Shebbydo
JF-Expert Member
- Feb 12, 2015
- 1,174
- 1,937
Utafiti huu umefanywa nchini Ujerumani kwa ushirikiano wa Wanasaikolojia, madaktari wa binadamu na chuo kikuu cha Technische Universitat of Berlin. Utafiti huu ulisimamiwa na daktari Berthold Ackermann.
Utafiti ulifanywa kwa watu 944 ambao walijitolea wenyewe kwa vipindi tofauti tofauti ndani ya miaka minne.
Mchanganyiko wa dawa za epinephrine na dimethyltryptamine zilitumika kwa ajili ya kuufisha mwili kwa muda wa dakika 20 wakati utafiti unafanyika. Mashine ya CardioPulmonary Recitation ilitumika kusisimua tena mapigo ya moyo ya watu hao waliokuwa wakifanyiwa utafiti.
Matokeo yaliyotokana na utafiti huu hayakutofautiana sana miongoni mwa wafanyiwa utafiti. Kwa maelezo ya kile walichokiona watafitiwa wakati walipokuwa katika hali ya kifo ni;
Kuona hali ya kuuacha mwili(detachment from the body), kuhisi kuelea hewani(feelings of levitation), Kujisikia amani kabisa(total serenity), usalama(security) na uwepo wa mwanga mkali sana(overwhelming light).
Mbali na utafiti huu uliofanyika Ujerumani pia kuna ushuhuda ambao uliwahi kutolewa na mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Pam Reynoild. Mama huyu alipatwa na ugonjwa uitwao Basilar Artery Aneurysm unaosababishwa na mshipa uliopo nyuma ya ubongo(Basilar Artery).
Ushuhuda huu upo kwenye kitabu cha daktari aliyekuwa akimfanyia utafiti mwanamke huyu, Dr. Michael Sabom, kiitwacho Light and Death.
Dr. Michael baada ya kugundua tatizo la Bi. Pam, alimrufaa kwa daktari ambaye alikuwa ni "specialist" wa upasuaji wa ubongo wa ugonjwa huu upasuaji ambao ni hatari na hufanyika mara chache. Upasuaji huo unafahamika kwa jina la Hypothermic Cardiac Arrest lakini ulipewa jina la utani la "Standstill".
Ili upasuaji huu ufanyike mgonjwa lazima afanyiwe taratibu zifuatazo(Procedures):
1:Jotoridi la mwili lazima lishushwe hadi nyuzi 16 za centigredi kutoka nyuzi 36.6 za centigredi.
2:Mapigo ya moyo na kupumua kuzuiliwe.
3amu iondolewe kwenye kichwa na
4:Ubongo usifanye kazi.
Kwa kifupi ni kufa ndani ya muda fulani.
Kwa mujibu wa Bi. Pam baada ya kufanyiwa mambo haya kwenye upasuaji wake, ulifika wakati akajiona anatoka kwenye mwili wake halisi na kukaa pembeni. Aliweza kuona jinsi madaktari walivyokuwa wakiufanyia mwili wake upasuaji. Akiwa pembeni alisikia sauti zikimwita "njoo" lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida. Alianza kusogea huku akiwa ameuacha mwili wake pale kitandani ukifanyiwa upasuaji akielekea kulikokuwa na zile sauti ambazo alianza kuzitambua, mojawapo ikiwa ni sauti ya bibi yake aliyefariki kipindi cha nyuma.
Sauti hizo ambazo zilikuwa zikitoka kwenye mwanga mkali alipozifikia ndipo aliweza kuwaona ndugu zake mbalimbali ambao walishafariki. Bi. Pam alitaka kuingia katikati ya ule mwanga mkali lakini baba yake mdogo ambaye naye alikuwa miongoni mwa wale watu aliowaona alimzuia akimwambia kuwa endapo akiingia katika mwanga huo hawatakuwa na uwezo wa kumrudisha kwenye mwili wake.
Baba yake mdogo ndiye aliyemchukua na kumrudisha pale ulipokuwa mwili wake. Kwa mujibu wake Bi. Pam anasema hakutaka kurudi kwenye mwili wake ule kwa jinsi alivyokuwa akijisikia amani katika huo ulimwengu mpya. Anafananisha kurudi kwenye mwili wake halisi na tukio la kujitupa ndani ya bwawa la kuogelea.
Je, kweli kuna maisha baada ya kifo? Ama ni mkanganyiko unaotokea kwenye ubongo? Lakini kwa mujibu wa madaktari waliokuwa wakimfanyia upasuaji, vifaa kama electroencephalogram(EEG) ambacho hutumika kuonesha ubongo kufanya kazi kilionesha ubongo umesimama kufanya kazi na vipimo vingine vilionesha hakuna damu iliyokuwa ikienda kwenye ubongo.
Hii inaweza kuwa kama hadithi ya kutunga lakini tuunganishe dot katika haya. Je, umewahi kuwa karibu na mtu ambaye anataka kukata roho huku akisema kuna watu wanataka kumchukuwa? Mimi binafsi niliwahi kuwa karibu wakati mjomba wangu anafariki alikuwa akiniambia nimshike mkono nimvute kuna watu wanataka kumchukua.
Vipi kuhusu watu wa meditation hasa astral body projection, vinahusiana vipi na hii hali iliyosimuliwa na Bi.Pam Reynoild?
Kuna mengi ya kujifunza katika dunia hii.
Utafiti ulifanywa kwa watu 944 ambao walijitolea wenyewe kwa vipindi tofauti tofauti ndani ya miaka minne.
Mchanganyiko wa dawa za epinephrine na dimethyltryptamine zilitumika kwa ajili ya kuufisha mwili kwa muda wa dakika 20 wakati utafiti unafanyika. Mashine ya CardioPulmonary Recitation ilitumika kusisimua tena mapigo ya moyo ya watu hao waliokuwa wakifanyiwa utafiti.
Matokeo yaliyotokana na utafiti huu hayakutofautiana sana miongoni mwa wafanyiwa utafiti. Kwa maelezo ya kile walichokiona watafitiwa wakati walipokuwa katika hali ya kifo ni;
Kuona hali ya kuuacha mwili(detachment from the body), kuhisi kuelea hewani(feelings of levitation), Kujisikia amani kabisa(total serenity), usalama(security) na uwepo wa mwanga mkali sana(overwhelming light).
Mbali na utafiti huu uliofanyika Ujerumani pia kuna ushuhuda ambao uliwahi kutolewa na mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Pam Reynoild. Mama huyu alipatwa na ugonjwa uitwao Basilar Artery Aneurysm unaosababishwa na mshipa uliopo nyuma ya ubongo(Basilar Artery).
Ushuhuda huu upo kwenye kitabu cha daktari aliyekuwa akimfanyia utafiti mwanamke huyu, Dr. Michael Sabom, kiitwacho Light and Death.
Dr. Michael baada ya kugundua tatizo la Bi. Pam, alimrufaa kwa daktari ambaye alikuwa ni "specialist" wa upasuaji wa ubongo wa ugonjwa huu upasuaji ambao ni hatari na hufanyika mara chache. Upasuaji huo unafahamika kwa jina la Hypothermic Cardiac Arrest lakini ulipewa jina la utani la "Standstill".
Ili upasuaji huu ufanyike mgonjwa lazima afanyiwe taratibu zifuatazo(Procedures):
1:Jotoridi la mwili lazima lishushwe hadi nyuzi 16 za centigredi kutoka nyuzi 36.6 za centigredi.
2:Mapigo ya moyo na kupumua kuzuiliwe.
3amu iondolewe kwenye kichwa na
4:Ubongo usifanye kazi.
Kwa kifupi ni kufa ndani ya muda fulani.
Kwa mujibu wa Bi. Pam baada ya kufanyiwa mambo haya kwenye upasuaji wake, ulifika wakati akajiona anatoka kwenye mwili wake halisi na kukaa pembeni. Aliweza kuona jinsi madaktari walivyokuwa wakiufanyia mwili wake upasuaji. Akiwa pembeni alisikia sauti zikimwita "njoo" lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida. Alianza kusogea huku akiwa ameuacha mwili wake pale kitandani ukifanyiwa upasuaji akielekea kulikokuwa na zile sauti ambazo alianza kuzitambua, mojawapo ikiwa ni sauti ya bibi yake aliyefariki kipindi cha nyuma.
Sauti hizo ambazo zilikuwa zikitoka kwenye mwanga mkali alipozifikia ndipo aliweza kuwaona ndugu zake mbalimbali ambao walishafariki. Bi. Pam alitaka kuingia katikati ya ule mwanga mkali lakini baba yake mdogo ambaye naye alikuwa miongoni mwa wale watu aliowaona alimzuia akimwambia kuwa endapo akiingia katika mwanga huo hawatakuwa na uwezo wa kumrudisha kwenye mwili wake.
Baba yake mdogo ndiye aliyemchukua na kumrudisha pale ulipokuwa mwili wake. Kwa mujibu wake Bi. Pam anasema hakutaka kurudi kwenye mwili wake ule kwa jinsi alivyokuwa akijisikia amani katika huo ulimwengu mpya. Anafananisha kurudi kwenye mwili wake halisi na tukio la kujitupa ndani ya bwawa la kuogelea.
Je, kweli kuna maisha baada ya kifo? Ama ni mkanganyiko unaotokea kwenye ubongo? Lakini kwa mujibu wa madaktari waliokuwa wakimfanyia upasuaji, vifaa kama electroencephalogram(EEG) ambacho hutumika kuonesha ubongo kufanya kazi kilionesha ubongo umesimama kufanya kazi na vipimo vingine vilionesha hakuna damu iliyokuwa ikienda kwenye ubongo.
Hii inaweza kuwa kama hadithi ya kutunga lakini tuunganishe dot katika haya. Je, umewahi kuwa karibu na mtu ambaye anataka kukata roho huku akisema kuna watu wanataka kumchukuwa? Mimi binafsi niliwahi kuwa karibu wakati mjomba wangu anafariki alikuwa akiniambia nimshike mkono nimvute kuna watu wanataka kumchukua.
Vipi kuhusu watu wa meditation hasa astral body projection, vinahusiana vipi na hii hali iliyosimuliwa na Bi.Pam Reynoild?
Kuna mengi ya kujifunza katika dunia hii.