Auz
JF-Expert Member
- Apr 6, 2016
- 13,221
- 10,944
Wako wazazi walioishia hospitali kwa mshtuko wa hizo taarifa. Utu hakuna, umebaki unyama tu, watu wakiganga njaa zao.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app
Tahadhari kwa wazazi, huu ni utapeli mpya umeibuka! - JamiiForumsAsubuhi hii baada ya kumpeleka mtoto shule nikapokea ujumbe huu wa simu:
"Habari ya saa hii mzazi uongozi wa shule tunapenda kukujulisha kwamba mwanao amepatwa na tatizo la ghafla huku shuleni. Kwa sasa tupo naye hospital mimi ni mwalimu"
Simu iliyotuma ujumbe huo ni 0712578670
Kila nilipojaribu kuipigia simu hii ilikuwa either busy au ilikuwa haipokelewi. Wapo hospitali gani ilikuwa mtihani mwingine.
Akili ikanituma kuwahi shule. Shuleni nilipofika, walimu walishangaa kwa kutokuwa na taarifa zozote kuhusiana na ujumbe huu na pia hapakuwa na tukio lolote lenye kuhusisha hospitali.
Jambo la kushukuru Mungu nimemwona mtoto yuko darasani bukheri wa afya.
Hali hii inatupeleka wapi?
Ninaandika haya huku mwili ungali wanitetemeka. Japo nashukuru Mungu halikuwa jambo la kweli lakini sidhani kuwa ilikuwa fair kuni subject kwenye degree hiyo ya stress.
Mamlaka husika zitulinde dhidi ya matepeli hawa.
Sent using Jamii Forums mobile app