Utani msibani

Utani msibani

Dr Aluta

Senior Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
121
Reaction score
39
Hivi huu utani msibani una mantik? Maana inafikia hatua mtu anazuia mpaka maiti! Jaman ifikie hatua tutumie akili zetu sawasawa.

Maana mtu una uchungu kisha mtu anakutania we ndo umemuua maiti.

Hivi hili jambo asili yake nini? Mwenye hoja makini naomba adadavue.

Nawasilisha
 
Usiombe kushuhudia utani wa Mjaluo na Mhaya.Ila makabila mengine yashazoea wanaona ni kawaida tena ukileta hasira unapigwa faini.
 
utani pamoja na kusaidia ktk majukumu ya msibani lakini huwafanya wafiwa kulia kwa uchungu zaidi hivyo 'kumaliza machozi' mapema jambo linaloshauriwa kisayansi kwamba usibane kilio na kulia nusu nusu au kimyakimya. Pia husaidia kukemea tabia mbovu
iongoni mwa wafiwa kwani hata uwe una hadhi gani msiba hutumika kama jukwaa huru la kukemea maovu serious kwa njia ya utani. PROUDLY AFRICAN
 
Hii ilitokea sehemu moja mkoani Mara kama sikosei ilikuwa mwezi march mwaka huu ulikuwa utani kati ya wajaluo na wahaya aliyekuwa amefariki ni mbaba mtu mzima ambaye ni mhaya sasa muda wa historia halisi ya marehemu ukafika ikasomwa wakati msomaji anamalizia wakatokea wajaluo na kumnyanganya mic na kuanza kutangaza pale msibani kwamba historia ya marehemu mliyosomewa awali ni ya uongo.sisi ndo tuna historia halisi akaanza kusoma marehemu fulani bin fulani ya kijaluo alizaliwa shirati mwaka ......alitorosha binti yetu aitwaye ....hd hivi sasa ......dah watu walikuwa na majonzi jeneza likiwa nje tayari kwa safari ya kuelekea Bukoba huku wengine mbavu hawana.
 
Ni mambo ya kijinga sana,unasubiri msiba ndio uutumie kama jukwaa la marekebisho,huo ni uchakavu wa fikra hasa katika dunia ya sasa hivi.Tena cha ajabu mambo kama hayo yanafanywa na watu waliostaarabika ni non sense.Kusubiri msiba ili ufanye marekebisho ni dalili za upuuzi uliokithiri
 
utani pamoja na kusaidia ktk majukumu ya msibani lakini huwafanya wafiwa kulia kwa uchungu zaidi hivyo 'kumaliza machozi' mapema jambo linaloshauriwa kisayansi kwamba usibane kilio na kulia nusu nusu au kimyakimya. Pia husaidia kukemea tabia mbovu
iongoni mwa wafiwa kwani hata uwe una hadhi gani msiba hutumika kama jukwaa huru la kukemea maovu serious kwa njia ya utani. PROUDLY AFRICAN

Purely not logical;Mtu ana majonzi kamwe hawezi kuzingatia lolote,zaidi ya kufikiria mtu waliyempoteza;Watu siku hizi wanaenda kwa mwendo wa vyama au vikundi vya kufa na kuzikana.Huo ni utamaduni uliojaa unafiki na uzandiki uliotukuka.Watu wanafikia mpaka wanabeza,ni mambo ambayo ni out dated,ya kipuuzi yanayopaswa kuachwa mara moja.Kama kweli una na machungu ya kweli kweli kwa nini usitoe msaada unaoonekana msibani,Utakuta mtu anatoa buku halafu anatoa UTANI ambao umejaa kejeli na bezo;ambazo wakati mwingine zinaweza hata kuhatarisha amani msibani,Huo ni ujinga uliobobea unapaswa kuachwa
 
Purely not logical;Mtu ana majonzi kamwe hawezi kuzingatia lolote,zaidi ya kufikiria mtu waliyempoteza;Watu siku hizi wanaenda kwa mwendo wa vyama au vikundi vya kufa na kuzikana.Huo ni utamaduni uliojaa unafiki na uzandiki uliotukuka.Watu wanafikia mpaka wanabeza,ni mambo ambayo ni out dated,ya kipuuzi yanayopaswa kuachwa mara moja.Kama kweli una na machungu ya kweli kweli kwa nini usitoe msaada unaoonekana msibani,Utakuta mtu anatoa buku halafu anatoa UTANI ambao umejaa kejeli na bezo;ambazo wakati mwingine zinaweza hata kuhatarisha amani msibani,Huo ni ujinga uliobobea unapaswa kuachwa

Ina maana msiba usingetokea;hayo maovu yatakemewaje? Je akifa mtu asiye mtani wako utaendelea kukaa na.Mimi nadhani tutafute namna sahihi ya kukemea maovu, na wala sio kukumbatia mambo ya kijinga yaliyopitwa na wakati.Kama ndo hivyo si huyo mhaya angeenda kuzikwa huko ujaluoni,ili kudumisha huo utani wao ambao hauna maana yeyote.Eti mnazingatia mila,zingine zimepitwa na wakati na wala hazina mantiki ndani yake;zaidi ya kuwa kielelezo cha jinsi alivyo mtu anayeendekeza mambo kama hayo.
 
Hiv huu utani msibani una mantik? mana inafikia hatua mtu anazuia mpaka maiti! jaman ifikie hatua tutumie akili zetu sawasawa. mana mtu una uchungu kisha mtu anakutania we ndo umemuua maiti. hiv hil jambo asili yake nin? mwenye hoja makini naomba adadavue.. nawasilisha...

Utani msibani hauna mantiki yoyote,kwanza wanaangalia na mazingira ya kufanya utani huo,palitokea msiba sehemu fulani ambapo panalindwa,mbona sikuona utani wa kijinga kama wa kunyanganya mic.Msiba ulienda vizuri mithili ya watu walio sehemu za ibada
 
Anyway tutaendelea kukumbushana taratibu mambo yanayopaswa kujiri msibani;hatimaye tutaelewa vizuri watu wote.Kwa ujumla utani hauna mantiki msibani,zaidi ya kuwa- provoke wafiwa;Jambo hili hata mimi binafsi linanikera sana,Yaani utakuta hata muda wa kupumzika unakuwa huna,tena hata kwa wanaosafirisha kwenda mbali na kifo kilipotokea
 
Hiv huu utani msibani una mantik? mana inafikia hatua mtu anazuia mpaka maiti! jaman ifikie hatua tutumie akili zetu sawasawa. mana mtu una uchungu kisha mtu anakutania we ndo umemuua maiti. hiv hil jambo asili yake nin? mwenye hoja makini naomba adadavue.. nawasilisha...

Bila shaka watakuwa wameelewa hasa wale wanaoendeleza utani msibani.Maana haiingii akilini mtu amefiwa eti ndo unapata nafasi ya kurekebisha maovu aliyo nayo.Kwa nini kama una nia njema usimwambie huyo unayemuita mtani wako katika mazingira mengine ya kawaida kama kweli una machungu naye,Unasubiri kipindi cha majonzi ndio umkejeli kwa vineno vyako vya kinafiki kwa daraja unaloliita utani?
 
Bila shaka watakuwa wameelewa hasa wale wanaoendeleza utani msibani.Maana haiingii akilini mtu amefiwa eti ndo unapata nafasi ya kurekebisha maovu aliyo nayo.Kwa nini kama una nia njema usimwambie huyo unayemuita mtani wako katika mazingira mengine ya kawaida kama kweli una machungu naye,Unasubiri kipindi cha majonzi ndio umkejeli kwa vineno vyako vya kinafiki kwa daraja unaloliita utani?

hiv yalianzaje haya madudu?
 
Ustaarabu ungekuwa unauzwa ningewanunulia hata kwa bei mbaya kiasi gani watu kama hao,Hao si watani halisi ni WANAFIKI WANAOFURAHIA MAJONZI NA MATESO WANAOPATA wenzao katika misiba,wanapaswa kuogopwa kama wapiga ramli chonganishi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom