Wanabodi Ijumaa Kareem
Natumaini sote tuko poa.
Kuna jambo nimekuwa nikiliona kwenye maofisi mengi ambamo nimepitia na nilipojaribu kuwauliza baadhi ya marafiki zangu wafanyao kwenye ofisi zingine nao kwa bahati mbaya wamekiri kuliona. Jambo lenyewe ni lile la baadhi ya staff wafanyao sehemu moja kuwa na mazoea ya kuitana 'mchumba', 'husband', 'wife'.n.k.
Inawezekana ni jambo la heri tu ..lakini kuna wakati inaletaga utata hasa mahusiano yanapoanza kuwa kama routine. Kiasi cha wengine hadi kuandamana sehemu za lunch pamoja na kuseviana kwenye simu kwa identities kama hizo hapo juu. Sababu za wengi wao kuitana hivi utasikia..'kafanana na mume wangu,'ana jina kama la mke wangu' au utasikia 'yupo kama boyfriend wangu' n.k . Hapa najiuliza tu kuwa ni sahihi kuendekeza hizi identities maofisini??..Make kama sikosei kuna kimsemo cha wahenga kwamba 'Maneno huumba'..Au iko poa tu wakubwa???
dah we nae una ka wivu....sasa wao wakiitana hivi unakwazika?au we hakuna anaekuita ita?
haiko poa wala nini we kama ni Juma utaseviwa Juma tu
sa nikusave "baby" hata mpenzi wako akiona unamwambiaje mbambiaje
mazoea yasivuke mipaka.....we SHOULD HAVE LIMITS
Na ukikuta yeye kakusevu 'mchumba'?...kisa jina lako limefanana na la mchumbaake??
Kwa upande wangu nafikiri utani wa namna hiyo haufai hata kidogo kwani,kamwe huwezi jua fikra za mtu mtu,huenda wewe ukachukulia kama utani lakini mwenzio anamaanisha anachokisema,na pia tujiulize ikiwa umo ndani ya ndoa unafikiri unamjengea heshima mumeo/mkeo kwa majina hayo?au ikiwa utasikia mwenzi wako anatumia majina hayo kazini kwake utaona poa tu?na pia vipi watu wanaowazunguka wanaamini ni utani tu au majina hayo yanasababisha wawaangalie kwa jicho lingine?so as for mi majina hayo ni big NO.
Kaka sina wivu banaa
Nimeuliza tu manake juzijuzi na mimi mtu mmoja alishaanza kuniita 'hubby' ..ikabidi niyeyushe.
kozo okamoto em tuongee kiutu uzima na kutoka moyoni bila kuficha ndo umkute mkeo yuko bize kuitana na juma mchumba mume wangu huko kazini kwake utaona poa tu?sema ukweli wako.