Usiombee kukosa hela

Usiombee kukosa hela

Duh...watu na vilimo vyenu ..kuna kijana kanifata juzi ananishawishi tulime ..amenipgia hesabu weee...mie kilimo nimestaafu...ila nnashawishika mno mno kulima katani...bado natake note...all the best..unalima nn?
Mwaka jana ilikuwa mpunga nililimia mbeya Usangu, mwaka huu nipo na mahindi, naona Pm yako umeifunga
 
Nashangaa Sana huu Uzi nimepitia tokea nacheki mech ya Simba mpk saa hv ila Hakuna at mwanamke mmoja amaekoment wamekausha tu utadhani kuwawai huwa hawaishiwi
 
Umenikumbusha mwaka 2006 kipindi nipo shule.Nilikua nimepanga geto nikaishiwa kila kitu na mfukoni sina ata mia mbovu na mama ndo anaumwa pakupata pesa ya matumizi sina. Nikawa nakula kwa wana ikafikia kipindi wakanichoka nikaamua kujiongeza usiku nikawa naenda kwenye mashamba ya watu naiba mkungu wa ndizi napeleka geto napika ndizi nane kila siku.namshukuru Mungu mama alipona akantumia pesa.

Nyingine nakumbuka mwaka 2009 nilivo telekezwa shule uganda.shule wakaamua kuninyanganya vitu vyangu na kunizuia kuingia darasani na Kula mpaka nilipe ada bahati nzuri ulikua msimu wa maembe na mafenesi nikawa najiongeza usiku naruka ukuta naenda kuiba maembe na mafenesi kwenye mashamba ya watu nakula ndio kilikua chakula changu mwezi mzima mpaka nikawa nikitoa ushuzi unatoka unaharufu ya maembe mchanganyiko na mafenesi.Nikaamua kutoroka saa sita usiku nikatembea kwa miguu mpaka saa nane mchana ndo nafika kampala nikanunua mkate wa buku nikaula siku tatu mpaka nafika mwanza but sasaivi namshukuru Mungu maisha si haba wazazi wangu na madogo wanakula maisha.
 
Afadhali yako huna familia

Mimi dogo amerudishwa school kisa nimeshidwa kulipa 8000 ya uji

Na mvua ndio zinanyesha hatari, dogo viatu vimechanika maji yanaingia mpaka ndani
,
Nikaenda kukopa vibuti vya kavaa dogo awe anavaa aende navyo shule, yule mama ananidai utazan amenikopesha moyo daily hodi haziishi
Dah pole mkuu
 
Alipoingia Hayati wa Africa ike sekeseke la vyeti bas mume wangu akasimamishwa kazi...ikaonekama cheti cha form 4 jina la kati kati likawa tofaut na cheti cha chuo...wakamsimamisha bila payment kwa 3mths..alidata..mie skudata...bas nikajikuta naenda mawenzi nikanunua matunda meengi embe ng'ong'o zile nilinunua kama za 9000.nikazitengeneza juic...asbh nikaenda nayo juic job...bas haikukaa hata masaa ikaisha..bas ikawa ndo kaz yangu jaman Mungu alinishika mkono niliuza juic bila aibu..yaan nikawa napata shiling kwa shiling ..yaan hom narudi na faida nene...wakawa wanaishobokea balaa! Lakin mwenzang alijikunyataaa....nilimtoa balaa....ila nyir mna aibuu..sijui tu
Mume wako inabidi amshukuru Mungu kila siku kwa kumpa mke kama wewe
 
Nnakumbuka enzi nimemaliza chuo nnapiga deiwaka K.koo, aloo kuna siku inakata hujapata hata mia na unatakiwa ule na kupanda daladala, eti leo nnakula msosi sahani buku 5 na nnaona kawaida? Mungu nikumbushe kukushukuru
 
Back
Top Bottom