ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,128
- 49,863
Miaka 60 Baada ya Ukoloni wa Waafrika tumeendelea kulaumu Wazungu kwa umaskini na migogoro yetu, huku sisi wenyewe hakuna cha maana tunafanya kujikwamua na hali hii.
View: https://twitter.com/africaupdates/status/1719966249482891718?t=hTpdjN24uzeWV8BoTCW2vg&s=19
Just imagine Wazungu waliyoweka mipaka ya Afrika wameiondoa na kuamua kufanya biashara baina yao huku wakitega mitego yao ya kuendelea kuzoa Mali Afrika.
Waafrika tulivyo mbumbumbu tumeamua kushirikiana na wakoloni kuiba Mali zetu wenyewe ila hatutaki kushirikiana wenyewe kwa wenyewe kujenga uchumi wa nchi zetu!
Angalia hii hapa;
- Hakuna miundombinu ya kuunganisha Afrika na Afrika ila tunajenga reli na Bandari kuimarisha kusomba Mali zetu kwenda nje!
View: https://twitter.com/africaupdates/status/1717567065975054762?t=ZcT2erV7rNYlBKUiJMD91A&s=19
- Tumeweka vikwazo vya kufanya biashara baina yetu ila tunafurahia kuwaona Wazungu walitoka kwao kuja Afrika tena kwa Biashara za kawaida kabisa kama kuuza viatu, kuwinda, nk, ambazo tungeweza kufanya wenyewe.
- Ukitaka kusafiri Nchi ya Afrika ni kama unataka kwenda kwenye mwezi, ni complications na costly sana.
View: https://twitter.com/africaupdates/status/1720253510896308558?t=zxu20NsNacsbPp0I7uAvrw&s=19
My Take
Sijajua mtu mweusi anakwama wapi hasa kwenye kujitambua.
Mfano, leo hii ukiangalia takwimu hata za Utalii hapa Tanzania unakuta Waafrika ni wengi, karibu nusu licha ya ugumu wa kusafiri na mavisa na gharama za juu zilizopo. Sasa je, ukiondoa visa unadhani Utalii utainuka kiasi gani?
Waafrika tuache upumbavu, kama tutarihusu free movements watu wawe na IDs tu, sio tu tutakuza Biashara bali hata migogoro na watu wanaokukimbia Nchi zao kwenda Ulaya vitakoma.
Afrika ndio Bara lenye Mali na potential kuliko Bara lolote hapa Duniani ila shida hatuna akili, na wengi wa viongozi ya Afrika ni kama mazombie tu wasiojitambua.
Waafrika wanatakiwa kuelewa kwamba uhusiano na Wazungu ni wa kinyonyaji na sio vinginevyo kulingana na walivyo set toka ukoloni.
Hakuna siku umaskini utaisha bila kubadili hili na ili kubadili lazima Waafrika tuwe na ushirikiano wa kibiashara sio wa kufanya mikutano ya AU Addis Ababa.
Hongera sana Kagame na Ruto Kwa kubaini kinachokwamisha Maendelea ya Africa.
View: https://twitter.com/FactsOnRwanda/status/1720092860828233805?t=3KYFiz9JPKLTGzNPdB9pPQ&s=19
View: https://twitter.com/africaupdates/status/1720253982218625061?t=l7DTEvnXYQpcOzl8q-HPjg&s=19
View: https://twitter.com/africaupdates/status/1719966249482891718?t=hTpdjN24uzeWV8BoTCW2vg&s=19
Just imagine Wazungu waliyoweka mipaka ya Afrika wameiondoa na kuamua kufanya biashara baina yao huku wakitega mitego yao ya kuendelea kuzoa Mali Afrika.
Waafrika tulivyo mbumbumbu tumeamua kushirikiana na wakoloni kuiba Mali zetu wenyewe ila hatutaki kushirikiana wenyewe kwa wenyewe kujenga uchumi wa nchi zetu!
Angalia hii hapa;
- Hakuna miundombinu ya kuunganisha Afrika na Afrika ila tunajenga reli na Bandari kuimarisha kusomba Mali zetu kwenda nje!
View: https://twitter.com/africaupdates/status/1717567065975054762?t=ZcT2erV7rNYlBKUiJMD91A&s=19
- Tumeweka vikwazo vya kufanya biashara baina yetu ila tunafurahia kuwaona Wazungu walitoka kwao kuja Afrika tena kwa Biashara za kawaida kabisa kama kuuza viatu, kuwinda, nk, ambazo tungeweza kufanya wenyewe.
- Ukitaka kusafiri Nchi ya Afrika ni kama unataka kwenda kwenye mwezi, ni complications na costly sana.
View: https://twitter.com/africaupdates/status/1720253510896308558?t=zxu20NsNacsbPp0I7uAvrw&s=19
My Take
Sijajua mtu mweusi anakwama wapi hasa kwenye kujitambua.
Mfano, leo hii ukiangalia takwimu hata za Utalii hapa Tanzania unakuta Waafrika ni wengi, karibu nusu licha ya ugumu wa kusafiri na mavisa na gharama za juu zilizopo. Sasa je, ukiondoa visa unadhani Utalii utainuka kiasi gani?
Waafrika tuache upumbavu, kama tutarihusu free movements watu wawe na IDs tu, sio tu tutakuza Biashara bali hata migogoro na watu wanaokukimbia Nchi zao kwenda Ulaya vitakoma.
Afrika ndio Bara lenye Mali na potential kuliko Bara lolote hapa Duniani ila shida hatuna akili, na wengi wa viongozi ya Afrika ni kama mazombie tu wasiojitambua.
Waafrika wanatakiwa kuelewa kwamba uhusiano na Wazungu ni wa kinyonyaji na sio vinginevyo kulingana na walivyo set toka ukoloni.
Hakuna siku umaskini utaisha bila kubadili hili na ili kubadili lazima Waafrika tuwe na ushirikiano wa kibiashara sio wa kufanya mikutano ya AU Addis Ababa.
Hongera sana Kagame na Ruto Kwa kubaini kinachokwamisha Maendelea ya Africa.
View: https://twitter.com/FactsOnRwanda/status/1720092860828233805?t=3KYFiz9JPKLTGzNPdB9pPQ&s=19
View: https://twitter.com/africaupdates/status/1720253982218625061?t=l7DTEvnXYQpcOzl8q-HPjg&s=19