Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,891
Herehoa!
Siasa zilianzishwa Kwa maslahi ya viongozi na watu wapendao utawala!
Biashara zilianzishwa Kwa maslahi ya wafanyabiashara kujipatia faida!
Mtu huanzisha kitu Kwa maslahi yake au kundi litakalomuunga Mkono!
Mtu Fulani huweza kuamua kutaka kuongoza wengine na kupigania maslahi ya jamii yake. Kwa kupinga dhuluma, uonevu, na Aina zote za uhalifu katika jamii yake. Lakini ili mwanasiasa afanye hayo itampasa aamue kuonea jamii zingine Kwa kuzifanyia uonevu, dhulma au Aina yoyote ya uhalifu.
Wazungu na Nchi za ulimwengu WA Kwanza zamani zilikuwa na Siasa Kama zetu au ambazo zinakaribiana na Siasa zetu. Lakini wakagundua namna Bora ya kuondoa malalamiko, uonevu, dhulma na uhalifu Kwa watu wetu wenyewe itawapasa kuvamia mataifa mengine. Na ndipo yakafikia uamuzi wa kuvamia nchi zingine zikiwemo nchi zetu za Afrika.
Ili tuwe na Uhuru ni lazima tuchafue nchi zingine. Tusipochafua tutachafuliwa, tusipoonea tutaonewa, tusipodhulumu tutadhulumiwa hizo ni kanuni za Siasa Kwa sisi Wanafalsafa.
Sio ajabu CHADEMA kila mwaka wakilalamika kuibiwa Kura na kuonewa. Siasa ziko hivyo. Hata hivyo wanamlalamikia Nani hasa. Kisiasa kanuni inayotumika ni kuhakikisha hauwi mhanga Bali unakuwa msababishaji na mpokea lawama.
Kisiasa ni Bora uambiwe unaiba Kura kuliko wewe ndio uwe mlalamishi.
Ili malalamiko haya yaishe, ni wajibu wetu kutafuta nchi ya kuzipelekea mambo yetu mabaya, sio Jambo dogo lakini linawezekana, Kwa maana hivi tunavyoishi ndio shida zaidi kuliko kuvamia wengine.
Wazungu walishatuvamia Hilo halina ubishi, wakatuonea na Siasa zao.
Waarabu, wahindi na wachina Leo ndio wapo nchini kwetu wakimiliki Kwa sehemu kubwa uchumi wetu, makampuni makubwa wao ndio wanayamiliki. Unajua maana yake hiyo?
Siasa za kujipendekeza Kwa wageni ndizo zinafanya uonevu uzidi Kwa wazawa wa nchi husika. Wakija tunajikomba kwao, wasipokuja basi tutawafuata huko kwao kujipendekeza.
Siasa ni uonevu ambao hutumia sera za ushawishi pasipo watu kujua.
Tanzania itatulazimu kuandaa kizazi bora kinachozijua Siasa za uonevu Kwa mataifa mengine, kizazi kilichopo nafikiri hakina Uelewa wa hiki nikisemacho. Sio ajabu hatuna watu wenye roho na akili zinazoweza kupanga mipango kabambe ya kudhibiti nchi zingine, isipokuwa tunauwezo wa kudhibitiana wenyewe Kwa wenyewe.
Juzi nilipata kusikia habari za Dada wa kinaijeria aliyeishutumu Hoteli Fulani Zanzibar Kwa kuratibu tukio la kubakwa kwake.
Ile Kwa wanasiasa na vijana machachari wa kitanzania wangemdhibiti vyema Kwa upande wa Mtandaoni, mpaka Ajue kuwa nchi yetu inaumoja.
Ukarimu uliopitiliza unaweza kuleta Siasa za uonevu ndani ya nchi yetu.
Na hii chanzo chake niliwahi kulisema, jamii zetu Mgeni anathaminiwa kuliko mwenyeji. Ni kawaida Mgeni akifika katika nyumba zetu kulikuwa chakula kizuri na kuwekewa katika vyombo vizuri ambavyo watoto wetu hatuwaruhusu kuvitumia, huo tunauita ukarimu lakini kimsingi ni upuuzi na kuwatengenezea watoto kasumba mbaya.
Ni vizuri kuwakarimu wageni lakini sio Kwa kiwango cha kuwadunisha watoto wetu au wenyeji wetu.
Hapa bongo, Akiletwa Mzungu au Mgeni kutoka Kenya kufanya kazi labda ni Udaktari au ualimu sio ajabu akalipwa pesa ndefu kuliko mzawa.
Lakini uliwahi kujiuliza Mtanzania akienda Kenya au nchi za nje atalipwa kuliko wenyeji?
Jibu ni hapana, Nina watu ninaoeafahamu wapo nchi za barafu huko Norway, UK, Ufaransa n.k. wote hulipwa mishahara ya kawaida na wengine hulipwa midogo zaidi kuliko Kwa kazi Ileile.
Hii IPO hata kwenye mpira, na Fani zingine.
Hii inatokana na kasumba mbaya ya Siasa ambazo tuliamua kujifanyia na kufanyiana uonevu sisi Kwa Sisi badala ya kukupeleka uonevu Kwa watu wengine hasa wasiotuheshimu.
Taikon nitaendelea kusema Jambo hili kadiri ya nitakapopata nafasi mpaka Dhana hii itakapowaingia waliowengi. Na naamini siku moja watatokea viongozi watakaofanya kile nilichokisema.
Nimemaliza!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Siasa zilianzishwa Kwa maslahi ya viongozi na watu wapendao utawala!
Biashara zilianzishwa Kwa maslahi ya wafanyabiashara kujipatia faida!
Mtu huanzisha kitu Kwa maslahi yake au kundi litakalomuunga Mkono!
Mtu Fulani huweza kuamua kutaka kuongoza wengine na kupigania maslahi ya jamii yake. Kwa kupinga dhuluma, uonevu, na Aina zote za uhalifu katika jamii yake. Lakini ili mwanasiasa afanye hayo itampasa aamue kuonea jamii zingine Kwa kuzifanyia uonevu, dhulma au Aina yoyote ya uhalifu.
Wazungu na Nchi za ulimwengu WA Kwanza zamani zilikuwa na Siasa Kama zetu au ambazo zinakaribiana na Siasa zetu. Lakini wakagundua namna Bora ya kuondoa malalamiko, uonevu, dhulma na uhalifu Kwa watu wetu wenyewe itawapasa kuvamia mataifa mengine. Na ndipo yakafikia uamuzi wa kuvamia nchi zingine zikiwemo nchi zetu za Afrika.
Ili tuwe na Uhuru ni lazima tuchafue nchi zingine. Tusipochafua tutachafuliwa, tusipoonea tutaonewa, tusipodhulumu tutadhulumiwa hizo ni kanuni za Siasa Kwa sisi Wanafalsafa.
Sio ajabu CHADEMA kila mwaka wakilalamika kuibiwa Kura na kuonewa. Siasa ziko hivyo. Hata hivyo wanamlalamikia Nani hasa. Kisiasa kanuni inayotumika ni kuhakikisha hauwi mhanga Bali unakuwa msababishaji na mpokea lawama.
Kisiasa ni Bora uambiwe unaiba Kura kuliko wewe ndio uwe mlalamishi.
Ili malalamiko haya yaishe, ni wajibu wetu kutafuta nchi ya kuzipelekea mambo yetu mabaya, sio Jambo dogo lakini linawezekana, Kwa maana hivi tunavyoishi ndio shida zaidi kuliko kuvamia wengine.
Wazungu walishatuvamia Hilo halina ubishi, wakatuonea na Siasa zao.
Waarabu, wahindi na wachina Leo ndio wapo nchini kwetu wakimiliki Kwa sehemu kubwa uchumi wetu, makampuni makubwa wao ndio wanayamiliki. Unajua maana yake hiyo?
Siasa za kujipendekeza Kwa wageni ndizo zinafanya uonevu uzidi Kwa wazawa wa nchi husika. Wakija tunajikomba kwao, wasipokuja basi tutawafuata huko kwao kujipendekeza.
Siasa ni uonevu ambao hutumia sera za ushawishi pasipo watu kujua.
Tanzania itatulazimu kuandaa kizazi bora kinachozijua Siasa za uonevu Kwa mataifa mengine, kizazi kilichopo nafikiri hakina Uelewa wa hiki nikisemacho. Sio ajabu hatuna watu wenye roho na akili zinazoweza kupanga mipango kabambe ya kudhibiti nchi zingine, isipokuwa tunauwezo wa kudhibitiana wenyewe Kwa wenyewe.
Juzi nilipata kusikia habari za Dada wa kinaijeria aliyeishutumu Hoteli Fulani Zanzibar Kwa kuratibu tukio la kubakwa kwake.
Ile Kwa wanasiasa na vijana machachari wa kitanzania wangemdhibiti vyema Kwa upande wa Mtandaoni, mpaka Ajue kuwa nchi yetu inaumoja.
Ukarimu uliopitiliza unaweza kuleta Siasa za uonevu ndani ya nchi yetu.
Na hii chanzo chake niliwahi kulisema, jamii zetu Mgeni anathaminiwa kuliko mwenyeji. Ni kawaida Mgeni akifika katika nyumba zetu kulikuwa chakula kizuri na kuwekewa katika vyombo vizuri ambavyo watoto wetu hatuwaruhusu kuvitumia, huo tunauita ukarimu lakini kimsingi ni upuuzi na kuwatengenezea watoto kasumba mbaya.
Ni vizuri kuwakarimu wageni lakini sio Kwa kiwango cha kuwadunisha watoto wetu au wenyeji wetu.
Hapa bongo, Akiletwa Mzungu au Mgeni kutoka Kenya kufanya kazi labda ni Udaktari au ualimu sio ajabu akalipwa pesa ndefu kuliko mzawa.
Lakini uliwahi kujiuliza Mtanzania akienda Kenya au nchi za nje atalipwa kuliko wenyeji?
Jibu ni hapana, Nina watu ninaoeafahamu wapo nchi za barafu huko Norway, UK, Ufaransa n.k. wote hulipwa mishahara ya kawaida na wengine hulipwa midogo zaidi kuliko Kwa kazi Ileile.
Hii IPO hata kwenye mpira, na Fani zingine.
Hii inatokana na kasumba mbaya ya Siasa ambazo tuliamua kujifanyia na kufanyiana uonevu sisi Kwa Sisi badala ya kukupeleka uonevu Kwa watu wengine hasa wasiotuheshimu.
Taikon nitaendelea kusema Jambo hili kadiri ya nitakapopata nafasi mpaka Dhana hii itakapowaingia waliowengi. Na naamini siku moja watatokea viongozi watakaofanya kile nilichokisema.
Nimemaliza!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam