Usultani unaujuwa au unausikia tu? cheki huu to start with:
Su huyo tu, na Mbowe na Baba'mkwe wake.
Balozi Kagasheki ni mbunge wa Bukoba mjini. Abubakari Kagasheki ni mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi wa
Wilaya ya Bukoba Mjini, jumuiya iliyoko chini ya CCM. Abdul Kagasheki anagombea awe Mjumbe wa
Halmashauri Kuu ya Taifa kutokea Bukoba Mjini. Suedi Kagasheki anagombea awe mjumbe wa kuwakilisha
Wilaya kwenye Mkutano Mkuu wa CCM Taifa tokea Bukoba Mjini. Katika hotuba yake kwa wajumbe
waliomchagua Abubakari Kagasheki, amesema na ninamnukuu, " Nawashukuru familia yangu kwa
kuniwezesha Kwa hali na mali katika uchaguzi huu. Kwa namna ya pekee niwashukuru Abdul Kagasheki na
Hamisi Kagasheki kwa kuniwezesha kwa hali na mali kushinda uchaguzi huu. Ndugu wajumbe, Familia
yetu inayo historia kubwa katika CCM kiasi kwamba Marehemu Baba wa Taifa akidai Uhuru alilala kwa
Baba yangu, na ndio maana hivi karibuni niliitwa Ikulu kwa ajili ya kupokea nishani iliyotolewa na
rais kwa ajiri ya baba yangu. Hivyo Familia yetu inaijua CCM zaidi ya yeyote katika wilaya
hii.Hivyo mtu wa FAMILIA YETU AKIGOMBEA TUTA HAKIKISHA ANAPITA KWA NJIA YOYOTE ILE" mwisho wa
kunukuu. Wanachama, wadau, na wakereketwa wa CCM Wilayani Hapa wamebaki na bumbuwazi na kujiuliza
HIVI SIASA ZA CCM BUKOBA MJINI KUHODHIWA NA FAMILIA MOJA, ni kwa ajili ya MASLAHI YA CHAMA,
WANACHAMA NA TAIFA AU NI ZA KUJINUFAISHA BINAFSI? NA JE, KWA VITISHO HIVI CHAMA BUKOBA MJINI KINA
ELEKEA WAPI?
Mwenyekiti wa chama ni Freeman Mbowe. Taja hata ndugu yake mmoja tu ambaye ana cheo ndani ya chama. Acha uwongo!
"Lissu kaja na dada yake. Ukienda kwa Mwenyekiti wa Chama ana ndugu watatu, Slaa kuna mke wake, nani ana utawala wa kifalme? Ndesamburo amekuja na mtoto wake na mkwe wake, Samahani Mh. Ndesamburo"
Mwenyekiti wa chama ni Freeman Mbowe. Taja hata ndugu yake mmoja tu ambaye ana cheo ndani ya chama. Acha uwongo!
"Lissu kaja na dada yake. Ukienda kwa Mwenyekiti wa Chama ana ndugu watatu, Slaa kuna mke wake, nani ana utawala wa kifalme? Ndesamburo amekuja na mtoto wake na mkwe wake, Samahani Mh. Ndesamburo"
Usiruke viunzi. Umesema mwenyekiti ana ndugu zake watatu, nitajie angalau mmoja tu, na si kuleta hii ya kaskazini. Maliza hiyo kwanza halafu ndiyo tujadilie ya kaskazini.Wabunge wa viti maalum, wao si kifalme tu, tuseme ni kaskazini tu, nawashangaa watu wanaojiita CHADEMA, wenzako wako bungeni huulizi wamepatikanaje."
Ikiwa hata wewe wa Mara, Nyelele anasema ni "ndugu" yangu, wa Kaskazini na wa Kaskazini inakuwaje? "mapacha"?
Wabunge wa viti maalum, wao si kifalme tu, tuseme ni kaskazini tu, nawashangaa watu wanaojiita CHADEMA, wenzako wako bungeni huulizi wamepatikanaje."
Ikiwa hata wewe wa Mara, Nyelele anasema ni "ndugu" yangu, wa Kaskazini na wa Kaskazini inakuwaje? "mapacha"?
Mwita Maranya naomba kuuliza tatizo ni kubebwa ama kubebwa na mzazi? Hivi kaka katika jamii yetu hii hadi sasa hujaona kuwa kubebana kupo sana? System ndani ya serkali yetu katika Institutions zote zimeharibika to the extent kila mara kuna kubebana ili mradi you fit the bill even if you cannot cover the costs…
Kuna kitu hapa utakuwa ume miss katika hayo maelezo yangu. Sisemi kuwa njia aliyopita makamba ni sahihi hasa ukizingatia ana cheo kikubwa mno kwa umri wake tokana tu na kubebwa. Ila namaanisha kuwa kama kote huko alibebwa basi alipofikia angekuwa ni mzalendo/mchapa kazi/na mwenye kusimamia yale ambayo ni manufaa kwa wananchi kwa kuleta mabadiliko chanya ambayo ni wazi tatizo lisingekupo na hakuna haja ya kulalama juu ya hilo.
Nikirudi huo mfano nimetumia… Nimewatumia kama watu ambao walikuwa considered vilaza but they made it. Sikuwatumia mifano ya kubebwa… Hata hivo tukitumia hio kubebwa Eva Peron anafuzu katika mfano wa waliobebwa. Take note ni ngumu sana mtu ambae ni Changudoa kuja kuwa katika Siasa na hatimae kuja kuwa mtakatifu na kuweza futa historia yake hio kwa kuweza tukuka kwa watu wake. As much as alibebwa alikuja dhihirisha she had so much in her na uwezo mkubwa wa kuweza simamia maisha bora kwa wananchi
Dadangu AshaDii huku kubebwa ndiko tunakopinga, iwe ni kubebwa na mzazi wake ama mjomba, shangazi ama cousin. Kisichokubalika hapa na ndicho nilikuhoji ni uhalalisho wa mtu kubebwa.
Kwakuwa kwa kufanya hivyo kuna mtu anakuwa ana sifa zote zinazostahili kushika wadhifa huo lakini ananyimwa nafasi ya kulitumikia taifa lake na kujiletea maendeleo kwa sababu tu kuna mtu ana magodfather.
Kwakuwa hii nchi ni yetu sote basi ni lazima tupiganie kuwekwa mifumo ambayo inamruhusu kila mtanzania kutumia kipaji chake ama taaluma yake kupata nafasi ya kulitumikia taifa lake. Hatuwezi kuvumilia kuwa na serikali ya koo fulani fulani vizazi hata vizazi.
Mkuu hujamalizia huyo Rashid Mwema ni nani hapa nchini.UNDUGU NDANI YA SERIKALI
Wananchi wengi wamekuwa wakilalamikia utawala mbovu ndani ya CCM na serikali yake. IGP Mwema alipewa u IGP kwa sababu ya uhusiano wake na Rais ameridhika, hana wasiwasi kufukuzwa wala kuwajibishwa.Polisi wanafanya unyama hadi kuteka raia lakini IGP hawajibishwi wala kupewa onyo ya aina yoyote. Wote tunafahamu kwamba IGP ni shemejiye rais kikwete. Kwa hiyo utendaji wake mbovu wa kazi hauwezi kushugulikiwa. Ina maana kwamba rais kikwete hawezi kumfukuza shemeji yake kazi hata kama polisi wakiwaua raia million moja. Huu ndio mtindo katika taasiri nyingi za serikali. Utakuta mtu anapewa wadhisha siyo kwa sababu ana uwezo, ila ni either ni rafiki au ndugu ya watawala
UNDUGU NDANI YA CHAMA TAWALA:
Ndani ya chama chetu tawala, viongozi wamekuwa wakiwahujumu wale wasio na majina. Kwa mfano. January Makamba ambaye nakumbuka alipofutiwa mtihani wa kidato cha nne baada ya kuiba, alikweha ghafla akaenda marekani, kutoka marekani, akaingia Foreign Affairs, mara Ikulu. Baada ya muda mfupi baba yake, Yusuff Makamba (ambaye pia anatuhumiwa kubaka na hatimaye kumpa mwananfunzi mimba akiwa mwalimu ), kipindi hicho akiwa katibu mkuu wa CCM, alijigamba kwamba mwanaye lazima awe Waziri kwenye safari yake ya Urais, alipindisha taratibu na leo mwanaye ni Naibu waziri.
January hakupigiwa kura na mtu. Chini ya miaka 7 tangu atoke chuo, ameshapitia kila cheo kikubwa humu nchini. Jiulizeni Mwaka 2006, Mwamvita Makamba alikuwa anajishughulisha na shuguli za upambaji wa sherehe pale Ukonga Prisons Mess. Leo ni CEO Vodaom. Vijana wangapi wa Kitanzania wamefanya kazi nzuri ndani ya Vodacom hadi yeye na kaka yake ndio wapewe hizi nafasi zote? Hii ni mifano tu ambayo nadhani tungejadili kwa umakini kwa mustakabli wa taifa letu. Hiyo siyo chuki ni picha kamili. CCM ma serkali yake haina Uadilifu. Baadhi yetu tunatarajia kuingia upinzani 2014 uli kuwaonyesha hawa mafisadi kwamba nchi siyo yao.
Watoto wa wakubwa na wenye madaraka wanajazwa kwenye nafasi nyeti na kubwa za uongozi wa hili taifa. Ndani ya CCM hauwezi kupata uongozi bila kuwa na jina kubwa. Watoto wa Mwinyi, Karamagi, Kawawa, Sokoine, Kikwete, Nchimbi, Mzindakaya, Karume etc watoto wa wakulima wataenda wapi? Benki kuu, ubalozi, NSSF, Foreign Affairs, TRA, etc ni watoto wa wakubwa. Hii tunahitaje kwama siyo uongozi wa kifalme? Ukiwa mwanamke mzuri, unapata viti maalum, ubalozi, uku wa wilaya au mkoa. Ukiwa na ukaribu na watawala
MATOKEO YAKE
Matokeo ya haya yote yamekuwa ni muendelezo wa ufisadi na utawala mbovu. Hali imeendelea kuwa duni kwa sababu hawa ma- Mwinyi wameweka pamba masikioni wakiendelea kujineemesha kwa kodi zetu huku wakitutawala kwa mabavu. Hii ndio sababu kubwa ya hawa mapolisi kuzidi kuwaua raia kwa sababu, viongozi wao, wanaongoza kwa kujuana. CHAMA CHA MAPINDUZI inachukiwa mno kutokana na huu mwendelezo wa undugu na ufisadi. Hakuna hata mmoja anayeweza kuwajibishwa. Kutokana na madhambi yake. Waungwana, tunaomba mjadili hii mada kwa umakini. Tupo wabunge kadhaa Bungeni tunaotayarisha Mswada utakaojadiliwa katika kikao kijacho, ikiwa bi kiroboto atakiruhusu
Ngozimbili, Selemani, GameTheory, George Smiley, Dume La Mbegu na Msaidizi wao Nyani Ngabu, njooni mjibu mada siyo copy and paste
UNASHANGAA NINI , NENDA cuba UONE USULTANI MCHAFU UNAOFANYWA NA CASTRO. kaka ya ke karithi kiti cha castro cha uraisi. Mtoto wa kastro ndiye mkuu wa nuklear. Kastro ananyumba zaidi ya hamsini nchini cuba. Leo hulala hii na keshi ile. kachukua eneo kama lile la kigamboni na humo kajenga majumba yake. Nenda Gabon, huko hupati uraisi mpaka utoke katika familia ya Bongo!Kama kuna mtu aliyewahi kusoma na january makamba tupe data. Kingine mbona watoto wa Mkapa wako kimya. Kikwete wako kama baba yao. Sifuri kichwani.
Lazima tuwe na sheria itakayozuia nepotism and shield national interest.
SIKILIZA SIIPENDI CCM hata kidogo lakini January Makamba hakufutiwa MTIHANI kidato cha NNE; alifaulu vizuri na kwenda Form V; CBG huko TANGA... na ni kutokana na matatizo yake na Waalimu akafutiwa MTIHANI Boarding School kama Angeiba Shule yote Ingefungiwa Mitihani yake; Alijaribu as a Private Candidate hakufanya Vizuri kuingia CHUO KIKUU; akaenda Kufanya Kazi kwenye kampuni ya Wakimbizi huko KIGOMA ni ya Kimarekani; Vijana wengi wamepata SHULE Marekani kutokana na Hiyo Kazi na alisoma Chuo cha kikatoliki na Masters aliomba msaada wa Serikali ya Mkapa; na alisomea Conflicts Resolutions.
Kwa ninavyofahamu yeye alikuwa ni Mtu wa kwanza kuwa na Bachelor na Masters za Conflicts Resolutions Nchini na Masters.
Nchi ilimsomesha Foreign Affairs ikampa kazi sio kwa Sababu ya Kikwete ni Qualification na Mkapa... baadaye akaendelea Vizuri... So PLEASE REKEBISHA MEMORY YAKO...
* Kampuni ya Wakimbizi inaitwa Care International ni sababu ya kufanya kazi huko kulimfanya abadilishe Carrier na kusomea Conflicts Resolutions
Kuweka mambo sawa katika elimu 'conflict' na mwalimu/walimu haziwezi kukufutia matokeo unaweza kufukuzwa tu shule. Lakini kama umefanya mtihani wa taifa, hata kama baada ya mtihani huo ukamtoa ngeu hata katibu wa necta, mtihani wako utasahihishwa na kama umefaulu utafaulu tu maana kuna wanaokufa baada ya mitihani na matokeo yao huwa yanatoka. Hakuna jinsi ambavyo angeweza kugombana na mwalimu akaacha kumfukuza shule halafu akamfutia matokeo ya mtihani maana hairuhusiwi. Mi najua vijana wengi wamezama marekani baada ya kufeli na walitumia vyeti vya kufoji kupata admision vyuo vya marekani...asijekuwa mmoja wapo!!! Kwamba amefanya kazi na shirika la wakimbizi akitokea Tanga na akiwa kidato cha sita aliyefeli nalo ni suala la kuchunguzwa maana huwezi kuwa mkuu wa kambi ya Mtabila kama ilivyodaiwa katika uzi fulani humu kama ama hauna links na USALAMA WA TAIFA (Kumbuka kambi hizi zilikuwa mipakani na kulikuwa na harakati nyingi za kutengeneza vikosi vya majeshi hadi wengine wakauawa mle mle na pia jua Nyerere alikuwa msuluhishi kipindi hiki...kwa hiyo F6 aliyefeli kufanyakazi Care International na kuwa mkuu wa kambi ni lazima kuna namna maana si rahisi hivyo. La kujiuliza vema ni hili JANUARI ni jina la kikristu,Yusufu Makamba ni muislamu ilikuwaje akakubali mwanae abatizwe na yeye abakie Muislamu??? Mwenye masikio na asikie na msije shangaa kesho keshokutwa akawa waziri mkuu au ... shauri yetu wabongo!
Huyu mzee wanasema ana watoto wengi wa nje ya ndoa kuliko kawaida. Hivyo usishangae