Utafiti: Nusu ya wanaume nchini wagumba

Speaker

JF-Expert Member
Aug 12, 2010
6,324
2,238
UTAFTI mpya umebaini kuwa nusu ya wanaume nchini ni wagumba ukipingana madai ya wengi kuwa tatizo hilo linawaathiri zaidi wanawake.
Kwa mujibu wa utafiti huo, uliofanywa na Chuo Kikuu cha Tiba Muhimbili kati ya mwaka 2009 na Septemba 2010 unaonyesha, asilimia 47.05 ya wanaume wanaokwenda kupima afya zao za uzazi, hawana uwezo wa kutungisha mimba.
Malengo ya utafiti huo uliosimamiwa na Dk Henry Mwakyoma, yalikuwa ni kubaini ni kwa kiasi gani wanaume huweza kuathiriwa katika via vyao vya uzazi na hatimaye kushindwa kutungisha mimba.

Utafiti huo ulionyesha kati ya wanaume 221 waliopimwa, asilimia 30.03 walikuwa na mbegu dhaifu na asilimia 17.02 walikuwa hawana kabisa mbegu zenye uwezo wa kutungisha mimba, zaidi ya maji tu.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi, Dk Mwakyoma alisema, ugumba kwa wanaume limekuwa tatizo sugu katika miaka ya hivi karibuni.

"Nasisitiza kuwa, pengine mwanaume aliwahi kupata watoto hapo awali, lakini sasa hivi hapati, bado atakuwa mgumba,"
alisema Dk Mwakyoma.Alisema hapo awali ilikuwa vigumu kupata idadi kamili ya wanaume wenye ugumba kwa sababu walikuwa hawajitokezi kupima.
"Angalau sasa hivi wanakuja na tunawapima, ingawa ni kazi ngumu kuwapa majibu yao,"
alisema Mwakyoma.

Sababu za ugumba

Mwakyoma alitaja sababu za ugumba kwa wanaume kuwa ni uambukizo katika tezi inayozalisha manii.
Alitaja sababu nyingine kuwa ni kemikali zinazoingia katika miili yetu, mionzi na wakati mwingine ajali inapoathiri tezi hiyo.

Dk Mwakyoma aliongeza kuwa, wanaoathirika zaidi ni wanaofanya kazi migodini, jeshini au wanaozungukwa na kemikali kwa muda mrefu
."Sababu nyingine ni joto kuzidi katika sehemu za siri za mwanaume, kubeba laptop, unene kupita kiasi na mazingira,"
alisema.

Dk Mwakyoma akifafanua jinsi kitengo chake kinavyopima manii ili kujua kama zina matatizo au zipo salama, alisema, [quote rangi ya mbegu pamoja na umbile huangaliwa ili kutambua ubora wake. Hata kwa kuziangalia tu, mbegu zenye rangi aidha kijivu au nyeupe si salama.[/quote]

Kwa upande wake, Dk Innocent Mosha, ambaye ni daktari wa uchunguzi wa magonjwa katika Hospitali ya Muhimbili alisema, wamefanikiwa kupata takwimu hizo kutokana na wanandoa wengi kufika hospitalini hapo kwa ajili ya kujua sababu ya kutokuwa na watoto katika ndoa yao.
Mara nyingi matokeo huonyesha tatizo liko kwa mwanaume. Lakini kuna tabu ya kuwaeleza ukweli, wengi hawataki kukubali,
alisema Dk Mosha.

Aliongeza,
Kesi kama hizo huleta migogoro ya kifamilia, kwani huenda mwanamke huyo amekwishamzalia mumewe watoto ambao kimantiki si wa kwake,
alisema Dk Mosha.

Dk Mosha alisema, kuna ugumba wa aina mbili; wa kuzawa nao na ugumba unaopatikana ukubwani.
"Wapo wanaozaliwa na ugumba, yaani mbegu zao aidha ni dhaifu au hawana kabisa mbegu tangu kuzaliwa kwao," alisema Dk Mosha.

Shirika la Afya duniani (WHO) linathibitisha kuwa, ujazo wa manii anaopaswa kuwa nao mwanaume ili aweze kutungisha mimba ni milligram moja na nusu hadi nne na nusu na kuongeza, "Ujazo wa manii ukipungua au ukizidi basi mbegu hizo zina matatizo" alisema Dk Mwakyoma.

Naye Dk Joshua Noreh wa kituo cha upandikizaji cha jijini Nairobi (IVF centre) alisema, tatizo la ugumba alianza kuliona tangu mwaka 2006 baada ya kupokea wanandoa wengi kutoka Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania waliofika kutafuta huduma ya upandikizaji wa mbegu ili kupata watoto.

Utafiti uliofanywa na WHO mwaka 2009 duniani, ulibainisha kuwa, mwanaume mmoja kati ya saba wanaofika kupima afya ya uzazi hugundulika na matatizo ya ugumba.


Haya:
Wandugu tufanye mazoeziiiiiiiiiiiiii.
Achaneni na chipssssssssss.
Acheni kupende penda minyama na kitimotoooooo.....
Acheni biaaaaaa.
Ooooh,mie sivai boxer hahaha,nashangaa wengine mnavaa hadi chupi joto hilo jamani
ndo maana hayo madude yana ning'inia hayataki jotooooooo.
 
Mhhhh!!!! ngoja nisikie wanaume mna coment vipi hapa, maana mwanamke asipozaa wao ni wa kwanza kumrushia mwanamke lawama oooh huzai, ooooh nazeeka sina mrithi, kumbe na wenyewe ni wagumba?????????? Natamani wanaume wooote wwsome gazeti hili au hapa jf
 
MMh hali ni mbaya sana.............kuna haja ya kutoa elimu pana sana kwenye makundi yaliyopo hatarini................lakini naona kicha cha habari kinapigiwa upatu sana...........NUSU ni statistics kubwa sana na wakati huo huo tukumbuke kuwa nusu ya watu Tanzania ni watu wa jamii ya kawaida wanaondesha shughuli za kawaida...........mbali kdg na athari zilizotajwa za kimazingira ama kishughuli.
 
huyo dr................... njaa tu inamsumbua..................... uongo......................... uongo.................. uongo......................
 
Haiwezi kuwa kweli na huu utafiti ni feki kabisa tena wasingetakiwa hata kuutoa. Kama tatizo lingekuwa ni kubwa kiasi hicho lazima tungeona wakina mama wanaohitaji watoto wakibaka...watuambie walipataje hizo mbegu wakapima kama siyo walichukua za wanaume waliokuwa wagonjwa....nakataa kabisa huu utafiti ni aibu kwa walioutoa!
 
Ingekuwa tatizo ni kubwa kiasi hiki tungeona hata mitaani tunakoishi. Karibu kila nyumba au familia ina mtoto. What a fake research!
 
Utafiti huu haujazingatia taaluma za kitafiti.

1) huwezi kugeneralize kuwa 50% wanatatizo kwa kuwa ina makosa mengi ya kitaalamu ikiwepo biasness, wanaume wowote wanaoenda kucheki afya zao za uzazi ni wengi wao obvious wana tatizo hilo, hivyo hawawakilishi wanaume wote wa tanzania.

2) kama kweli sababu zilizotolewa kama visababishi vya tatizo joto, laptop use n.k basi haifai kuchukua sample toka dar kwa kuwa joto ndio nyumbani kwake na ni miongoni ya mikoa ambayo kuna matumizi makubwa ya laptop n.k

kama kweli alikua na nia ya kufanya utafiti wa aina hii basi angechagua watu randomly toka jamii mbali mbali zenye exposure tofauti katika mikoa mbali mbali na sio wale tuu walioenda hospitali kucheki tatizo hapo ingekuwa imetulia.

Haya ni matatizo ya madaktari wetu wasio na ujuzi wa utafiti.

poor research design will lead to poor results which will always lead to contradiction.


NB: Gazeti lililotoa taarifa hii ni mwananchi, na bahati mbaya huenda waandishi wetu wa mwananchi wameshazoea kutoa habari za Chadema, CCm ,JK,Slaa N.k. pia kuna uwezekano hawa waandishi wakawa hawana uwezo wa kuanda matokea ya kitafiti za afya.
 
UTAFTI mpya umebaini kuwa nusu ya wanaume nchini ni wagumba ukipingana madai ya wengi kuwa tatizo hilo linawaathiri zaidi wanawake.
Kwa mujibu wa utafiti huo, uliofanywa na Chuo Kikuu cha Tiba Muhimbili kati ya mwaka 2009 na Septemba 2010 unaonyesha, asilimia 47.05 ya wanaume wanaokwenda kupima afya zao za uzazi, hawana uwezo wa kutungisha mimba.
Malengo ya utafiti huo uliosimamiwa na Dk Henry Mwakyoma, yalikuwa ni kubaini ni kwa kiasi gani wanaume huweza kuathiriwa katika via vyao vya uzazi na hatimaye kushindwa kutungisha mimba.

Utafiti huo ulionyesha kati ya wanaume 221 waliopimwa, asilimia 30.03 walikuwa na mbegu dhaifu na asilimia 17.02 walikuwa hawana kabisa mbegu zenye uwezo wa kutungisha mimba, zaidi ya maji tu.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi, Dk Mwakyoma alisema, ugumba kwa wanaume limekuwa tatizo sugu katika miaka ya hivi karibuni.


alisema Dk Mwakyoma.Alisema hapo awali ilikuwa vigumu kupata idadi kamili ya wanaume wenye ugumba kwa sababu walikuwa hawajitokezi kupima.
alisema Mwakyoma.

Sababu za ugumba

Mwakyoma alitaja sababu za ugumba kwa wanaume kuwa ni uambukizo katika tezi inayozalisha manii.
Alitaja sababu nyingine kuwa ni kemikali zinazoingia katika miili yetu, mionzi na wakati mwingine ajali inapoathiri tezi hiyo.

Dk Mwakyoma aliongeza kuwa, wanaoathirika zaidi ni wanaofanya kazi migodini, jeshini au wanaozungukwa na kemikali kwa muda mrefu alisema.

Dk Mwakyoma akifafanua jinsi kitengo chake kinavyopima manii ili kujua kama zina matatizo au zipo salama, alisema, [quote rangi ya mbegu pamoja na umbile huangaliwa ili kutambua ubora wake. Hata kwa kuziangalia tu, mbegu zenye rangi aidha kijivu au nyeupe si salama.

Kwa upande wake, Dk Innocent Mosha, ambaye ni daktari wa uchunguzi wa magonjwa katika Hospitali ya Muhimbili alisema, wamefanikiwa kupata takwimu hizo kutokana na wanandoa wengi kufika hospitalini hapo kwa ajili ya kujua sababu ya kutokuwa na watoto katika ndoa yao.
Mara nyingi matokeo huonyesha tatizo liko kwa mwanaume. Lakini kuna tabu ya kuwaeleza ukweli, wengi hawataki kukubali,
alisema Dk Mosha.

Aliongeza,
Kesi kama hizo huleta migogoro ya kifamilia, kwani huenda mwanamke huyo amekwishamzalia mumewe watoto ambao kimantiki si wa kwake,
alisema Dk Mosha.

Dk Mosha alisema, kuna ugumba wa aina mbili; wa kuzawa nao na ugumba unaopatikana ukubwani.
"Wapo wanaozaliwa na ugumba, yaani mbegu zao aidha ni dhaifu au hawana kabisa mbegu tangu kuzaliwa kwao," alisema Dk Mosha.

Shirika la Afya duniani (WHO) linathibitisha kuwa, ujazo wa manii anaopaswa kuwa nao mwanaume ili aweze kutungisha mimba ni milligram moja na nusu hadi nne na nusu na kuongeza, "Ujazo wa manii ukipungua au ukizidi basi mbegu hizo zina matatizo" alisema Dk Mwakyoma.

Naye Dk Joshua Noreh wa kituo cha upandikizaji cha jijini Nairobi (IVF centre) alisema, tatizo la ugumba alianza kuliona tangu mwaka 2006 baada ya kupokea wanandoa wengi kutoka Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania waliofika kutafuta huduma ya upandikizaji wa mbegu ili kupata watoto.

Utafiti uliofanywa na WHO mwaka 2009 duniani, ulibainisha kuwa, mwanaume mmoja kati ya saba wanaofika kupima afya ya uzazi hugundulika na matatizo ya ugumba.


Haya:
Wandugu tufanye mazoeziiiiiiiiiiiiii.
Achaneni na chipssssssssss.
Acheni kupende penda minyama na kitimotoooooo.....
Acheni biaaaaaa.
Ooooh,mie sivai boxer hahaha,nashangaa wengine mnavaa hadi chupi joto hilo jamani
ndo maana hayo madude yana ning'inia hayataki jotooooooo.
 
Kuna upotoshaji mkubwa sana katika huo utafiti.. majibu yanahusisha wale ambao walienda hospitali kwa matatizo ya infertility which is obvious kupata hiyo asilimia kwani tunategemea wagonjwa ndio wanatafuta matibabu..
 
MMh hali ni mbaya sana.............kuna haja ya kutoa elimu pana sana kwenye makundi yaliyopo hatarini................lakini naona kicha cha habari kinapigiwa upatu sana...........NUSU ni statistics kubwa sana na wakati huo huo tukumbuke kuwa nusu ya watu Tanzania ni watu wa jamii ya kawaida wanaondesha shughuli za kawaida...........mbali kdg na athari zilizotajwa za kimazingira ama kishughuli.

Kweli kabisa.
kama ni nusu basi wangekua wame mpima kila mwanaume.
Mimi hawajanipima bado so utafiti wao sio sahihi.
 
Utafiti huu haujazingatia taaluma za kitafiti.

1) huwezi kugeneralize kuwa 50% wanatatizo kwa kuwa ina makosa mengi ya kitaalamu ikiwepo biasness, wanaume wowote wanaoenda kucheki afya zao za uzazi ni wengi wao obvious wana tatizo hilo, hivyo hawawakilishi wanaume wote wa tanzania.

2) kama kweli sababu zilizotolewa kama visababishi vya tatizo joto, laptop use n.k basi haifai kuchukua sample toka dar kwa kuwa joto ndio nyumbani kwake na ni miongoni ya mikoa ambayo kuna matumizi makubwa ya laptop n.k

kama kweli alikua na nia ya kufanya utafiti wa aina hii basi angechagua watu randomly toka jamii mbali mbali zenye exposure tofauti katika mikoa mbali mbali na sio wale tuu walioenda hospitali kucheki tatizo hapo ingekuwa imetulia.

Haya ni matatizo ya madaktari wetu wasio na ujuzi wa utafiti.

poor research design will lead to poor results which will always lead to contradiction.


NB: Gazeti lililotoa taarifa hii ni mwananchi, na bahati mbaya huenda waandishi wetu wa mwananchi wameshazoea kutoa habari za Chadema, CCm ,JK,Slaa N.k. pia kuna uwezekano hawa waandishi wakawa hawana uwezo wa kuanda matokea ya kitafiti za afya.

Well said mkuu.
Nahisi haya ndo yale yale ya Redet kulipua mambo.
Tanzania utafiti una fanyiwa ofisini na sio kutoka kuangalia ulimwengu halisi
uko vipi....No wonder wana siasa wakiugua hawatibiwi tanzania na hawana hata mda wa
kuwasikiliza madaktari.
 
Kuna haja ya kufanya utafiti wa kina na kuomba ushauri au kuisoma taarifa yenyewe vyema kabla ya kuitoa kwenye vyombo vya habari.

1. Si kweli kwamba nusu ya wanaume ni wagumba. Nasema hivi kwa sababu watu waliokwenda kupima tayari walikua na tatizo, hivyo ukiwapima lazima utakuta kuna tatizo. Huwezi kwenda kupima manii kwa shida ya kuumwa jicho, bali unaenda pale baada ya kuona kuna shida kwenye issue za uzazi, hivyo basi uwezekano wa kukutwa na tatizo ni mkubwa kwa wale waliokwenda hapo. Aendeaye sipitali lazima ana shida, na ukiona zinduma ambari iko nyuma.

2. Ili kuwa na matokeo sahihi, utafiti huu ungepaswa kupima watu toka kwenye jamii (random sampling) na siyo kwenda kupima watu wenye shida tayari. Huwezi kwenda kupima kama baharini kuna mchanga ama la? bali ukitaka kujua kama msitu una mchanga ama la hapo unaweza kupima na unaweza kujua kama kuna mchanga au hapana.

3. Hiyo asilimia 50% kati ya watu 221 walopimwa haiwiani na idadi yote ya wanaume waliopo hapa nchini, tena walau wale ambao tayari wameshajaribu kutafuta mtoto.
 
[SUB]Safari hii wanaume tumeshikwa pabaya[/SUB] - mbona hii ni hatari sasa
 
Nadhani kuna makosa katika kuelewa tafsiri halisi ya matokeo ya utafiti huo. Tafiti haijasema kwamba nusu ya wanaume wote tz ni wagumba, imesema nusu ya wale wanaofika hospitali kupata ufumbuzi ya maswala yao ya uzazi hukutwa ni wagumba. Nadhani si swala la kushangaza sana, sababu hatutegemei wanaume ambao hawana matatizo ya uzazi kwenda hospitali kusaka msaada. Ingekuwa hii study ni randomized clinical study hapo kweli tungesema kwamba kiasi fulani matokeo yake yanawakilisha kile ambacho kipo katika jamii. None the less, ujumbe ni kwamba ugumba kwa wanaume upo, na ni significant kama ilivyo kwa wanawake so tuache kunyanyapaa wakinamama.
 
Malengo ya utafiti huo uliosimamiwa na Dk Henry Mwakyoma, yalikuwa ni kubaini ni kwa kiasi gani wanaume huweza kuathiriwa katika via vyao vya uzazi na hatimaye kushindwa kutungisha mimba.

MWANANCHI liache propaganda zisizo na tija ,magazeti mmeshauza ila huu upotoshaji ipo siku utawagharimu,
Hiyo 50% ya watanzania ni analysis yenu na wala si ya huyo Dr ,
Kama alikuwa anataka kujua ni % ngapi ya watz imeathiriwa , si angechukua random samples za watz ?
 
study hii ina mapungufu mengi sana. Pamoja na mapungufu yaliyotajwa, pia hatujaonyeshwa muda uliotumika na age groups. na kama walienda wanandoa comperative study ingeonyeshwa hapa. Mara nyingi study za namna hii ni kwa ajili ya kufurahisha donors wa nje ili waendelee kuomba misaaada
 
Back
Top Bottom