maju
Senior Member
- Oct 20, 2011
- 118
- 28
Watanzania wenzangu kuna wizi mpya unaotumiwa na kampuni inayotoa huduma kushirikiana na makampuni yetu ya simu za mnkononi inayojitangaza kupitia radio ya clouds FM, kwamba wanauza magari, viwanja , kupangisha nyumba na kutafutia watu kazi.Utafiti uliofanyika umeonesha dhairi hii kampuni ni ya kitapeli na haina uwezo huo technically.Hawa wahuni wanachofanya ni kumiliki namba ya SHORT CODE mfano; 155xx ect, ambayo hutolewa ana TCRA kisha kuisajili kwenye makampuni ya simu ili wagawane mapato kwa kila sms zipitiazo kwenye SHORT CODE hiyo (kila sms Tshs. 500). Kisha huitangaza kwa nguvu zote kwenye Radio station husika. Mtanzania anayetuma sms huliwa pesa zake wakati hawa jamaa hawana hata database ya huduma husika, hata ofisi zao hawana hata miundombinu zaidi ya komputa ya muhudumu wa ofisi. Mwisho wa siku hawa jamaa hupitia kwenye makampuni ya simu kufuatilia sms zilizoingia ili wapate mgawo wao. Nawasihi watanzania tuwe makini na hizi promosheni za wizi zinazopitia short code zitolewazo na tcra kwenye simu za mkononi. Na TCRA wawe makini na watu wanaowapatia hizi short code kwani watanzania wanazidi kuibiwa na hawa matapeli.