Usimvue nguo mume wako

Usimvue nguo mume wako

Ubishi mwingi matokeo yake ni ndoa kutokudumu. Hali ya sasa hivi ya uimara wa ndoa ni mbaya sana kwa sababu ya mitandao. Tunaanika mahusiano ya ndani ya chumba kwenye mitandao ya kijamii. Na humu JF kuna bandiko kadhaa zinazohusu hayo mambo ya ndani. Na imefikia hata kuweka picha.

Tuombe maadili mema ili kudumisha furaha ya ndoa na mahusiano
Aminaaaaaa.. Hallelujah!!!


Mahondaw wa Smart911
 
Wasichana wengi sana kabla ya ndoa uitamani sana na hata kwa maombi, ila wakiishapata tu uanza kuibomoa, na hasa wakishapata vyeti au watoto, uanza kujiinua kiburi, lawama, kutopenda ndugu za mume, wivu na chokochoko tele, mwanaume yakimshinda na kuikimbia nyumba uanza kulilia tena kwenye nyumba za ibada na kwa waganga wa kienyeji, kulilia kuirudisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Abarikiwe huyu mzazi kwa kweli

You get what you work for not What you wish for
 
Back
Top Bottom