MJENGA
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 884
- 848
Ndugu zangu poleni na majukumu. Leo nimeona tukumbushane jambo muhimu la kuliewa sote Waafrika.
Nimeona tujikumbushe ni wapi wakubwa wa dunia wanatupeleka sisi tuitwao dunia ya tatu. Ni kwamba kuanzia karne ya 14 hadi 16 huko Ulaya tayari vijitaifa (nation states) vilikuwa vimeanza kupata nguvu za kidola na kiuchumi.
Hivyo kwasababu ya ubabe, matumizi ya nguvu kujitanua kidola kuliibuka vita kubwa sana iliyopiganwa kwa takribani miaka 30 huku vita hiyo.kwa upande mwingine ikibebwa na imani ya katoliki dhidi ya waasi wake walioongozwa na Martin Luther.
Mwaka 1648 Uliitishwa mkutano wa amani uitwao Westphalia ambapo vijistate hivyo vilikubaliana mambo kadhaa ikiwemo kusitisha vita na kila mmoja kuheshimu mipaka ya mwingine na kamwe kutoingilia uhuru wa.maswala ya ndani ya nchi mwingine (sovereignty).
Baada ya hapo uchumi wao ulikua sana na kuka wa na hitaji la masoko na wafanyakazi wenye gharama nafuu wa viwandani na mashambani.
Mwaka 1884/1885 waliitana wakubwa hao chini ya Chancellor wa Ujerman Bismack wakatugawana sisi waafrika kwaajili ya kututawala na kupata malighafi za viwanda vyao na nguvu kazi isiyo na gharama.
Hapo ndipo dhana ya utandawazi (globalization ) ilipoanza. Waafrika tulinyonywa sana hadi damu wakati huo. Babu zetu walichukuliwa kwwnda kutumikishwa Ulaya na Amerika.
Kwa mchango wa nguvu kazi za babu zetu na wizi wa malighafi na rasilimali zetu waliweza kuendeleza nchi zao kwa kujenga mifumo imara ya mitaji na faida kwaajili ya maendelwo zaidi.
Ukoloni ulipokwisha miaka ya 1960 wakubwa hao walikaa tena miaka ya 1980 wakasema lazima tuurudishe ukoloni Afrika tena kutokana na kunogewa na wizi na uporaji.
Walikuja na mpango wa marekebisho ya kimfumo (Structural Adjustment Program- SAP) ukiwa ni.mpango uliolenga kuuzima mpango kababmbe wa waafrika kudai marekebisho mapya ya mfumo wa uchumi duniani (New International Economic Order) ambao uliitaka jumuiya ya kimataifa kurekebisha mifumo nyonyaji ya kibiashara kupitia WTO, IMF na WB ili waafrika nao wawe na mazingira sawa ya ushindani wa kibiashara na kiuchumi.
Hivyo SAP ililazimisha waafrika kuhurisha mifumo yao yankiuchumi (liberalozation of economy) kwa kuruhusu masoko huria (free markets) na mfumo wa siasa za vyama vingi.
Wakubwa hao walijua fika kuwa waafrika hatuna uwezo wa kufanya investments kubwa hivyo kwa uhuria huo wa.masoko ungewapa nafasi wao kutawala biashara na shughuli zingine za kiuchumi Afrika.
Aidha kupitia mifumo ya vyama vingi vya siasa walijua kuwa tutagawanyika na hivyo watatutawala kirahisi kupia vyombo vyake vyankinyonyaji vya IMF, WTO na WB. Baada ya kufanikiwa katika maeneo hayo tunashuhudia Afrika ikiwa na migogoro mingi ya kisiasa huku wao wakiendelea kuchota rasilimali zetu kilaini kabisa.
Viwanda vingi vilivyoanzishwa wakati wa mwanzo baada ya uhuru katika nchi.nyingi za Afrika vimekufa si kwasababu nyingine bali kwa mikono ya wakubwa hao kutotaka tupate mifumo imara ya kiuchumi ya kututoa huku tuliko.
Ndugu zangu utandawazi kwa maana halisi si kama watu mnavyoutafsiri kirahisirahisi, huo ni ukoloni kabisa unaotumia nyenzo na vyombo vya kimataifa kuinyonya Afrika.
Madeni makubwa ya nchi za Afrika ambayo yanadaiwa na WB yanatengenezwa kimkakati (si rahisi nikaeleweka hapa) ili nchi za Afrika ziendelee kuwa tegemezi.
Hivyo kwa picha hiyo, ni vema tuelewe malengo ya wazungu kwetu sisi waafrika kuwa siyo.mazuri. Na ni vema mkajua kuwa.wakubwa hao hawapendi.kusikia nchi masikini zinajitambua na kuanza kupambana kujikomboa.
Tanzania ilipo sasa imejitambua na hongera sana Rais Dr. John Pombe Magufuli kwa kuutambua ulaghai wa wakubwa hao na hivyo kuamua kwa dhati kuikomboa Tanzania.
Kelele unazopigiwa kuhusu madai ya udikteta na kujaribu kukuharibia taswira ili uchukiwe na wananchi wako ili mwishowe wao wajihalalishie kukutoa madarakani.
Ninakuomba, simama imara kwani Watanzania wenye akili kama mimi tuko wengi na tunakuunga mkono. Unapoipeleka Tanzania kila mwenye akili timamu anaona.
Kasi ya maendeleo si ya kuridhisha kama tulivyozoea kuimbiwa bali wakati huu kasi ni kubwa kiasi inawatisha wakubwa hao. Pigana Jemedari tuko nyuma yako.
Watanzania wote niwaombe tumuunge mkono Rais wetu na tusikubali kwa namna yoyote adhalilishwe na manyang'au na.majizi. Tumuombee aongoze ukombozi wa kweli.
Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki Africa. Siku si nyingi Afrika itahesabiwa haki na hao wanaotutawala na kutunyonya na kututesa. Mungu amewaandalia mahali pao stahiki.
Nimeona tujikumbushe ni wapi wakubwa wa dunia wanatupeleka sisi tuitwao dunia ya tatu. Ni kwamba kuanzia karne ya 14 hadi 16 huko Ulaya tayari vijitaifa (nation states) vilikuwa vimeanza kupata nguvu za kidola na kiuchumi.
Hivyo kwasababu ya ubabe, matumizi ya nguvu kujitanua kidola kuliibuka vita kubwa sana iliyopiganwa kwa takribani miaka 30 huku vita hiyo.kwa upande mwingine ikibebwa na imani ya katoliki dhidi ya waasi wake walioongozwa na Martin Luther.
Mwaka 1648 Uliitishwa mkutano wa amani uitwao Westphalia ambapo vijistate hivyo vilikubaliana mambo kadhaa ikiwemo kusitisha vita na kila mmoja kuheshimu mipaka ya mwingine na kamwe kutoingilia uhuru wa.maswala ya ndani ya nchi mwingine (sovereignty).
Baada ya hapo uchumi wao ulikua sana na kuka wa na hitaji la masoko na wafanyakazi wenye gharama nafuu wa viwandani na mashambani.
Mwaka 1884/1885 waliitana wakubwa hao chini ya Chancellor wa Ujerman Bismack wakatugawana sisi waafrika kwaajili ya kututawala na kupata malighafi za viwanda vyao na nguvu kazi isiyo na gharama.
Hapo ndipo dhana ya utandawazi (globalization ) ilipoanza. Waafrika tulinyonywa sana hadi damu wakati huo. Babu zetu walichukuliwa kwwnda kutumikishwa Ulaya na Amerika.
Kwa mchango wa nguvu kazi za babu zetu na wizi wa malighafi na rasilimali zetu waliweza kuendeleza nchi zao kwa kujenga mifumo imara ya mitaji na faida kwaajili ya maendelwo zaidi.
Ukoloni ulipokwisha miaka ya 1960 wakubwa hao walikaa tena miaka ya 1980 wakasema lazima tuurudishe ukoloni Afrika tena kutokana na kunogewa na wizi na uporaji.
Walikuja na mpango wa marekebisho ya kimfumo (Structural Adjustment Program- SAP) ukiwa ni.mpango uliolenga kuuzima mpango kababmbe wa waafrika kudai marekebisho mapya ya mfumo wa uchumi duniani (New International Economic Order) ambao uliitaka jumuiya ya kimataifa kurekebisha mifumo nyonyaji ya kibiashara kupitia WTO, IMF na WB ili waafrika nao wawe na mazingira sawa ya ushindani wa kibiashara na kiuchumi.
Hivyo SAP ililazimisha waafrika kuhurisha mifumo yao yankiuchumi (liberalozation of economy) kwa kuruhusu masoko huria (free markets) na mfumo wa siasa za vyama vingi.
Wakubwa hao walijua fika kuwa waafrika hatuna uwezo wa kufanya investments kubwa hivyo kwa uhuria huo wa.masoko ungewapa nafasi wao kutawala biashara na shughuli zingine za kiuchumi Afrika.
Aidha kupitia mifumo ya vyama vingi vya siasa walijua kuwa tutagawanyika na hivyo watatutawala kirahisi kupia vyombo vyake vyankinyonyaji vya IMF, WTO na WB. Baada ya kufanikiwa katika maeneo hayo tunashuhudia Afrika ikiwa na migogoro mingi ya kisiasa huku wao wakiendelea kuchota rasilimali zetu kilaini kabisa.
Viwanda vingi vilivyoanzishwa wakati wa mwanzo baada ya uhuru katika nchi.nyingi za Afrika vimekufa si kwasababu nyingine bali kwa mikono ya wakubwa hao kutotaka tupate mifumo imara ya kiuchumi ya kututoa huku tuliko.
Ndugu zangu utandawazi kwa maana halisi si kama watu mnavyoutafsiri kirahisirahisi, huo ni ukoloni kabisa unaotumia nyenzo na vyombo vya kimataifa kuinyonya Afrika.
Madeni makubwa ya nchi za Afrika ambayo yanadaiwa na WB yanatengenezwa kimkakati (si rahisi nikaeleweka hapa) ili nchi za Afrika ziendelee kuwa tegemezi.
Hivyo kwa picha hiyo, ni vema tuelewe malengo ya wazungu kwetu sisi waafrika kuwa siyo.mazuri. Na ni vema mkajua kuwa.wakubwa hao hawapendi.kusikia nchi masikini zinajitambua na kuanza kupambana kujikomboa.
Tanzania ilipo sasa imejitambua na hongera sana Rais Dr. John Pombe Magufuli kwa kuutambua ulaghai wa wakubwa hao na hivyo kuamua kwa dhati kuikomboa Tanzania.
Kelele unazopigiwa kuhusu madai ya udikteta na kujaribu kukuharibia taswira ili uchukiwe na wananchi wako ili mwishowe wao wajihalalishie kukutoa madarakani.
Ninakuomba, simama imara kwani Watanzania wenye akili kama mimi tuko wengi na tunakuunga mkono. Unapoipeleka Tanzania kila mwenye akili timamu anaona.
Kasi ya maendeleo si ya kuridhisha kama tulivyozoea kuimbiwa bali wakati huu kasi ni kubwa kiasi inawatisha wakubwa hao. Pigana Jemedari tuko nyuma yako.
Watanzania wote niwaombe tumuunge mkono Rais wetu na tusikubali kwa namna yoyote adhalilishwe na manyang'au na.majizi. Tumuombee aongoze ukombozi wa kweli.
Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki Africa. Siku si nyingi Afrika itahesabiwa haki na hao wanaotutawala na kutunyonya na kututesa. Mungu amewaandalia mahali pao stahiki.