Utabiri wa hali ya hewa Tanzania ni feki?

dudus

JF-Expert Member
Feb 28, 2011
22,125
49,384
Kwa muda sasa kumekuwa na madai kwamba utabiri wa hali ya hewa nchi hii ni feki. Kufuatia madai hayo, niliamua mwenyewe msimu huu kufuatilia kwa karibu ili niweze kuthibitisha.

Katikati ya Septemba 2018 haoooo wakaibuka. Wakatabiri kwamba mvua za vuli zingeanza mwishoni mwa mwezi huo au mapema Oktoba na zingenyesha juu ya wastani kwa maeneo mengi nchini. Leo ni Oktoba 16 na wakulima wengi tulishaandaa mashamba na kupanda zaidi ya wiki mbili zilizopita tukisubiria "utabiri" kutimia lakini HOLAAA! Imekula kwetu; hasara juu ya hasara.

Utabiri nchi hii ni kizungumkuti. Inawezekana zikanyesha pengine hata juu ya wastani kama walivyotabiri na kama ambavyo imeanza huko Uganda lakini timing yao imekuwa ya hovyo kabisa. Nawashauri wakulima watumie njia za asili za utabiri wa majira badala ya kutegemea mamlaka hii labda kwa mawio na machweo tu.

=== UPDATES - 01.11.2018 ===

Baada ya mwanzoni mwa Septemba 2018 kutabiri kwamba mwishoni mwa mwezi huo zingenyesha mvua za "hatari" ambazo zingeleta maafa sehemu kubwa ya nchi; utabiri ambao haukutimia, Hali ya Hewa waliibuka na tabiri kadhaa kurekebisha ule wa awali na kuwashauri wakulima kuandaa mashamba ili kutumia "vizuri" mvua tarajiwa. Hata hivyo, hakuna utabiri uliotimia.

Pengine kwa kugundua tabiri zao za awali hazikutimia, Oktoba 18, DG mwenyewe aliitangazia dunia kwamba Oktoba 20 ndio ingekuwa siku yenyewe na "akatabiri" sehemu kubwa ya nchi zingemwagika mvua kubwa sana. Wakulima walishauriwa kuanza kupanda mbegu kwani muda ulikuwa "umekwisha". Leo ni Novemba 01, 2018 hizo mvua hazioneshi hata dalili kwamba zitanyesha badala yake ni jua kali kila kona ya nchi. Naendelea kuwashauri wakulima kutumia njia za asili za utabiri wa hali ya hewa. Mamlaka ya Hali ya Hewa ni muhimu wakajitafakari kwani tabiri zao zinakosa uhakika japo kwa 10%.
 
Bado unawaamini hao ???
Kuna mwaka waliwahi kutabiri ukame. Ikanyesha mvua mpaka ikapewa jina Elnino,. Na Kuna mwaka walitabiri mvua kidogo Sana ikanyesha mvua ikaondoka na daraja la matumbi pale buguruni.
Kifupi fanya mambo yako hao jamaa achana nao.
Wanaweza kukutembeza mjini na mwamvuli ukaonekana mchawi. Kutwa umevaa koti na viatu vya mvua ukidhani itanyesha kumbe jua Kali.
Kamera zao sijui huwaga hazioni au sijui huwa zinamulika wapi. Hata sielewi.
 
Aisee nimeshangaa maeneo mengi isipokuwa mikoa ya kusini wameshaweka mbegu chini tangu mwanzoni mwa mwezi october ila mvua hakuna mpaka sasa
 
Aisee nimeshangaa maeneo mengi isipokuwa mikoa ya kusini wameshaweka mbegu chini tangu mwanzoni mwa mwezi october ila mvua hakuna mpaka sasa
Hawa jamaa wanatia watu hasara sana Mkuu.
 
Bado unawaamini hao ???
Kuna mwaka waliwahi kutabiri ukame. Ikanyesha mvua mpaka ikapewa jina Elnino,. Na Kuna mwaka walitabiri mvua kidogo Sana ikanyesha mvua ikaondoka na daraja la matumbi pale buguruni.
Kifupi fanya mambo yako hao jamaa achana nao.
Wanaweza kukutembeza mjini na mwamvuli ukaonekana mchawi. Kutwa umevaa koti na viatu vya mvua ukidhani itanyesha kumbe jua Kali.
Kamera zao sijui huwaga hazioni au sijui huwa zinamulika wapi. Hata sielewi.
Miongoni mwa taasisi incompetent nchini kwa sasa ni hii inayoitwa mamlaka ya hali ya hewa.
 
Utabiri wa Hali ya Hewa ni estimation tuu. Sio lazma uwe wa kweli nahakuna mtu anaweza kuutabiri kwa 100% accuracy.
Kuna haja gani ya kuwa na chombo cha aina hiyo? Kama sio wa kweli hata mtoto mdogo anaweza kutabiri. Umefika wakati sasa to get rid of this institution ambayo inakula kodi za bure huku ikitia wakulima hasara. Tani kwa tani za mbegu zimemwagwa ardhini kutokana na utabiri wa hawa jamaa. They have to show up to apologize hasara waliyotia wakulima.
 
Pole kwa hasara mpendwa mkulima:(:( hawa watabiri wetu sio wa kuwaamini kila kitu wanachosema. Amini 2/10 ya hadithi zao mkuu vinginevyo utaendelea kuleta mirejesho ya hasara zako.
 
Utabiri wa Hali ya Hewa ni estimation tuu. Sio lazma uwe wa kweli nahakuna mtu anaweza kuutabiri kwa 100% accuracy.
Kama hujui maana ya hii mamlaka ndio utabaki kujiaminisha ki hivyo. Lakini, Utabiri wa hali ya hewa ni mamlaka ambayo ikikosea tu kidogo huleta hasara kubwa mno kwenye nchi nyingine.
Mfano;
Utabiri wa hali ya hewa ndiyo mamlaka ambayo huelekeza mahali ambapo kimbunga kitapitia hivyo msije mkakutwa na hicho kimbunga ghafla mkafa wote. Tena mnaelekezwa cha kufanya, saa kitapita na ukubwa wa uharibifu. Kwa hivyo, kama hawa wangelikuwa wanatabiri kwa kubashiri ka hawa wa kwetu nadhani kusingelibaki mtu hai.
Tatizo la hawa wenzetu wa Mamlaka ya hali ya hewa Tz ni "Ubashiri" mwingi. Wanaangalia trend ya mvua miaka 10 iliyopita wanaona leo itakuwa hivi. Ndipo wanatokezea na kutangaza bila hofu kuwa itakuwa hivi. Wanasahau kuwa kuna kitu kipya kinaitwa' Badiliko la tabia nchi."
Hali ya hewa imebadilika. Haina utaratibu tena hivyo wasibashiri bali waweke vyombo sahihi au waombe kutoka kwa wengine wawape utabiri wa kweli. Ukitaka kupata utabiri wa kweli, omba FAO watakutumia utabiri unaoutaka na hakuna kosa lolote. Nawasilisha
 
Back
Top Bottom