Usipokee simu iwapo katika charge

Usipokee simu iwapo katika charge

si kweli...habari ya hovyo hii..ni kuipuuza tu..
We endelea kubisha kila kitu kama Kenge. Ngoja siku ulipuliwe na hicho kisimu chako cha Mchina ndio utajua kuwa hiyo habari ni ya kweli au siyo kweli.
 
E jamani kwann mabishano? Msg sent aliesikia kasikia wanaoona si ya kweli endeleeni kubisha....ndo waleee wanaoamini hakuna Mungu kesho wakimkuta sijui wataomba kurudi duniani!!?????
 
E jamani kwann mabishano? Msg sent aliesikia kasikia wanaoona si ya kweli endeleeni kubisha....ndo waleee wanaoamini hakuna Mungu kesho wakimkuta sijui wataomba kurudi duniani!!?????
Ungelijua watu wangapi duniani wanaongea na simu zikiwa kwenye charger, usingeendelea kuelezea hii habari. Msipokee kila lisemwalo.
 
Mi natumia BlackBerry,simu ikiwa chaji kuna maeneo nikigusa,inatetemesha(sisimua) kiana
 
Salim Kikeke
WAPENZI SAMBAZENI UJUMBE HUU.
Kwa mara nyengine tena kijana wa India-
Mumbai Amefariki dunia Leo asubuhi,
alipokua akipokea simu aina ya Android
ilipokua kaika Charge. alipopokea Madaktari
wanasema alihisi mtetemo katika Moyo wake
na mkonononi akarushwa na umeme
(akaungua)
-Tafadhali usipokee Simu pindi iwapo katika
Charge
-Tafadhali usijibu Simu pindi iwapo katika
Charge
Kwa Sababu Miale ya Simu inaguvu mara
1000 zaidi ya
ufikiliavyo...
USIPOKEE SIMU IWAPO KATIKA CHARGE
Tafadhali #Share kwa Marafiki waone Ujumbe
huu.
maajabu ya dunia mkuu naomba uweke source ya habari ili tuione kwa mapana zaidi na siyo kiufupi zaidi
 
Sijakusoma
Nina maanisha mamilioni ya watu kila siku huongea na simu zikiwa kwenye charger na hakuna matatizo yoyote yanayowapata. Hiyo story ya mtoa maada ni unique case ambayo kwa akili ya kawaida haingii kabisa kichwani labda angetwambia kulitokea radi or something ndo ikampiga huyo mtumiaji otherwise hiyo ni myth.
 
Ni busara sana kama hujui jambo ukauliza,au ukatafuta kwenye internet ukajihabarisha badala ya kubeza bila kufanya jitihada zozote.
Wakuu tunachotakiwa kujua ni kwamba mwili wa mwanadamu unatumia damu,damu husukumwa na moyo
ambao wanasayansi wanajua una nguvu fulani ya umeme ambayo huuwezesha kufanya shughuli zake vizuri,
umeme huu unapoingiliwa na umeme mwingine kutoka nje huusababishia kufanya kazi bila mpangilio
na wakati mwingine husimama na kusababisha damu kushindwa kufikia sehemu muhimu za mwili
na hii inaweza kusababisha kifo kama huyo mgonjwa yuko mbali na daktari anayejua afanye nini ili kumuokoa.
Madaktari wanajua wanapoletewa mgonjwa aliyepigwa na umeme hata kama anaonyesha anaendelea vizuri kuna kipimo wanamfanyia kuhakikisha moyo wake upo vizuri kimapigo/normal operation.
Mimi nadhani kwa kuwa jf ni uwanja wa kuhabarishana,na tumepata mengi humu ni vema unapopata uzi wenye
lengo la kuleta taarifa,tuulize maswali mleta uzi atujibu,tuboreshe pale tunapoona tuna taarifa nzuri zaidi ili mwisho tunufaike sote.
Mambo ya afya ni tofauti na siasa,hapa hakuna ushabiki maana kila mtu anatakiwa kuwa na afya njema tuendelee na maisha.Niseme sisi kazini kwetu kwenye safety procedure ni marufuku kupokea simu ikiwa kwenye charge kwa sababu ya kuepuka madhara aliyoyasema mleta uzi.
Kwa wanaoendelea kuenzi mazoea,endeleeni mpaka hapo ndugu zenu watakapoleta ushuhuda wa marehemu humu jukwaani,kwa wapenda mafundisho ni vema hili ukaliongeza kwenye mambo mapya unayojifunza
asanteni.
 
Uwongo huo. Tangu hizi habari zisambazwe viwanda vya simu vingeshatoa tahadhari kwenye user's manual.
 
Jamani hadi mtu kuchukua hadhar kwa maisha yake mwenyewe pia tunasubiri tuekewe kwenye manuals? E wazungu set us ( africans) free
 
Ni busara sana kama hujui jambo ukauliza,au ukatafuta kwenye internet ukajihabarisha badala ya kubeza bila kufanya jitihada zozote.
Wakuu tunachotakiwa kujua ni kwamba mwili wa mwanadamu unatumia damu,damu husukumwa na moyo
ambao wanasayansi wanajua una nguvu fulani ya umeme ambayo huuwezesha kufanya shughuli zake vizuri,
umeme huu unapoingiliwa na umeme mwingine kutoka nje huusababishia kufanya kazi bila mpangilio
na wakati mwingine husimama na kusababisha damu kushindwa kufikia sehemu muhimu za mwili
na hii inaweza kusababisha kifo kama huyo mgonjwa yuko mbali na daktari anayejua afanye nini ili kumuokoa.
Madaktari wanajua wanapoletewa mgonjwa aliyepigwa na umeme hata kama anaonyesha anaendelea vizuri kuna kipimo wanamfanyia kuhakikisha moyo wake upo vizuri kimapigo/normal operation.
Mimi nadhani kwa kuwa jf ni uwanja wa kuhabarishana,na tumepata mengi humu ni vema unapopata uzi wenye
lengo la kuleta taarifa,tuulize maswali mleta uzi atujibu,tuboreshe pale tunapoona tuna taarifa nzuri zaidi ili mwisho tunufaike sote.
Mambo ya afya ni tofauti na siasa,hapa hakuna ushabiki maana kila mtu anatakiwa kuwa na afya njema tuendelee na maisha.Niseme sisi kazini kwetu kwenye safety procedure ni marufuku kupokea simu ikiwa kwenye charge kwa sababu ya kuepuka madhara aliyoyasema mleta uzi.
Kwa wanaoendelea kuenzi mazoea,endeleeni mpaka hapo ndugu zenu watakapoleta ushuhuda wa marehemu humu jukwaani,kwa wapenda mafundisho ni vema hili ukaliongeza kwenye mambo mapya unayojifunza
asanteni.
Simu haipokei umeme direct kutoka kwenye soketi. charger ndio inapokea umeme na kuupoza kulingana na mahitaji ya simu kisha huingia kwenye simu

Simu inahitaji umeme wenye nguvu kidogo sana na hauwezi kuleta madhara kwa binadamu

Hata ukikata waya unaotoka kwenye charger kwenda kwenye simu na uuguse huwezi kuhisi chochote labda urambe na ulimi ndio utahisi kitu

kwa umeme huu kuua mtu ni hadthi za abunuwasi
na hata kama charger itapitisha moto zaidi basi simu itaunguza fuse immediately

kwa ufupi hakuna kitu kama hicho
 
Simu haipokei umeme direct kutoka kwenye soketi. charger ndio inapokea umeme na kuupoza kulingana na mahitaji ya simu kisha huingia kwenye simu

Simu inahitaji umeme wenye nguvu kidogo sana na hauwezi kuleta madhara kwa binadamu

Hata ukikata waya unaotoka kwenye charger kwenda kwenye simu na uuguse huwezi kuhisi chochote labda urambe na ulimi ndio utahisi kitu

kwa umeme huu kuua mtu ni hadthi za abunuwasi
na hata kama charger itapitisha moto zaidi basi simu itaunguza fuse immediately

kwa ufupi hakuna kitu kama hicho
Mkuu sina cha kuongeza,kama naongea na mtu anayetest umeme kwa kulamba,hata kama ni mdogo kiasi gani
hapo nakubali yaishe!ila nakushauri tafuta taarifa zaidi ili ujihabarishe kuhusu umeme na usalama wa mwili wako.
Kama haitakusaidia wewe basi itawasaidia watoto au jamaa zako wengine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom