Saint_Mwakyoma
JF-Expert Member
- Jun 8, 2019
- 865
- 1,204
Jana nilikutana na fundisho kubwa sana kwenye maisha yangu baada ya kukutana na mzee wa bodaboda aliyenipa ushauri mzito utasema alitumwa na Mungu juu yangu.
Mwakyoma: Mzee umemuona yule dada aliye nisindikiza vizuri
Mzee wa boda: Ndio nimemuona , vipi ndio mkeo
Mwakyoma: Hapana , ni mtoto wa mwenye nyumba hapo nilipopanga , kiukweli ni mwanamke mwenye kila kitu chema ila najiuliza sana kivipi huyo mwanaume wake aliamua kumuacha na kumsusa mtoto wao
Mzee wa boda: Ha ha ha, wewe ina maana hujui mpaka leo siri ya ndoa
Mwakyoma: Inawezekana sijui
Mzee wa boda : Mwanamke anaweza kua na tabia zote nzuri na utu kwa asilimia mia, wewe ukatokea kumpenda sana ila kumbuka na yeye anahisia kama wewe za kumpenda mtu ukitoa tabia zote nzuri unamuona nazo
Mwakyoma : Mmmmh , sijaelewa vizuri hapo
Mzee wa boda: Mwanamke anaweza akampenda mwanaume kwa roho yake yote, na wakati huo anajua kabisa huyo mwanaume kamwe hawezi kumfanya yeye kuwa mke wake wala kufanya maisha pamoja nae lakini bado akampenda hivyo hivyo.
Mwakyoma: Sasa kwa nini wanafanya hivyo
Mzee wa boda: Kwasababu hayo ndio mapenzi , kumpenda mtu bila sababu yoyote yani unajikuta unampenda tu lakini hayo yote hubadilika pindi anapotokea mtu kama wewe ambae anavutiwa na tabia za binti na kutangaza ndoa
Mwakyoma: Kwaio wanao tangazaga ndoa wengi wao wanakosea
Mzee wa boda: Ndio , wengi wao wanakosea hata mimi nilikosea angalia vidole vyangu siunaona nimevaa pete kidole cha kati hiyo ni pete ya ndoa ambayo imenifanya mpaka leo nimekua dereva bodaboda na umri wangu huu
Mwakyoma: Mzee pole sana nini kilitokea
Mzee wa boda: Nilikua kijana wa rika lako kipindi hicho nina mali za urithi na biashara zikienda poa huko mkoani , nikavutiwa na mwanamke mwenye tabia nzuri kama hizi ulizolua unasifia yule dada niliekukuta nae, nikamueleza lengo langu la kutaka kumuoa na akaniambia nisubilie jibu baada ya kama mwezi alikuja kukubali na nikamuoa
Mwakyoma: Aise! Mzee ulipenda
Mzee wa boda: Ndio nilipenda sana , mwanzoni tuliishi vizuri sana , yeye akiwa mwajiliwa wa serikali mimi nikiwa na biashara zangu mengine nimazito nikikuelezea mwanangu lakini nilishindwa kuvumilia niliyokua nafanyiwa siku moja nikaamua kukaa pembeni naapa !! Siku chukua mwezi maduka yangu ya kumla na store ziliwaka moto mala magari ya nock engine nk
Mwakyoma: duuuu! Sasa nani alikua anafanya hivyo
Mzee wa boda: Hahahaha , ni yeye mwanangu mwanamke asiyekupenda ni sumu hata kama anatabia nzuri hizo tabia ni kwajili ya watu wote lakini mapenzi ni kwa mtu special ampendae kama wewe si huyo ampendae ni bora utulie tu kamwe hutamuona mbaya.
Mwakyoma: Kwaio inawezekana huko kwa mwanaume wake alizingua ndio maana karudi pale kwao na mwanake
Mzee wa boda: Haha siwezi jua lakini nakwambia hili asikudanganye mtu kama unataka kuona dunia nzuri oa mwanamke anaekupenda na usiniulize utajuaje kama anakupenda , mwanamke anayekupenda hato tafuta kigezo cha kukupenda ni atakupenda tu!! Uwe na ulemavu ,mfupi, kichaaa, masikini choka, tajiri ,uwe na elimu uwe hauna yani hakuna kigezo atakiangalia ili akupende kila siku atakua anakuona mpya mala zote
Mwakyoma : Mzee nashuka hapo kwenye kibanda daaa! Asante kwa kuniosha macho mkuu
Mzee wa boda: Usiwaze sana ,ila maneno yangu yakumbuke sana maana huwa mimi sio muongeaji sana ila leo sijui nini Mungu kanipa nikwambie.
Wakuu naomba kuwasilisha 🙏🏿
Mwakyoma: Mzee umemuona yule dada aliye nisindikiza vizuri
Mzee wa boda: Ndio nimemuona , vipi ndio mkeo
Mwakyoma: Hapana , ni mtoto wa mwenye nyumba hapo nilipopanga , kiukweli ni mwanamke mwenye kila kitu chema ila najiuliza sana kivipi huyo mwanaume wake aliamua kumuacha na kumsusa mtoto wao
Mzee wa boda: Ha ha ha, wewe ina maana hujui mpaka leo siri ya ndoa
Mwakyoma: Inawezekana sijui
Mzee wa boda : Mwanamke anaweza kua na tabia zote nzuri na utu kwa asilimia mia, wewe ukatokea kumpenda sana ila kumbuka na yeye anahisia kama wewe za kumpenda mtu ukitoa tabia zote nzuri unamuona nazo
Mwakyoma : Mmmmh , sijaelewa vizuri hapo
Mzee wa boda: Mwanamke anaweza akampenda mwanaume kwa roho yake yote, na wakati huo anajua kabisa huyo mwanaume kamwe hawezi kumfanya yeye kuwa mke wake wala kufanya maisha pamoja nae lakini bado akampenda hivyo hivyo.
Mwakyoma: Sasa kwa nini wanafanya hivyo
Mzee wa boda: Kwasababu hayo ndio mapenzi , kumpenda mtu bila sababu yoyote yani unajikuta unampenda tu lakini hayo yote hubadilika pindi anapotokea mtu kama wewe ambae anavutiwa na tabia za binti na kutangaza ndoa
Mwakyoma: Kwaio wanao tangazaga ndoa wengi wao wanakosea
Mzee wa boda: Ndio , wengi wao wanakosea hata mimi nilikosea angalia vidole vyangu siunaona nimevaa pete kidole cha kati hiyo ni pete ya ndoa ambayo imenifanya mpaka leo nimekua dereva bodaboda na umri wangu huu
Mwakyoma: Mzee pole sana nini kilitokea
Mzee wa boda: Nilikua kijana wa rika lako kipindi hicho nina mali za urithi na biashara zikienda poa huko mkoani , nikavutiwa na mwanamke mwenye tabia nzuri kama hizi ulizolua unasifia yule dada niliekukuta nae, nikamueleza lengo langu la kutaka kumuoa na akaniambia nisubilie jibu baada ya kama mwezi alikuja kukubali na nikamuoa
Mwakyoma: Aise! Mzee ulipenda
Mzee wa boda: Ndio nilipenda sana , mwanzoni tuliishi vizuri sana , yeye akiwa mwajiliwa wa serikali mimi nikiwa na biashara zangu mengine nimazito nikikuelezea mwanangu lakini nilishindwa kuvumilia niliyokua nafanyiwa siku moja nikaamua kukaa pembeni naapa !! Siku chukua mwezi maduka yangu ya kumla na store ziliwaka moto mala magari ya nock engine nk
Mwakyoma: duuuu! Sasa nani alikua anafanya hivyo
Mzee wa boda: Hahahaha , ni yeye mwanangu mwanamke asiyekupenda ni sumu hata kama anatabia nzuri hizo tabia ni kwajili ya watu wote lakini mapenzi ni kwa mtu special ampendae kama wewe si huyo ampendae ni bora utulie tu kamwe hutamuona mbaya.
Mwakyoma: Kwaio inawezekana huko kwa mwanaume wake alizingua ndio maana karudi pale kwao na mwanake
Mzee wa boda: Haha siwezi jua lakini nakwambia hili asikudanganye mtu kama unataka kuona dunia nzuri oa mwanamke anaekupenda na usiniulize utajuaje kama anakupenda , mwanamke anayekupenda hato tafuta kigezo cha kukupenda ni atakupenda tu!! Uwe na ulemavu ,mfupi, kichaaa, masikini choka, tajiri ,uwe na elimu uwe hauna yani hakuna kigezo atakiangalia ili akupende kila siku atakua anakuona mpya mala zote
Mwakyoma : Mzee nashuka hapo kwenye kibanda daaa! Asante kwa kuniosha macho mkuu
Mzee wa boda: Usiwaze sana ,ila maneno yangu yakumbuke sana maana huwa mimi sio muongeaji sana ila leo sijui nini Mungu kanipa nikwambie.
Wakuu naomba kuwasilisha 🙏🏿