Wacha leo niseme juu ya hii kitu
1. Kwanza ni nini? Jina lake ni utoko kwa Kiswahili sanifu kabisa, tofauti na wengi hasa waislam ( samahani lakini ni kuelimishana tu maana wengine mtapanic hapa tu) mlivyoaminishwa kuwa ni uchafu si uchafu, unapotoka nje kwenye chupi hapo ni uchafu lakini ukiwa uko ndani kwenye ajili yake si uchafu.
Nitatoa mfano ndani ya tumbo lako kuna utumbo wenye kupitisha masalia the minute yanatoka kwenye haja hapo tunasafisha ni uchafu, mbona hujikamui utumbo ukasema unatembea na uchafu.
Pili Masikio mdomo pua hutoa uchafu lakini mbona hujikamui ni unasubiri mpaka utoke kwa kuuhisi au kuona?
Kwa nini mnang’ang’ania kuvuruga asili ya uke, mnajua madhara yake??
2. Ukiingiza uume ukatoka na hivyo vitu vyeupe jua mke/ mpenzi wako ana muda kiasi hajafanya hilo tendo.
Mimi ni mwanamke najua ninachozungumza. Uke ukitumika leo na kesho na kuendelea hukuti hiyo kitu.
Kwa maana nyingine mnawasaidia wenza wenu( wale wasio waaminifu) kuiondoa hii alama kizembe sana poleni[emoji3][emoji3][emoji3]wanawake nisamehe nimetoka siri ya kambi leo.
3. Utoko asili hauna madhara kwa mwanamme na hauna harufu mbaya ya kukera, ukikutana na harufu mbaya mpeleke mwenzio apate matibabu ni mgonjwa, nukta.
4. Utoko ni afya ya uke ni maumbile alivyotuumba Mungu, na kila alichoumba Mungu ni chema na kupendeza acheni mbwembwe za kusokomeza sijui magadi, ndimu, vidole, vistick, kuchomelea udi n.k.
Uke na uheshimiwe uwe asili. Uke ni zawadi asili tuliyopewa wanawake[emoji847][emoji847]. Uke wake uume vingine ni matumizi mabaya ya uke asili wa mwanamke!!
5. Utoko si uchafu ukiwa ndani ya uke. Nasisitiza mpaka utoke hapo nje mahali tu naona na kushika na kunusa hapo ndio uchafu.
NIMEMALIZA!