Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,341
- 51,907
USITAFUTE UMÀARUFU KWA NGUVU UTAJIDHALILISHA NA KUISHIA KUJICHUKIA.
Anaandika, Robert Heriel.
Mtibeli.
Watu wengi hupenda kujulikana, na wengi huhusisha kujulikana kama moja ya nguzo za kuheshimiwa. Kuna ukweli katika hilo lakini itategemea unajulikana kwa jambo gani. Nini kinachopelekea wewe kufahamika.
Na Watu wengi ambao hulazimisha kujulikana na ikatokea wakajulikana mara nyingi utawatambua kwa majivuno, dharau na kiburi walichonacho. Fikiria mtu ati anakudharau au anakiburi kisa anajulikana. Inachekesha sio!
Katika mchakato wa kutafuta kujulikana wengi hujikuta katika mateso makubwa, utumwa na hata kutenda mambo ya hovyo yanayowadhalilisha au kubomoa jamii.
Fikiria mtu anatafuta kujulikana kwa kutukana Watu wengine hasa Watu mashuhuri ili naye ajulikane.
Fikiria mtu anatunga taarifa za uzushi zenye kuvuta akili za Watu kirahisi ili ajulikane.
Fikiria mtu anafanya tukio la kipuuzi ikiwezekana kuvujisha picha za uchi ili ajulikane.
Fikiria mtu anatunga hadithi zisizo na maadili kama za kishoga au kisagaji ili kupata kujulikana.
Elewa kuwa uongo unasafiri haraka kuliko Ukweli. Lakini uongo licha ya kasi kubwa lakini hufa mapema lakini ukweli haufi.
Ili ufurahie kujulikana au umaarufu basi hakikisha haya yanafanyika;
1. Kuwa Mnyenyekevu na mpole
Kuwa kama Taikon Master, Mtibeli au Watibeli wengine. Usidharau mtu. Mheshimu kila mtu kwa kuzingatia kigezo cha tabia njema na uadilifu.
Saidia yeyote anayekuomba msaada.
Usijione Bora kuliko wengine.
Usiwe mjivuni mbele za Watu duni (ambao unaona umewazidi mambo fulani)
2. Ukifanya jambo lolote usitegemee kulipwa iwe kwa sifa, mali au chochote. Furaha yako iwe kusaidia Watu na kubadilisha maisha ya Watu wengine wawe bora.
3. Kazi zako na kipaji chako ndio kikutangaze.
4. Ishi Kawaida. Kujulikana isiwe sababu ya kutaka ku- Fake maisha.
Maisha uliyonayo ndio yako. Usitake kwa vile Watu wanakujua basi ufikiri umependa daraja la kutakiwa kuwa na maisha ya kifahari. Maisha mazuri ni vile utakavyoishi kwa uhalisia ulionao.
5. Hakikisha kujulikana kwako kuwe na faida ndani ya jamii. Usiharibu jamii yako. Inakudhalilisha na mwishowe utakuja kujichukia na hiyo itafanya uyaone maisha hayana maana.
6. Hakikisha unajenga pale palipobomoka.
Zipo kasumba ambazo umezikuta ambazo baadhi ni Wrong ideologies, Kwa mfano kabila lako labda linalaumiwa kwa tabia fulani mbaya. Basi jitahidi ujenge pale ambapo kuna mtu kwenye kabila lenu alipabomoa na kuharibu sifa za jamii uliyotoka ili uwathibitishie kuwa ninyi hampo hivyo. Na kuna Watu wengi wema na wazuri katika jamii yenu.
7. Usitake kujulikana kwa sababu ya Pesa. Utaishia kujidhalilisha.
8. Usitumie kujulikana kwako kama sehemu ya kuvunja haki za wengine.
Ni kweli unaweza kuwa unafahamika, ni maarufu lakini usipende kutumia umaarufu wako kudhulumu haki za wengine. Huko ni kujidhalilisha na utajichukia.
9. Hakikisha unatumia kujulikana kwako kutetea Haki na wanyonge wanaoonewa.
Usiwe kibaraka wa waovu au watawala wahalifu na waovu. Pale unapoona jambo haliendi sawa, sema kwa ukweli bila kumpunja yeyote. Usimpunje mwenye haki wala usimuadhibu isivyohaki Muovu.
10. Hakikisha watoto wako wataheshimika kwa umaarufu ulionao. Yaani uwe umaarufu wenye uadilifu.
Kuwa maarufu kwa mambo ya kihalifu au uovu ni kuwanyima watoto na familia yako haki. Fikiria watoto wako wataishije ikiwa Mama yao ni Kahaba Maarufu? Fikiria watoto wako wataishije ikiwa baba yao ni shoga maarufu? Au unajulikana kwa kuuza madawa ya kulevya na kuharibu watoto wa wengine?
Kwa nini uwabebeshe mzigo watoto wako kujenga mahali ulipobomoa wewe? Muda wa kujenga mahali pao penyewe wataupata wapi?
Acha ubinafsi.
Kujulikana ni jambo zuri ikiwa utajulikana kwa uadilifu na mambo yenye tija ndani ya jamii yako.
Fikiria unaandika mambo ya kuchochea ushoga au uasherati alafu siku watoto wako wasome huo uchafu wako alafu wafanyiane kile ulichokiandika wewe baba au mama yao.
Taikon ninajua kuwa kila mtu, ndio hata wewe unakitu kizuri na chema ambazo ukikitumia vizuri kitakufanya ujulikane na kuheshimiwa kupitia kitu hicho. Jaribu kulinda heshima yako ili kujenga heshima ya watoto wako.
Ukizeeka utazeeka kwa uzee mwema. Na ukifa utakufa kwa kifo cha kheri ambacho utaacha watoto wako wakiwa katika hali ya kujivunia. Pesa na Utajiri pekee havitoshi kuwarithisha watoto. Bali warithishe na jina bora, jina lenye heshima.
Watu wakisema, watoto wa fulani(wako) wajivunie maisha yako.
Hivyo ndivyo Watibeli tulivyo.
Nipumzike sasa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Anaandika, Robert Heriel.
Mtibeli.
Watu wengi hupenda kujulikana, na wengi huhusisha kujulikana kama moja ya nguzo za kuheshimiwa. Kuna ukweli katika hilo lakini itategemea unajulikana kwa jambo gani. Nini kinachopelekea wewe kufahamika.
Na Watu wengi ambao hulazimisha kujulikana na ikatokea wakajulikana mara nyingi utawatambua kwa majivuno, dharau na kiburi walichonacho. Fikiria mtu ati anakudharau au anakiburi kisa anajulikana. Inachekesha sio!
Katika mchakato wa kutafuta kujulikana wengi hujikuta katika mateso makubwa, utumwa na hata kutenda mambo ya hovyo yanayowadhalilisha au kubomoa jamii.
Fikiria mtu anatafuta kujulikana kwa kutukana Watu wengine hasa Watu mashuhuri ili naye ajulikane.
Fikiria mtu anatunga taarifa za uzushi zenye kuvuta akili za Watu kirahisi ili ajulikane.
Fikiria mtu anafanya tukio la kipuuzi ikiwezekana kuvujisha picha za uchi ili ajulikane.
Fikiria mtu anatunga hadithi zisizo na maadili kama za kishoga au kisagaji ili kupata kujulikana.
Elewa kuwa uongo unasafiri haraka kuliko Ukweli. Lakini uongo licha ya kasi kubwa lakini hufa mapema lakini ukweli haufi.
Ili ufurahie kujulikana au umaarufu basi hakikisha haya yanafanyika;
1. Kuwa Mnyenyekevu na mpole
Kuwa kama Taikon Master, Mtibeli au Watibeli wengine. Usidharau mtu. Mheshimu kila mtu kwa kuzingatia kigezo cha tabia njema na uadilifu.
Saidia yeyote anayekuomba msaada.
Usijione Bora kuliko wengine.
Usiwe mjivuni mbele za Watu duni (ambao unaona umewazidi mambo fulani)
2. Ukifanya jambo lolote usitegemee kulipwa iwe kwa sifa, mali au chochote. Furaha yako iwe kusaidia Watu na kubadilisha maisha ya Watu wengine wawe bora.
3. Kazi zako na kipaji chako ndio kikutangaze.
4. Ishi Kawaida. Kujulikana isiwe sababu ya kutaka ku- Fake maisha.
Maisha uliyonayo ndio yako. Usitake kwa vile Watu wanakujua basi ufikiri umependa daraja la kutakiwa kuwa na maisha ya kifahari. Maisha mazuri ni vile utakavyoishi kwa uhalisia ulionao.
5. Hakikisha kujulikana kwako kuwe na faida ndani ya jamii. Usiharibu jamii yako. Inakudhalilisha na mwishowe utakuja kujichukia na hiyo itafanya uyaone maisha hayana maana.
6. Hakikisha unajenga pale palipobomoka.
Zipo kasumba ambazo umezikuta ambazo baadhi ni Wrong ideologies, Kwa mfano kabila lako labda linalaumiwa kwa tabia fulani mbaya. Basi jitahidi ujenge pale ambapo kuna mtu kwenye kabila lenu alipabomoa na kuharibu sifa za jamii uliyotoka ili uwathibitishie kuwa ninyi hampo hivyo. Na kuna Watu wengi wema na wazuri katika jamii yenu.
7. Usitake kujulikana kwa sababu ya Pesa. Utaishia kujidhalilisha.
8. Usitumie kujulikana kwako kama sehemu ya kuvunja haki za wengine.
Ni kweli unaweza kuwa unafahamika, ni maarufu lakini usipende kutumia umaarufu wako kudhulumu haki za wengine. Huko ni kujidhalilisha na utajichukia.
9. Hakikisha unatumia kujulikana kwako kutetea Haki na wanyonge wanaoonewa.
Usiwe kibaraka wa waovu au watawala wahalifu na waovu. Pale unapoona jambo haliendi sawa, sema kwa ukweli bila kumpunja yeyote. Usimpunje mwenye haki wala usimuadhibu isivyohaki Muovu.
10. Hakikisha watoto wako wataheshimika kwa umaarufu ulionao. Yaani uwe umaarufu wenye uadilifu.
Kuwa maarufu kwa mambo ya kihalifu au uovu ni kuwanyima watoto na familia yako haki. Fikiria watoto wako wataishije ikiwa Mama yao ni Kahaba Maarufu? Fikiria watoto wako wataishije ikiwa baba yao ni shoga maarufu? Au unajulikana kwa kuuza madawa ya kulevya na kuharibu watoto wa wengine?
Kwa nini uwabebeshe mzigo watoto wako kujenga mahali ulipobomoa wewe? Muda wa kujenga mahali pao penyewe wataupata wapi?
Acha ubinafsi.
Kujulikana ni jambo zuri ikiwa utajulikana kwa uadilifu na mambo yenye tija ndani ya jamii yako.
Fikiria unaandika mambo ya kuchochea ushoga au uasherati alafu siku watoto wako wasome huo uchafu wako alafu wafanyiane kile ulichokiandika wewe baba au mama yao.
Taikon ninajua kuwa kila mtu, ndio hata wewe unakitu kizuri na chema ambazo ukikitumia vizuri kitakufanya ujulikane na kuheshimiwa kupitia kitu hicho. Jaribu kulinda heshima yako ili kujenga heshima ya watoto wako.
Ukizeeka utazeeka kwa uzee mwema. Na ukifa utakufa kwa kifo cha kheri ambacho utaacha watoto wako wakiwa katika hali ya kujivunia. Pesa na Utajiri pekee havitoshi kuwarithisha watoto. Bali warithishe na jina bora, jina lenye heshima.
Watu wakisema, watoto wa fulani(wako) wajivunie maisha yako.
Hivyo ndivyo Watibeli tulivyo.
Nipumzike sasa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam