Usultani: Mifano Mizuri ni Rashid Mwema na January Makamba

Muke Ya Muzungu

JF-Expert Member
Jun 17, 2009
3,444
264
UNDUGU NDANI YA SERIKALI
Wananchi wengi wamekuwa wakilalamikia utawala mbovu ndani ya CCM na serikali yake. IGP Mwema alipewa u IGP kwa sababu ya uhusiano wake na Rais ameridhika, hana wasiwasi kufukuzwa wala kuwajibishwa.Polisi wanafanya unyama hadi kuteka raia lakini IGP hawajibishwi wala kupewa onyo ya aina yoyote. Wote tunafahamu kwamba IGP ni shemejiye rais kikwete. Kwa hiyo utendaji wake mbovu wa kazi hauwezi kushugulikiwa. Ina maana kwamba rais kikwete hawezi kumfukuza shemeji yake kazi hata kama polisi wakiwaua raia million moja. Huu ndio mtindo katika taasiri nyingi za serikali. Utakuta mtu anapewa wadhisha siyo kwa sababu ana uwezo, ila ni either ni rafiki au ndugu ya watawala

UNDUGU NDANI YA CHAMA TAWALA:
Ndani ya chama chetu tawala, viongozi wamekuwa wakiwahujumu wale wasio na majina. Kwa mfano. January Makamba ambaye nakumbuka alipofutiwa mtihani wa kidato cha nne baada ya kuiba, alikweha ghafla akaenda marekani, kutoka marekani, akaingia Foreign Affairs, mara Ikulu. Baada ya muda mfupi baba yake, Yusuff Makamba (ambaye pia anatuhumiwa kubaka na hatimaye kumpa mwananfunzi mimba akiwa mwalimu ), kipindi hicho akiwa katibu mkuu wa CCM, alijigamba kwamba mwanaye lazima awe Waziri kwenye safari yake ya Urais, alipindisha taratibu na leo mwanaye ni Naibu waziri.

January hakupigiwa kura na mtu. Chini ya miaka 7 tangu atoke chuo, ameshapitia kila cheo kikubwa humu nchini. Jiulizeni Mwaka 2006, Mwamvita Makamba alikuwa anajishughulisha na shuguli za upambaji wa sherehe pale Ukonga Prisons Mess. Leo ni CEO Vodaom. Vijana wangapi wa Kitanzania wamefanya kazi nzuri ndani ya Vodacom hadi yeye na kaka yake ndio wapewe hizi nafasi zote? Hii ni mifano tu ambayo nadhani tungejadili kwa umakini kwa mustakabli wa taifa letu. Hiyo siyo chuki ni picha kamili. CCM ma serkali yake haina Uadilifu. Baadhi yetu tunatarajia kuingia upinzani 2014 uli kuwaonyesha hawa mafisadi kwamba nchi siyo yao.

Watoto wa wakubwa na wenye madaraka wanajazwa kwenye nafasi nyeti na kubwa za uongozi wa hili taifa. Ndani ya CCM hauwezi kupata uongozi bila kuwa na jina kubwa. Watoto wa Mwinyi, Karamagi, Kawawa, Sokoine, Kikwete, Nchimbi, Mzindakaya, Karume etc… watoto wa wakulima wataenda wapi? Benki kuu, ubalozi, NSSF, Foreign Affairs, TRA, etc ni watoto wa wakubwa. Hii tunahitaje kwama siyo uongozi wa kifalme? Ukiwa mwanamke mzuri, unapata viti maalum, ubalozi, uku wa wilaya au mkoa. Ukiwa na ukaribu na watawala

MATOKEO YAKE
Matokeo ya haya yote yamekuwa ni muendelezo wa ufisadi na utawala mbovu. Hali imeendelea kuwa duni kwa sababu hawa ma- Mwinyi wameweka pamba masikioni wakiendelea kujineemesha kwa kodi zetu huku wakitutawala kwa mabavu. Hii ndio sababu kubwa ya hawa mapolisi kuzidi kuwaua raia kwa sababu, viongozi wao, wanaongoza kwa kujuana. CHAMA CHA MAPINDUZI inachukiwa mno kutokana na huu mwendelezo wa undugu na ufisadi. Hakuna hata mmoja anayeweza kuwajibishwa. Kutokana na madhambi yake. Waungwana, tunaomba mjadili hii mada kwa umakini. Tupo wabunge kadhaa Bungeni tunaotayarisha Mswada utakaojadiliwa katika kikao kijacho, ikiwa "bi kiroboto" atakiruhusu

Ngozimbili, Selemani, GameTheory, George Smiley, Dume La Mbegu na Msaidizi wao Nyani Ngabu, njooni mjibu mada siyo copy and paste
 
Mbona husemi ndesamburo na lucy owenya.freeman mbowe na edwin mtei,zitto kabwe na muhonga.tundu lissu na dadake,kipenzi chetu dr.wilbroad slaa na kipenzi chake zamani....orodha haina mwisho.mbona hamjasema iweje iwe kwa january makamba pekee?mbona mnamuogopa sana huyu kijana mwenye kipaji.DAIMA JARIBIO LA KUMKASHIFU NA KUTAKA KUMHARIBIA JINA LITASHINDWA NA ZAIDI TUTAWAJUA TU KWA ROHO ZENU ZILIZOJAA CHUKI NA WIVU WA KIKE.NYIE HAKUNA KIZURI ISIPOKUWA CHA SLAA PEKE YAKE HUU NDO U DICTATOR WA MAWAZO!
 
Well said, hapo mkuu umenena sana tena kwa undani ila katika watoto wa wakubwa watoto wa Mwl Nyerere wako fukara kama watanzania wengine hawana kitu kama ni majina wametengeneza wenyewe na kama ni nyadhifa hakuna
hata mmoja ambaye ni mbunge, balozi, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa naibu waziri wala waziri pamoja na kuwa baba
yao alitawala miaka 25 sawa na vipindi vya vyote vya Mwinyi, Mkapa na Kikwete awamu nzima ya kwanza.

Badala ya Nyerere ulitakiwa kutaja watoto wa Karume na viongozi wengine wa serikali ya chama cha mapinduzi huyo Makongoro katengeneza jina mwenyewe alipokuwa mbunge Arusha mjini kupitia upinzani NCCR-Mageuzi hakubebwa na mtu yeyote serikalini maana miaka ile upinzani ulikuwa kama ugonjwa wa ukoma na huo uenyekit wa CCM wa mkoa wa Mara kaupata kutokana na kukubalika na kusema ukweli unaokabili viongozi wa chama tawala kuwa wamejaa rushwa, mafisadi, wabinafsi na hawana nia ya maendeleo dhahiri ya nchi ya Tanzania isipokuwa matumbo yao na familia zao
 
Kweli wewe nimeamini ni ngozi mbili niko nauhakika ngozi hiyzi ni govi,kama kweli ungekuwa na akili badala ya kujibu pumba ungetoa hoja ndio maana mtoa mada kasema tujadili kama wewe sio raia/mwananchi basi badala ya kupoteza muda wako kujibu pumba ni heri ungeipotezea nikupe akiba ya maneno mie kama naona post sijaikubali au kiuelewa japokuwa imeandikwa kwa kiswahili huwaga naipotezea tu na kwenda paande nyingine.wake up man leta hoja sio pumba kilaza mkubwa govi aka ngozi mbili
 
Mbona husemi ndesamburo na lucy owenya.freeman mbowe na edwin mtei,zitto kabwe na muhonga.tundu lissu na dadake,kipenzi chetu dr.wilbroad slaa na kipenzi chake zamani....orodha haina mwisho.mbona hamjasema iweje iwe kwa january makamba pekee?mbona mnamuogopa sana huyu kijana mwenye kipaji.DAIMA JARIBIO LA KUMKASHIFU NA KUTAKA KUMHARIBIA JINA LITASHINDWA NA ZAIDI TUTAWAJUA TU KWA ROHO ZENU ZILIZOJAA CHUKI NA WIVU WA KIKE.NYIE HAKUNA KIZURI ISIPOKUWA CHA SLAA PEKE YAKE HUU NDO U DICTATOR WA MAWAZO!

Sasa mbona haujajibu hoja mkuu?
 
Kama kuna mtu aliyewahi kusoma na january makamba tupe data. Kingine mbona watoto wa Mkapa wako kimya. Kikwete wako kama baba yao. Sifuri kichwani.
Lazima tuwe na sheria itakayozuia nepotism and shield national interest.
 
Mbona husemi ndesamburo na lucy owenya.freeman mbowe na edwin mtei,zitto kabwe na muhonga.tundu lissu na dadake,kipenzi chetu dr.wilbroad slaa na kipenzi chake zamani....orodha haina mwisho.mbona hamjasema iweje iwe kwa january makamba pekee?mbona mnamuogopa sana huyu kijana mwenye kipaji.DAIMA JARIBIO LA KUMKASHIFU NA KUTAKA KUMHARIBIA JINA LITASHINDWA NA ZAIDI TUTAWAJUA TU KWA ROHO ZENU ZILIZOJAA CHUKI NA WIVU WA KIKE.NYIE HAKUNA KIZURI ISIPOKUWA CHA SLAA PEKE YAKE HUU NDO U DICTATOR WA MAWAZO!
Ndesamburo hayuko serikalini na hana nia ya kuwania nafasi yoyote serikalini. Mzee Mtei pia hayuko serikalini, hana madaraka yoyote kwenye chama ila tu sifa za kuwa mwanzilishi. Kajipange upya. Huwezi kufananisha nafasi aliyotumia Mzee Makamba kuwajenga wanae, Kikwete kumpachika shemeji yake kama mkuu wa polisi, rafiki yake aliyekuwa anamtafutia visura London kama mkuu wa usalama wa taifa, na Shimbo aliyemhifadhi wakati alipotoroka Mondulu kama afisa wa juu jeshini. Nasikia hata huko usalama wa taifa wameanza kujazana watoto wa wakubwa hata kama hawana skills na ndio maana usalama wa taifa umedorora mpaka Waethiopia na wasomali wanasafirishwa kutoka mpaka wa Kenya hadi Malawi na hakuna anayejua kinachojiri.
 
SIKILIZA SIIPENDI CCM hata kidogo lakini January Makamba hakufutiwa MTIHANI kidato cha NNE; alifaulu vizuri na kwenda Form V; CBG huko TANGA... na ni kutokana na matatizo yake na Waalimu akafutiwa MTIHANI Boarding School kama Angeiba Shule yote Ingefungiwa Mitihani yake; Alijaribu as a Private Candidate hakufanya Vizuri kuingia CHUO KIKUU; akaenda Kufanya Kazi kwenye kampuni ya Wakimbizi huko KIGOMA ni ya Kimarekani; Vijana wengi wamepata SHULE Marekani kutokana na Hiyo Kazi na alisoma Chuo cha kikatoliki na Masters aliomba msaada wa Serikali ya Mkapa; na alisomea Conflicts Resolutions.

Kwa ninavyofahamu yeye alikuwa ni Mtu wa kwanza kuwa na Bachelor na Masters za Conflicts Resolutions Nchini na Masters.

Nchi ilimsomesha Foreign Affairs ikampa kazi sio kwa Sababu ya Kikwete ni Qualification na Mkapa... baadaye akaendelea Vizuri... So PLEASE REKEBISHA MEMORY YAKO...

* Kampuni ya Wakimbizi inaitwa Care International ni sababu ya kufanya kazi huko kulimfanya abadilishe Carrier na kusomea Conflicts Resolutions
 
nngu007

Waliosoma na January Galanos wanasema kwamba alifutiwa mtihani. Alikuja kureseat kama private candidate. Form 6 akafeli alipata DIV-4 Akashindwa kwenda chuo kikuu. Ni ufisadi ndio uliomsaidia hadi kupata scholarship

1. Jiulize, mtu aliyefeli anawezaje kupata scholarship kama siyo ufisadi. Wale wanaopata DIV 1 wanakosaje skolaship kama siyo ufisadi. January ni fisadi. Tuelezwe aliwavukaje hao wengine hadi kapewa scholarship?
2. Mwenyewe unadiriki kutamka kwamba hakufanya vizuri, Iweje apate hivyo vyeo vyeto kama siyo kubebwa?
3. Wale waliofaulu mbele yake wako wapi? Si walivukwa kwa sababu ni mtoto wa makamba
4. Kuanzia leo ahachane na mambo ya kujigamba kwamba ana akili. Mwenye akili awe yeye?

Wenye akili wapo. Wamejaa nje ya nchi kwa sababu hawana ndugu ndani ya system kuwabeba. Wakija bongo wanazungushwa weee hadi wanakata tamaa. January anajitakia haya yote kwa majigambo yake. Vilaza wanaobebwa bewa tu hawa. Waliosoma naye wakaenda chuo na kupata First class honors wanabaki kuwa maofisa kwenye wizara wakati wao bila chochote cha maana wanarukishwa tu,,,, 2015 inakuja watatafuta pa kujifichia
 
Last edited by a moderator:
Waliosoma na January Galanos wanasema kwamba alifutiwa mtihani. Alikuja kureseat kama private candidate. Form 6 akafeli alipata DIV-4 Akashindwa kwenda chuo kikuu. Ni ufisadi ndio uliomsaidia hadi kupata scholarship

1. Jiulize, mtu aliyefeli anawezaje kupata scholarship kama siyo ufisadi. Wale wanaopata DIV 1 wanakosaje skolaship kama siyo ufisadi. January ni fisadi. Tuelezwe aliwavukaje hao wengine hadi kapewa scholarship?
2. Mwenyewe unadiriki kutamka kwamba hakufanya vizuri, Iweje apate hivyo vyeo vyeto kama siyo kubebwa?
3. Wale waliofaulu mbele yake wako wapi? Si walivukwa kwa sababu ni mtoto wa makamba
4. Kuanzia leo ahachane na mambo ya kujigamba kwamba ana akili. Mwenye akili awe yeye?

Wenye akili wapo. Wamejaa nje ya nchi kwa sababu hawana ndugu ndani ya system kuwabeba. Wakija bongo wanazungushwa weee hadi wanakata tamaa. January anajitakia haya yote kwa majigambo yake. Vilaza wanaobebwa bewa tu hawa. Waliosoma naye wakaenda chuo na kupata First class honors wanabaki kuwa maofisa kwenye wizara wakati wao bila chochote cha maana wanarukishwa tu,,,, 2015 inakuja watatafuta pa kujifichia


1st Degree hakupata Scholarship only Masters... Soma Vizuri... Yeah Wanabebana ni CHAMA TAWALA... SIKIPENDI HICHO CHAMA..
 
Usultani unaujuwa au unausikia tu? cheki huu to start with:
3.jpg

2.jpg


Su huyo tu, na Mbowe na Baba'mkwe wake.
 
Usultani unaujuwa au unausikia tu? cheki huu to start with:
3.jpg

2.jpg


Su huyo tu, na Mbowe na Baba'mkwe wake.
Tunajua unapotosha makusudi. Mzee Mtei hana cheo chochote katika chama mbali ya kuwa mwanzishi. Freeman aliupata uongozi kwenye chama kwa merits zake mwenyewe. Hii ni tofauti na hulka zenu CCM.
 
Mbona husemi ndesamburo na lucy owenya.freeman mbowe na edwin mtei,zitto kabwe na muhonga.tundu lissu na dadake,kipenzi chetu dr.wilbroad slaa na kipenzi chake zamani....orodha haina mwisho.mbona hamjasema iweje iwe kwa january makamba pekee?mbona mnamuogopa sana huyu kijana mwenye kipaji.DAIMA JARIBIO LA KUMKASHIFU NA KUTAKA KUMHARIBIA JINA LITASHINDWA NA ZAIDI TUTAWAJUA TU KWA ROHO ZENU ZILIZOJAA CHUKI NA WIVU WA KIKE.NYIE HAKUNA KIZURI ISIPOKUWA CHA SLAA PEKE YAKE HUU NDO U DICTATOR WA MAWAZO!

daah umenichoma kweli..lakini CHADEMA na mimi ni kama mkanda na suruwali..
 
Usultani utaiangamiza nchi.sanduku la kura paleeee 2015 tunalisubiri kwa hamu
 
....[/QUOTE]
Hivyo Ngozimbili tujibu kosa kwa Makosa? Mtu akiiba na wewe uibe kwa sababu fulani ni mwizi?
 
nngu007

Mkuu thanx kwa kuweka kumbukumbu sawa........sasa mbona elimu na kazi alizowahi kufanya kwa mujibu wa taarifa ni out of profession????? Mbona kama in a way unakubaliana na HonMP on nepotism.......????? Au hoja yako hapa inapeleka mjadala upande gani???
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom