majira yanayotembea kwa kasi.

Lakini Ulimwengu wa kiroho hauna Muda wala Wakati. Maisha yanakua constant Milele na Milele. Yawe mabaya ama mazuri yatakua ya milele na milele.

Ukifa leo na mwingine akafa Miaka 2000 ijayo hakuna aliyewahi ama kuchelewa.

Ujira ni uleule.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiv ni kweli siku ya ufufuo ipo au ni tricky tu ya kutufariji pindi tunapofiwa na ndugu na jamaa ili tuamini ipo siku tutaonana nao paradiso na kama kweli ipo? Maana watu wamefariki miaka zaidi ya Ma elfu iliyopita ila hatujawahi kusikia habari za ufufuo wao au inakuaje? Maana kila siku watu wanazidi kuzaliana na kufa.
Muda huhesabiwa kwa wenye uhai tu.

Lakini wafu hawana saa, wiki, mwezi, mwaka, wala miaka, wao wana 'sasa' peke yake na hawana jana wala kesho.

Ufufuo waweza kuwepo kwa sura tofauti na ufufuo tuliokaririshwa na kuuamini.

Nilichotaka kukueleza tu ni kwamba muda wa kufa hadi kufufuka ni mfupi sana ni sawa na kulizima gari na kuliwasha.

Hivyo hiyo miaka millioni mia tano utakayoishi mavumbini hautahisi kusota hata kidogo.

Utahisi kama ulilala kidogo na kisha kuamka.

Yote kwa yote, ufufuko uwepo au kama kifo ndiyo 'kantolee' basi mwanadamu hautakuwa na ulichopoteza.

Malipo yetu sisi wanadamu ni kumshukuru M/Mungu kwa kutuumba na kututofautisha na viumbe wengine kwa kutupatia akili (utashi) na uhai tutakaopata kuishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom