Utata kwenye muungano

Gamba la Nyoka

JF-Expert Member
May 1, 2007
7,022
9,285
(1)Ni dhahiri kuna mambo ya muungano na yasiyo ya muungano, je Pindi Mzanzibari atakapokuwa raisi wa Tanzania nzima, ana uhalali gani wa kuiwakilisha/kutoa maamuzi juu ya mambo yasiyo ya Muungano yanayoihusu Tanganyika?

(2)Maadamu mipaka ya Tanganyika haijawekwa wazi kikatiba, je Raisi wa Tanzania mwenye ajenda ya Uzanzibari ndani yake akiamua kuunda Mkoa mpya wa Tanzania(kwa kushauriana na Raisi wa Zanzibar ofcourse) kwa kuchukua ardhi ya kale ya Tanganyika let say Tanga akaunganisha na Unguja na kuuweka mkoa huu chini ya mamlaka ya serikali ya Zanzibar itakuwaje?.

(3) Ni nini haswa Mtanganyika ananufaika nacho katika Muungano wa style yetu?, tunaona Mzanzibar anaweza kununua ardhi kwa wepesi kabisa mahali popote rasmi ndani ya Tanganyika, anaweza kuomba kupiga na kupigiwa kura ya Uraisi, udiwani, ubunge bila Sharti la Muda maalumu wa Kukaa Tanganyika, Swali ni je Mtanganyika ananufaika na nini kutoka Zanzibar?
 
mmmhh! anyaway,,siku zote natilia mashaka sana sababu zilizopelekea kuungana/muungano.shaka yangu huongezeka kila mara inapojidhihirisha viongozi wa ccm wanapoonekana wazi kutotaka/ruhusu majadiliano juu ya muungano wenyewe na muundo wake wala marekebisho!
 
Huu Muungano haufai kabisa na kwa bahati mbaya kwenye mchakato wa uundwaji wa katiba mpya hawaruhusu kuhoji uhalali wa Muungano. Hii ni fitina ilifanywa na serikali ya Magamba kwa kushirikiana na nyumba ndogo yao (CUF). Lakini wazalendo wa Tanganyika tusirudi nyuma
(1)Ni dhahiri kuna mambo ya muungano na yasiyo ya muungano, je Pindi Mzanzibari atakapokuwa raisi wa Tanzania nzima, ana uhalali gani wa kuiwakilisha/kutoa maamuzi juu ya mambo yasiyo ya Muungano yanayoihusu Tanganyika?

(2)Maadamu mipaka ya Tanganyika haijawekwa wazi kikatiba, je Raisi wa Tanzania mwenye ajenda ya Uzanzibari ndani yake akiamua kuunda Mkoa mpya wa Tanzania(kwa kushauriana na Raisi wa Zanzibar ofcourse) kwa kuchukua ardhi ya kale ya Tanganyika let say Tanga akaunganisha na Unguja na kuuweka mkoa huu chini ya mamlaka ya serikali ya Zanzibar itakuwaje?.

(3) Ni nini haswa Mtanganyika ananufaika nacho katika Muungano wa style yetu?, tunaona Mzanzibar anaweza kununua ardhi kwa wepesi kabisa mahali popote rasmi ndani ya Tanganyika, anaweza kuomba kupiga na kupigiwa kura ya Uraisi, udiwani, ubunge bila Sharti la Muda maalumu wa Kukaa Tanganyika, Swali ni je Mtanganyika ananufaika na nini kutoka Zanzibar?
 
Back
Top Bottom