Utafiti Marekani umeonesha kwamba watu waliozaliwa kuanzia mwaka 1997 ni wabishi, wajuaji na hawana heshima

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,321
Screenshot 2023-04-26 165803.png


Marekani utafiti umeonyesha kwamba ni vigumu sana kufanya kazi na kizazi Z ama generation Z ambao wamezaliwa kuanzia mwaka 1997.

Meneja na wakurugenzi wa wakuu wa utumishi walioulizwa kwenye utafiti wamesema ni ngumu sana kufanya kazi na kizazi Z kwani ni wabishi, wajuaji, hawana nidhamu wala heshima.

Kizazi Z hujiamini kupita kiasi, hujiona wanajua kila kitu, hutaka hata kuwafundisha wakuu wao wa kazi.

Huko China serikali inalalamika kwamba wasomi wa sasa hasa kizazi Z hawataki kazi ngumu, hawataki kazi za shamba wanataka kazi laini za online, za kuvaa suti na kula kuku kwa mrija.

Je, unakubaliana na utafiti huo?

Fox News
 
... dunia inaenda kasi sana. Ndio aina ya kizazi cha hakuna Mungu, dini ni utapeli, kataa ndoa, etc. Hayo mambo usingeyaongea hivyo miaka 25 iliyopita ukaeleweka.

Au kukutana na akina dada wamevaa skin tight tena tight kali zikiwachora exactly walivyo eti wako bize maofisini wakihudumia wateja!
 
Tatizo wazee hawapendi kukosolewa hata kama wemekosea, na hii hulka ni ipo dunia nzima
Sasa hawa vijana wa leo wako well informed na dunia ya leo, sio sisi tulikuwa tunapigiwa hadithi za maisha na wazee wetu
 
Back
Top Bottom