Usiku wa manane

Usiku wa manane

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286

usiku.jpg
1.
Masaa kumi na mbili, toka jua la utosi,
Tena upate kandili, sidhani utusitusi,
Kiza chake si kalili, nyakati za wasiwasi,
Chukua udhu uswali, kwa mola wako Qudusi.
Usiku wa manane, ni usiku wa shari.
2.
Nyakati yake zohali, visoke hupanda rasi,
Wanga hufanya shughuli, kutia watu nuhusi,
Usiku una makali, nadhani kama makasi,
Niwache nifanye fali, kwalo niite farisi,
Usiku wa manane, ni usiku wa shari.
3.
Jambazi huiba mali, wakiipata nafasi,
Usingizini u mbali, ati wapiga gambusi,
Kumbe umelala chali, waibiwa kirahisi,
Lala yako afadhali, upone yake risasi,
Usiku wa manane, ni usiku wa shari.

Dotto Chamchua Rangimoto(Njano5)
0762845394/0784845394
Mzalendo.njano5@gmail.com
Morogoro Tanzania
 
Ni usiku wa manane.
Tena wenye giza nene.
Wembamba hadi wanene.
Waloshiba kwa senene.
Tena tusimuliane.
Hadi siku za manene.
Vyema sana tujuane.
Tungo tusimuliane.
Mikataba tuichane.
Na wala tusigombane.
Na mchana wa sanane.
Kwa masiku yalingane
.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom