Utabiri wa Shehe Yahya umetimia?!

Hivi mmesahau kwa huyu ni yule shehe aliyewahi kutabiri kwamba kwenye uchaguzi wa 2005 Tanzania ingepata rais wa kike????????????????????????. Yeye yupo kazini jamani

Huko mbona mbali sana jamani, mimi nilishawahi kupiga simu kati ya moja ya vipindi vyake redioni na kumuuliza juu ya mahesabu yake inakuwaje kila siku anatabiri kwamba timu fulani ya mpira itashinda au itashindwa je inakuwaje pale timu zinapotoka draw/ suluhu bila ya kufungana mbona hajawahi sema hata siku moja mahesabu yake yanakwqenda vipi?

Kilichoendelea sijui ila swali langu sikujibiwa wala kuongelewa kabisa.
 
Huko mbona mbali sana jamani, mimi nilishawahi kupiga simu kati ya moja ya vipindi vyake redioni na kumuuliza juu ya mahesabu yake inakuwaje kila siku anatabiri kwamba timu fulani ya mpira itashinda au itashindwa je inakuwaje pale timu zinapotoka draw/ suluhu bila ya kufungana mbona hajawahi sema hata siku moja mahesabu yake yanakwqenda vipi?

Kilichoendelea sijui ila swali langu sikujibiwa wala kuongelewa kabisa.

Komamanga,
Labda endelea kuwa mvumilivu bado anatafuta jibu la sivyo mtafute tena siku ya kipindi kupitia Channel Ten.
 
Alitabiri kifo cha kiongozi na mtu maaraufu nchini kutokea mwezi Juni

Tayari wafuatao wametutoka:

  1. Kaimu Mufti Mkuu, Sheikh Suleiman Gorogosi
  2. Prof Haroub Othman
Kabla yao alitangulia Mwana mipasho Bi. Nasma Khamis Kidogo. Kumbe hii sayansi ya Nyota inafanya kazi!
Shekhe Yahaya hana kitu,anabahatisha tu,mbona yeye aliponea chupuchupu,kwanza ashauriwe aache kuchuria watu,vifo vyote hupangwa na Mungu hata kama binadamu ndio walipanga hakiwi bila Mungu kuamua.Aache kudanganya watu kwani yeye ni nani eti anajua Mungu kapanga nini.Kama anatoa miti shamba aendelee ila kudanganya kwa utabiri aache kwani anawadanganya watu kisaikolojia.
 
Watu hufariki siku miezi yote. Waliomaarufu na vinginevyo. Utabiri ni ujanja na ubabaishaji tu. aina nyingine ya ufisadi na kukaribisha majini. Washindwe!
 
I dont trust this man either...! Wizi mtupu.! Kuna siku alisema watu wa nyoto yangu (taurus) ili mapenzi yadumu inatakiwa kuimba wakati wakujamiana..! How on earth one can sing during sex..?
 
Alitabiri kifo cha kiongozi na mtu maaraufu nchini kutokea mwezi Juni

Tayari wafuatao wametutoka:

  1. Kaimu Mufti Mkuu, Sheikh Suleiman Gorogosi
  2. Prof Haroub Othman
Kabla yao alitangulia Mwana mipasho Bi. Nasma Khamis Kidogo. Kumbe hii sayansi ya Nyota inafanya kazi!


Hana lolote. ajitabirie yeye atatuka lini ndio tutajua ni mtabiri
 
...Kuna siku alisema watu wa nyoto yangu (taurus) ili mapenzi yadumu inatakiwa kuimba wakati wakujamiana..! How on earth one can sing during sex..?
Haa haa haaaaa !! Labda alimaanisha kulia, ila akatumia sanaa ya lugha. BTW unatakiwa kujaribu kuimba siku moja ili utujulishe kama haiwezekani au la !! :D
 
Haa haa haaaaa !! Labda alimaanisha kulia, ila akatumia sanaa ya lugha. BTW unatakiwa kujaribu kuimba siku moja ili utujulishe kama haiwezekani au la !! :D


hahahhahh kwikwikwik kwidikwidi hahahahahahahahah hehehehhehhehehhehehhehhehehehh nicheke mie natamani niwepo wakati wa kuimba
 
Mkuu, kweli unataka specifics?

All in all, upande wangu mimi hawa watabiri wangekaa na tabiri zao tu, watuletee za hali ya hewa peke yake!

What I meant to say mkuu ni kwamba utabiri wake uko in general mno so hauwezi kusema anafanya utabiri. Angekua anasema specificaly kitatokea hiki labda ungesema ana nguvu fulani ziwe za Kimungu au za kigiza. Hata mimi sasa hivi naweza kusema mwezi fulani mtu fulani maarufu atakufa and chances are it wil happen maana watu maarufu wako wengi duniani na kila mwezi kuna mtu maarufu anayekufa.
 
Wengi walishaondoka na wengi wataondoka so huu siyo utabiri wa kuaminika.Angalia threads zinazoulizia wana JF mbalimbali wako wapi.
Jaribu kutabiri kitu kingine ndugu.

Mh dada WoS I think mchangiaji was being sarcastic in regards to the whole issue na siyo kwamba he/she was trying to make an actual prediction.
 
I dont trust this man either...! Wizi mtupu.! Kuna siku alisema watu wa nyoto yangu (taurus) ili mapenzi yadumu inatakiwa kuimba wakati wakujamiana..! How on earth one can sing during sex..?
Uliimba? Ungeimba um-prove wrong! Wewe mwenyewe hukutimiza masharti halafu unalalamika ni "mwongo". Mwongo gani kama hata hukujaribu.
 
Hakuna kitu cha ajabu hapo.Cha ajabu kitakuwa kama kuna mwaka ambao hakuna kifo kabisa nchini, hata cha mtoto mchanga!
 
What I meant to say mkuu ni kwamba utabiri wake uko in general mno so hauwezi kusema anafanya utabiri. Angekua anasema specificaly kitatokea hiki labda ungesema ana nguvu fulani ziwe za Kimungu au za kigiza. Hata mimi sasa hivi naweza kusema mwezi fulani mtu fulani maarufu atakufa and chances are it wil happen maana watu maarufu wako wengi duniani na kila mwezi kuna mtu maarufu anayekufa.
Unaposema awe specific una maana gani? Aseme majina ya watu watakaopatwa na majanga, siku, saa, tarehe na mwaka? Mmh, kama ni hivyo sasa ni shughuli! Mi nadhani alikuwa specific kwa maana kwamba alitaja mwezi (Juni), akataja mahali (hapa nchini), akaspecify kwamba si mtu yeyote bali mtu maarufu. Yaani kwenu haya maelezo hayatoshi? Kwani kilichobakia hapo ni jina tu. Mengine yote yameshatabiriwa.

Tukubali kwamba elimu hiyo ya mzee Yahya wengi wetu hatuijui. Na si makosa yetu. Kutokuijua haina maana kwamba haipo. Kwani mangapi hatuyajui hata kwa elimu ya kawaida ya kisayansi? La maana tungedadisi huyu mzee anawezaje kujua future events? What is the source of his knowledge?
 
haya mambo ya utabiri wala sio kitu kigeni katika hii dunia, inategemea na imani yako tu na kwa jinsi gani unavyoyachukulia haya mambo,
haya mambo yanakuwa na maelezo au majina tofauti kulingana na imani au upeo wa wahusika, ningependa nizungumzie mifano ambayo tunaipata kwenye biblia
1. joseph (yusufu), baada ya kutiwa gerezani, alifanikiwa kutoka na kuwa mtu mkubwa sana baada ya kutafsiri ndoto kwa kumweleza pharaoh kuwa kutakuwa na miaka ya neema na miaka ya balaa, sasa watu wa dini watatuambiwa ni mipango ya Mungu, vipi shehe Yahaya asiwe mpango wa Mungu, kutafsiri ndoto kwamba mambo fulani yatatokea huo sio utabiri
2. wakati wa Yesu kuzaliwa, wataalamu wa nyota (kama shehe Yahaya) kutoka far east (labda India au China)Mamajusi, katika kutazama mambo yao ya nyota wakaona kuna mtoto kazaliwa Yelusalem ambaye atakuwa mtu mkubwa sana, hivyo wakaamua kuja Yelusalemu kuja kutoa zawadi zao wakiongozwa na hayo mambo yao ya nyota, na moja kwa moja Herode akajua ujio wa watu hao maarufu na Herodi akawaambia wakimwona waje wamweleze, lakini Biblia inatuambia Malaika wa Mungu, akawatokea na kuwaambia wasirudi kwa Herode, swali ni kuwa hawa jamaa ni watabiri kama shehe Yahaya tu, na waliuona mipango ya Mungu kwa kutabiri ujio wa mtu asiye wa kawaida na still Mungu akawa upande wao,
kwa hiyo bac kwa mtazamo wangu, shehe Yahaya anaweza kuwa mtabiri wa kweli lakini kwenye kiwango chake, yaani anaweza kutabiri kutakuwa na vifo mwezi wa sita na hapo ndio ukawa ni mwisho wake yaani hawezi kusema ni nani na tarehe hipi lakini wapo wengine wenye uwezo huo, Kwa wenye imani

tafakuli zangu tu
 
Unaposema awe specific una maana gani? Aseme majina ya watu watakaopatwa na majanga, siku, saa, tarehe na mwaka? Mmh, kama ni hivyo sasa ni shughuli! Mi nadhani alikuwa specific kwa maana kwamba alitaja mwezi (Juni), akataja mahali (hapa nchini), akaspecify kwamba si mtu yeyote bali mtu maarufu. Yaani kwenu haya maelezo hayatoshi? Kwani kilichobakia hapo ni jina tu. Mengine yote yameshatabiriwa.

Tukubali kwamba elimu hiyo ya mzee Yahya wengi wetu hatuijui. Na si makosa yetu. Kutokuijua haina maana kwamba haipo. Kwani mangapi hatuyajui hata kwa elimu ya kawaida ya kisayansi? La maana tungedadisi huyu mzee anawezaje kujua future events? What is the source of his knowledge?

Mkuu maana ya utabiri ni kutabiri haswa nini kitatokea na kitatokeaje. Kasema mtu maarufu atakufa June, watu wangapi maarufu wamesha kufa hii June? Sasa ni yupo kati ya hao ndiyo alikuwa ame tabiri watakufaa? Siwezi kuamini kitu kwa kufuata tu mkumbo lazima niridhike kuwa kitu ni kweli. Sikatazi wengine kuamini ila mimi siwezi amini hivi hivi tu. Kama wewe ni mmoja wanaoamini kwamba kweli ana uwezo wa kutabiri that's all fine and well.
 
Sri Lanka kuna mtabirio kasema September Serikali itaanguka. Hivi sasa ananyea debe ili atoe reference yake. BBC NEWS | South Asia | Sri Lanka astrologer is arrested and Sri Lankan Astrologer Jailed SASA nyinyi mwamtaka nini mzee wa watui!!! ETI awe "specific"

Kwa mzee wetu kuna siku alikuwa anarejea tabiri zake kwenye chanel TEN. Basi jamaa akapiga simu akimuuliza atabiri yeye mwenyewe ataitika wito wa Mwenyezi MUNGU lini. Lakini akamjibu kuwa aende ofisini magomeni ndipo atakapomweleza. Kazi kweli kweli. Sijui kama jamaa alienda ama la.
 
Mkuu maana ya utabiri ni kutabiri haswa nini kitatokea na kitatokeaje. Kasema mtu maarufu atakufa June, watu wangapi maarufu wamesha kufa hii June? Sasa ni yupo kati ya hao ndiyo alikuwa ame tabiri watakufaa? Siwezi kuamini kitu kwa kufuata tu mkumbo lazima niridhike kuwa kitu ni kweli. Sikatazi wengine kuamini ila mimi siwezi amini hivi hivi tu. Kama wewe ni mmoja wanaoamini kwamba kweli ana uwezo wa kutabiri that's all fine and well.
Hebu sikia mkuu! Kitu chenyewe kinaitwa "Utabiri". Kitu kilichotabiriwa maana yake chaweza kutokea au kinaweza kisitokee. Utabiri is not a certain foreseen event. Utabiri unaacha mwanya wa jambo kutotokea pia. Ndo maana unaitwa utabiri. Shida ya wengi wanataka utabiri uwe na jibu hakika, kamili, lisilo na mashaka. Huu si utabiri tena.

Sikulazimishi uamini hayo yaliyotabiriwa. Unaweza kuyabeza pia. Lakini unapoyabeza uwe na grounds badala ya kusema tu "hakuna kitu hapo". Huwezi kuyabeza tu kwa vile hakutaja jina la mtu, na hakusema tarehe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom