Utamu wa mabinti walio okoka


Hapo kwenye red,
Jihadhari usije ukapotea.
Kwenye Biblia kuna andiko moja linasema 'usiibe', sasa wewe unasema tusi-base kwenye andiko moja ??
Ina maana kwenye Biblia kuna andiko lingine linaweza kuruhusu kuiba ??.
Kumbuka, Neno la Mungu ni amri, usibadilishe ili kujifariji.
 

Hapo kwenye red,
Una maana Biblia haijakataza kusuka nywele na kuvaa mapambo ??
Hebu nukuu hiyo sehemu ya Biblia inayoruhusu kusuka nywele na kuvaa mapambo !!!
Kumbuka, Neno la Mungu ni amri, usipindishe na kulainisha hata kidogo.
 

Hapo kwenye Imani, ni lazima iambatane na matendo yanayo-support imani husika.
Ukimwamini Yesu, matendo yako lazima yaonyeshe Imani hiyo, yaani matendo yako yatafuata amri zake Yesu unayemwamini.

Biblia inasema hivi katika Yakobo 02:14-26....

14 Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa?
15 Ikiwa ndugu mwanamume au ndugu mwanamke yu uchi na kupungukiwa na riziki,
16 na mtu wa kwenu akawaambia, Enendeni zenu kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini asiwape mahitaji ya mwili, yafaa nini?
17 Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake.
18 Lakini mtu atasema, Wewe unayo imani, nami ninayo matendo. Nionyeshe imani yako pasipo matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.
19 Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka.
20 Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai?
21 Je! Baba yetu Ibrahimu hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipomtoa Isaka mwanawe juu ya madhabahu?
22 Waona kwamba imani ilitenda kazi pamoja na matendo yake, na ya kwamba imani ile ilikamilishwa kwa njia ya matendo yale.
23 Maandiko yale yakatimizwa yaliyonena, Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa ni haki; naye aliitwa rafiki wa Mungu.
24 Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake.
25 Vivyo hivyo na Rahabu, yule kahaba naye, je! Hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipowakaribisha wajumbe, akawatoa nje kwa njia nyingine?
26 Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa.
 

ukitaka kuifaidi maandiko ktk Biblia fuatilia hilo andiko lilitolewa na nani, kwa watu gani waliokuwa katika mazingira gani, mji gani, nk. otherwise utakuwa kama unakariri andiko bila kujua real meaning! ngoja nikupe mfano wa maandiko...Usiue ni amri ya Mungu (Kutoka 20:13 "You shall not murder"), sasa una habari unaweza ukawa umeokoka lakini ukawa muuaji? maybe utasema HAIWEZEKANI kwa vile uuaji ni kutoa uhai wa mwili wa mtu. fine, twende 1Yohana 3:15 "Anyone who hates his brother ia a murderer, and you know that no murderer has eternal life ini him'. unaona jinsi maandiko yanavyotegemeana?!!! anyway believe what you believe!
 
Hapo kwenye red,
Una maana Biblia haijakataza kusuka nywele na kuvaa mapambo ??
Hebu nukuu hiyo sehemu ya Biblia inayoruhusu kusuka nywele na kuvaa mapambo !!!
Kumbuka, Neno la Mungu ni amri, usipindishe na kulainisha hata kidogo.

nimekujibu hili swali katika post yangu niliyokunukuhu! aidha, nimesema amini unavyoamini basi lakini usituaminishe eti kuvaa nguo za thamani na dhahabu ni dhambi. hiyo haipo katika zile amri kumi ambazo Mungu aliziandika ktk mbao mbili za mawe, wala haimo ktk summary ya Bwana Yesu kwamba 'mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako....., mpende jirani yako kama nafsi yako'! fuatilia maandiko hayo kwa nini Paulo aliyatoa kwa kanisa husika na mazingira ya wakati huo yalikuwaje? mpendwa fuatilia kwa makini unayoyaamini maana kuna wachungaji feki wanapotosha maandiko kwa maslahi yao!
 

Ukiwa umeokoka huwezi kumchikia ndugu yako, maana amri kuu kuliko zote ni upendo.
Yaani kuwapenda watu wote hata adui zetu tuwapende.
Ukiona jamaa anasema ameokoka halafu anamchulia mtu, huyo wokovu hauko kwake, maana akakuwa kishavunja amri ya Upendo.
Wokovu sio mchezo, watu wanadhani kuokoka ni kutamka tu kuwa umeokoka.
Kuokoka ni kumkiri Yesu kuwa ni Bwana, na kufuata amri, maagizo na maelekezo yake YOTE.
Maana ukikosa kwenye amri moja umekosa kwenye amri zote.

Angalia hapa...

Mathayo 05:43-48 inasema...

43 Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.


Yakobo 02:08-11 inasema...

8 Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako, mwatenda vema.
9 Bali mkiwapendelea watu, mwafanya dhambi na kuhukumiwa na sheria kuwa wakosaji.
10 Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.
11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria.
 
Mr. President napingana na wewe uso kwa uso; kauli yako si kweli! Nipe mifano ya waliookoka ambao maisha yamewashinda nami nitakupa walioyashinda maisha na wako vizuri katika kila kitu!
 

Wewe ni msabato?

Ukikurupuka kuanzisha ubishi hakuna mashindano ya sheria wala kukariri vifungu vya Biblia hapa. Yawezekana ulisoma ukitafuta sehemu ya kukosoa kiasi ukasahau kuona nilichokusudia kumueleza aliyeuliza swali.

Nilipomwambia ajisomee Mathayo 19:16-26 nilikuwa namjibu hilo swali lake kuhusu matendo na nilipomwambia imani yake inatosha, usifikiri nilikosea, nilimaanisha. Contradictions hazitaisha kwa matendo, bali kwa imani.

Imani chanzo chake ni kusikia: Basi imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo. Warumi 10:16

Nenda usome Mathayo:19:16-26 ndio utapata ujumbe wote niliomweleza, kuanzia katikati hakutakusaidia kuelewa.
 
Huyu hawezi okoka. Maana wazee wa kanisa na wachungaji lazima watachombeza tu. Ni bora abaki huko huko mitaani.

Huyu akiwa kweli kaokoka nami nitaanza sali kwenye hilo kanisa! Nawajua ndugu zangu hawa huwa hawana neno pale wanapogundua utatunza siri!!!
 

Mpendwa, mimi nafuatilia sana Maandiko ya Biblia, ndio maana sidanganywi na mtu yoyote.
Nasoma sana Biblia ili nisidanganywe.
Mtu asikwambie kitu chochote katika Imani ya Kikristo bila kuthibitisha kwenye Maandiko.
Mtu anaweza kukwambia kuwa kufanya jambo fulani ni sawa tu, nawe ukakubali bila ya kuangalia Maandiko.

Paulo Mtume alishatuonya mapema kuhusu kubadilisha Neno la Mungu na kuchuja Injili...
Paulo Mtume alisema hivi katika Wagalatia 01:06-12 akisema....

6 Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine.
7 Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo.
8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe.
9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe.
10 Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.
11 Kwa maana, ndugu zangu, injili hiyo niliyowahubiri, nawajulisha ya kuwa siyo ya namna ya kibinadamu.
12 Kwa kuwa sikuipokea kwa mwanadamu wala sikufundishwa na mwanadamu, bali kwa ufunuo wa Yesu Kristo.
 
hujui usemalo

 
ngoja nikawanawishe hizo nyuso kwanza ndo ujue vyema fn ya make up lol... Sio hizi za kibongo tunajikandika kama matope .....mfano: kuna bidada mmoja wa star tv wa kipindi cha sanaa blaa blaaa full kujichubua na make upo anakandika kama nyumba ya udongo lol
 

hapa lazima mabinti wapite kama hawapajuu
 

hapa lazima mabinti wapite kama hawapajui
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…