cosa nostra
JF-Expert Member
- Sep 17, 2010
- 1,773
- 1,801
bashite style
Wasanii, uzeni rekodi nzuri mujulikane badala ya kutegemea vituko kama sehemu ya kujitangaza.Habari wakuu nimekuta bandiko katika ukurasa wa Prof. Jay kuhusu kukamatwa kwa msanii ROMA na kuchukuliwa kwa baadhi ya vitu vya studio ya Tongwe record sijui ni kiki au kweli? Mwenye kujua kinachoendelea
=======
View attachment 491832
Baada ya kuzagaa kwa taarifa kuhusu kukamatwa kwa Msanii Roma Mkatoliki akiwa studio na kupelekwa kusiko julikana, Muungwana Blog imefika katika studio za Tongwe Records jijini Dar es salaam ambapo mkasa mzima ulikuwa hivi...
Kwa mujibu wa Mashuhuda (Majina yanahifadhiwa) walio ambao pia wanaishi katika nyumba ambayo inapatikana studio ya Tongwe, wameijuza Muungwana kuwa April 5, 2017 ambayo ilikuwa ni jana, katika majira ya Saa moja jioni ilionekana gari aina ya Noah nyeusi nje ya studio hizo, ambapo walishuka watu zaidi ya Watano na kuingia ndani ya studio hizo.
Watu hao bila ya kujitambulisha walitamka kuwa wanamuhitaji Roma na mwenzake ambapo walimchukua na kutoka nae nje, na baada ya muda kidogo walirejea ndani na kuwachukua wengine watano akiwemo na Prodyuza wa studio hiyo Anayeitwa Moni.
Mbali na kuwachukua watu hao pia mashuhuda hao wemeeleza baadhi ya vifaa vya studio hiyo pia vimebebwa ikiwemo TV, na Computer.
Kwa Mujibu wa Mwanasheria wa Studio hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Edin ameiambia Muungwana Blog kuwa nikweli tukio hilo limetokea na mpaka sasa hawajui Roma na wenzake wamepelekwa wapi na hivyo hawezi kuelezea zaidi mpaka atakapojua walipo wakina Roma, ambapo aliongeza kuwa anakwenda kuripoti katika kituo cha polisi cha Oysterbay Jijini humo.
Chanzo: Blogs
Umenisaidia mkuu kujibu swali la mheshimiwa hapo juu,Mtu kachukuliwa , eti unasema kiki. Roma atafute kiki gani hapa Tanzania wakati mpaka kuku wanamfahamu.
Mwana mmoja Anaitwa J Murder.Tongwe records inamilikiwa na nani?
Una uhakika gani kuwa wamechukuliwa na polisiHivi unaweza kutafuta kiki kwa kutumia polisi? Wewe utakua na akili ya mende.
Una uhakika gani kuwa wamechukuliwa na polisi
usikumbushe Ben, naweza kulia...!Ben alitoweka ikawa siku , ikawa wiki,Leo ni miezi bila bila.
Namimi najutia sana hizo 10% sijui kilinilaghai kitu gani!heri yako ulikuwa na 10%. never had one and never will. God forbid me from having any