Salahan
JF-Expert Member
- Sep 10, 2014
- 2,942
- 3,606
UGUMU WA MAISHA HUANZIA AKILINI MWAKO.
Ebu fikiria Dada anayechoma mahindi maeneo ya Manzese Darajani kuanzia saa 12 jioni mpaka SAA 2 usiku, kwa siku moja anauwezo wa kuchoma mahindi .50. Kila hindi moja ananunua shambani kwa shilingi 100/- Na Anauza kwa sh.600/-
Hiyo ina maana mahindi 50 ananunua kwa shilingi 5000/- akichoma na kuuza anapata sh.30,000/-. Akitoa pesa ya mtaji (5000/- ya mahindi na 1500/- ya mkaa) anabakiwa na sh.23,500/- kwa siku.
Hivyo kwa mwezi huyu mchoma mahindi atakuwa ameingiza kiasi cha sh.705,000/-
Mwalimu mwenye Degree anayeanza kazi analipwa 584,000/- akikatwa kodi pamoja na makato mengene ya mifuko ya jamii anabakiwa na sh.425,000/.
Tofauti ya Mwalimu wa degree na Muuza mahindi ni
Kuwa Mwalimu kanaajiriwa,
muuza mahindi kajiajiri.
Mwalimu anafanya kazi masaa 9 kwa siku (saa2 asubuh hadi 11jioni)
muuza mahindi anafanya kazi masaa matatu kwa siku (saa 12 jioni hadi 2 usiku).
Mwalimu anatumia muda wake wa ziada kusahihisha mitihani na homework,
mchoma mahindi anatumia muda wake wa ziada kutafuta fursa nyingine za kupata hela zaidi..
UOGA WAKO NDIO UMASKINI WAKO..