Utapeli mpya Magufuli Terminal

Wadau napenda kuwajulisha kuwa mnapofika katika stand hii na kama unataka kusafiri usiku kuwa kutumia magari maarufu kama IT na hasa ukishukia stand ya daladala unakutana na wapiga debe wanaotangaza kuwa kuna magari ya IT wakati si kweli.

Wanachofanya wanakuchukua hadi ndani ya kituo cha Magufuli kwenye ofisi za kukatia tiketi mabasi na kukuhakikishia kuwa kuna basi linaloondoka usiku huo huo wakati si kweli.

Stand ya Magufuli hakuna basi lolote linaloruhusiwa kuondoka usiku yote yanaondoka asubuhi kuanzia saa 12.

Mi yamenikuta nikaenda hadi kituo cha polisi lakini hakuna msaada wowote wa maana na inaonekana mapolisi wanajua mchezo huu na hawaonyeshi kuukomesha wma wameshindwa au wanalambishwa asali na wahusika.Hali hii wadau inasababisha usumbufu mkubwa usio wa lazima.Serikali ipige marufuku kabisa wapiga debe ambao wanaendelea kuwa kero sana kwa abiria.

Pia inaonekana hata tiketi za mtandaoni bado ni issue isiyo ya lazima kwa hawa jamaa.Kwa kifupi kunahitajika kampuni ya kusimamia logistics zote za stand ili kuleta tija na hadhi ya stand hii ya kimataifa.
Duh, pole kwa kuja Dar jana na kutapeliwa hapohapo. IT zinapita Magufuli Stand na unatoa pesa hujaona wala kuingia kwenye gari!!!
Karibu mjini!!
 
Wapiga debe wapigwe marufuku kabisa ni chanzo kikuu cha uvivu na kichaka kikubwa cha uhalifu.
 
Wewe ni mshamba hapo hauna hoja kabisa walikuona zoba ukaingizwa kingi na kama mjanja huwezi kutoa pesa bila kuona basi na hasa likiwa na abiri

Wadau napenda kuwajulisha kuwa mnapofika katika stand hii na kama unataka kusafiri usiku kuwa kutumia magari maarufu kama IT na hasa ukishukia stand ya daladala unakutana na wapiga debe wanaotangaza kuwa kuna magari ya IT wakati si kweli.

Wanachofanya wanakuchukua hadi ndani ya kituo cha Magufuli kwenye ofisi za kukatia tiketi mabasi na kukuhakikishia kuwa kuna basi linaloondoka usiku huo huo wakati si kweli.

Stand ya Magufuli hakuna basi lolote linaloruhusiwa kuondoka usiku yote yanaondoka asubuhi kuanzia saa 12.

Mi yamenikuta nikaenda hadi kituo cha polisi lakini hakuna msaada wowote wa maana na inaonekana mapolisi wanajua mchezo huu na hawaonyeshi kuukomesha wma wameshindwa au wanalambishwa asali na wahusika.Hali hii wadau inasababisha usumbufu mkubwa usio wa lazima.Serikali ipige marufuku kabisa wapiga debe ambao wanaendelea kuwa kero sana kwa abiria.

Pia inaonekana hata tiketi za mtandaoni bado ni issue isiyo ya lazima kwa hawa jamaa.Kwa kifupi kunahitajika kampuni ya kusimamia logistics zote za stand ili kuleta tija na hadhi ya stand hii ya kimataifa.
Pole sana NDUGU. Na Asante Kwa kutoa angalizo. Hapo kuna watu hawatimizi wajibu wao. Pengine wanasubiri yule Mr. President afufuke awaambie Cha kufanya maana alitoa angalizo kuhusu jina lake kutumika kama jina la kituo hicho! Naona sasa wanaanza kuchafua jina lake.
 
Mimi nafahamu. IT stands for in transit
Ila nimeishawasikia watu wa Dar waki-refer gari yoyote ya binafsi kama IT. Otherwise, unaendaje ndani ya stendi ya Magufuli kutafuta gari ya IT?
Dar ipi iyo?
 
Polisi walio stendi hawana msaada wowote kwa abiria pale anapofanyiwa uhuni, iwe na basi au wapiga debe au wakatisha tiketi
 
Hii nchi ina viongozi wa ajabu sana, kwa nini daradara ipitie pale stendi ya magufuli lakin mtu anayeenda pale stendi kupanda gari za mikoani anaenda kushushiwa stendi ya daradara kule? Au lengo lenu ni kuhakikisha tu lile daraja la juu linatumika? Hivi mnapopanga mipango yenu mnaenda kujaribu kupita huo mlolongo au mnakaa maofisini kwenye kiyoyozi ndo mnapanga? Nyie mnasafili kwa magari binafsi ndo maana hamuoni kadhia hizi. Wekeni kituo cha daradara pale ili anayeenda mikoani ashuke palepale akapande gari acheni kutesa wananchi
 
IT ziko bandarini, chang’ombe, Buguruni, kibo, mbezi stand nje uelekeo wa moro, kibamba shule, maili moja, misugusugu, kongowe na kuendelea, na huwezi kutoa nauli hujaingia kwenye gari hapo kuna costa za hakuna kulala za uyole to dar, au dar to mbeya, au arusha na moshi to Dar au dar to arusha na moshi na zote hua zina parking zake zinazoeleweka anzia kidongo chekundu,
Wewe ndiyo umemsaidia maana wengine wanamzodoa tu
 
Bwanamkubwa we ni mgeni daslama, hayo magari huwa tunayadakia pale kimara kituo ya kwanza tu ukimalizaiza ubungo sijui wanaitaje pale, hata zile coster zinaitwa hakuna kulala zinakuwepo pale... MAGUFULI UMEENDA KUFANYA NINI?
 
Hayo ni magari yaliyosajiliwa rasmi kwa ajili ya kusafirisha abiria wenye shughuli zao binafsi.

Yaani kama unataka kusafirisha msiba, au kusafirisha kundi la watu fulani kutoka sehemu moja kwenda nyingine, mnakodi kwa makubaliano maalum.
asante
 
Ungeenda zako kibo ungekua special Hire za kutosha za uhakika.
Kabisaa
pale Rombo IT za kutosha... Jamaa sijui mgeni wa jiji
anakua kama mdogo angu aliniuliza kwenda zanzibar kwa boti bei gani nikamjibu, akauliza tena na bei ya bus je? afu ndani ya mwendokasi nilijiskia aibu kwa ajili yake
 
Back
Top Bottom