Ushuhuda: Nilikimbia Ualimu Kuepuka Matatizo

Hao wanaosema kuna walimu wana mafanikio wasome hapa:

Kuna jamaa yupo huku Mbezi Beach ni mwalimu, huyu bwana mara ya kwanza kuonana nae nilifiikiri ni mtu mwenye wadhifa mkubwa sana kwenye Taasisi fulani. Ni muhudhuriaji mzuri wa vikao vya jioni na ni mzungushaji mzuri wa round, gari zuri (Mark II grand). Hali hii ilinifanya nitake kuwa karibu naye ndipo nilipobaini kuwa ni mwalimu wa shule moja ya Serikali iliyopo katikati ya jiji.

Huyu bwana ni Graduate, ukitoa shule yake hiyo anafundisha shule nyingine mbili binafsi, hapo hapo anaduka kubwa tu la kuuza bidhaa za jumla karibu kabisa na sehemu tunayokaa vikao vyetu.

Sasa naomba mnisaidie, kama ualimu ni kuandaa somo la kesho yake ukiwa sehemu tulivu, azimio, andalio la somo na masuala mengine ambayo walimu nafikiri wanaelewa zaidi, Je huyu mtaalamu wetu anayafanya hayo sasa ngapi? Je vipi kuhusu ufanisi wake darasani?
 
Kwani umeambiwa mtu kujua chuo ndo kufanikiwa katika maisha?
KUJUA CHUO SIO KUFANIKIWA HILI LIKO WAZI KABISA MKUU,VIVYO HIVYO KUKIMBIA UALIMU SIO KUWA NA MAISHA MAZURI KWA SABABU NI WATU WANGAPI WAMESOMA Bcom na KOZI ZINAZOENDANA NA HIZO NA WANASOTA TU MTAANI NA MWISHOWE UKIMBILIA KUOMBA TEMPO ZA KUFUNDISHA MASHULENI NA HIVYO BASI KUWA NA MAISHA MAZURI NI AKILI ZA MTU NA HAIJALISHI ANAFANYA KAZI GANI......WADAU HAKUNA MAFANIKIO HALALI UTAKAYOYAPATA KWA HARAKA LAZIMA UTAPITIA MAGUMU MENGI.
 
Kwani umeambiwa mtu kujua chuo ndo kufanikiwa katika maisha?

Mpwa una visa wewe....hapa hatuzungumzii kila mtu, tunazungumzia walimu Mpwa....nipe mfano wa Mwalimu gani amebaki akafundisha kwa moyo wote huku ana mafanikio? Nimekupa mfano wa Walimu ambao wamefanikiwa but walikua hawa-attend vipindi kama inavyotakiwa kwasababu muda mwingi wa deal na biashara zao.....hebu na wewe nifundishe hao unaowafahamu wewe waliwezaje? Mimi salary yangu wakati naanza hio kazi Take Home ilikua around Tshs. 372,000/= na huu ni mshahara wa graduate, sasa hebu nipigie bajeti Mpwa....ukifanya maiak kama kumi ndio utafikisha kama laki nane au milioni pengine....huna overtime, huna house allowance, una meical ya kizushi zushi tu, huna transport allowance....No Mpwa kuwa mkweli wa roho yako tusiendekeze malumbano bhana
 
Hii taaaluma imedharauliwa sana na kwa muda mrefu, ni wakati sasa wa waalimu kufanya maamuzi magumu. Alichoeleza Elii ndio hali halisi ya walimu na mazingira yao ya kazi. Pole sana kaka, mdogo wangu yuko mwaka wa kwanza pale DUCE ualimu kweli kabugi.
 
Asante kwa kunielewa vyema Mpwa wangu, it is high time maamuzi magumu yachukuliwe
Hii taaaluma imedharauliwa sana na kwa muda mrefu, ni wakati sasa wa waalimu kufanya maamuzi magumu. Alichoeleza Elii ndio hali halisi ya walimu na mazingira yao ya kazi. Pole sana kaka, mdogo wangu yuko mwaka wa kwanza pale DUCE ualimu kweli kabugi.
 
mpwa Elli nilivyomaliza form 6 niliomba UD tukafanya mtihani wa chuo nika'apply na diploma ya ualimu matokeo ya diploma yalitoka mapema kabla ya yale ya chuo nimechaguliwa TTC Korogwe kwa masomo ya Geography na Mathematics (GM),
wiki iliyofuata yakatoka ya chuo UDSM nimechaguliwa Architecture miaka mitano, kwa wakati ule wa mheshimiwa sana mkapa walimu walikuwa ndo wenye hela vijijini nilijishauri sana kusoma ualimu lakini mmmh!, bora si kwenda ualimu.
 
Last edited by a moderator:
kwa lugha ya akina Mulugo tunasema hivi; Good, Gooder, Goodest...mosie uwedi mia
mpwa Elli nilivyomaliza form 6 niliomba UD tukafanya mtihani wa chuo nika'apply na diploma ya ualimu matokeo ya diploma yalitoka mapema kabla ya yale ya chuo nimechaguliwa TTC Korogwe kwa masomo ya Geography na Mathematics (GM),
wiki iliyofuata yakatoka ya chuo UDSM nimechaguliwa Architecture miaka mitano, kwa wakati ule wa mheshimiwa sana mkapa walimu walikuwa ndo wenye hela vijijini nilijishauri sana kusoma ualimu lakini mmmh!, bora si kwenda ualimu.
 
Mpwa mwalimu mwenzio Mohamedi Mtoi yupo online hapo namuona,
mia nyiao ye amjini kabisa, sio iwe wiighaewo tundui, nyiao ataja mzi haona sungu kufuza wenetu.
mosie mtoi hongea kwa ndima yakufuza wenetu.
 
Last edited by a moderator:
kuendelea kufanya kazi ya ualimu tanzania unahitaji hopeless mind, vinginevyo ukiwa timamu unaacha ndani ya wiki.
 
Mosie mueke aje nguku zakwe iwe.....atakua hapo Tanga mjini hapo anakula Uono Bonge na Vibua tu kwa kwenda mbele......
Mpwa mwalimu mwenzio Mohamedi Mtoi yupo online hapo namuona,
mia nyiao ye amjini kabisa, sio iwe wiighaewo tundui, nyiao ataja mzi haona sungu kufuza wenetu.
mosie mtoi hongea kwa ndima yakufuza wenetu.
 
Mpwa hilo jina lako na hio comment yako pia vinahtihaji the same mind kuelewa....kha Mpwa una visa weye haya bhana tumekuelewa
kuendelea kufanya kazi ya ualimu tanzania unahitaji hopeless mind, vinginevyo ukiwa timamu unaacha ndani ya wiki.
 
mpwa Elli nilivyomaliza form 6 niliomba UD tukafanya mtihani wa chuo nika'apply na diploma ya ualimu matokeo ya diploma yalitoka mapema kabla ya yale ya chuo nimechaguliwa TTC Korogwe kwa masomo ya Geography na Mathematics (GM),
wiki iliyofuata yakatoka ya chuo UDSM nimechaguliwa Architecture miaka mitano, kwa wakati ule wa mheshimiwa sana mkapa walimu walikuwa ndo wenye hela vijijini nilijishauri sana kusoma ualimu lakini mmmh!, bora si kwenda ualimu.

Wakuu Elli na zumbemkuu.

Nawauzieni siri! Kazi nzuri niya mwenzako, na jitihada zako ndio zitakutoa.

Uzuri wote Elli na zumbemkuu) kwa kuwa mnatokea Lushoto mtakuwa mna mfahamu vizuri Mwalimu Soka, mwalimu Soka alikuwa anakaa Chakechake akifundisha Kitopeni mimi nikiwa bwana mdogo (Chabebi) nikisoma Hazina (Lushoto Primary kwa sasa). Nilisoma tuition kwake, alikuwa anachacharika kwenye kila aina ya kitu kinachoita kuingiza pesa! Leo Mwl Soka yuko kwenye mitumba kesho yuko kwenye Mbao, leo amefungua Glossary anauza bia, mara kesho amekuwa wakala wa bia wilaya ya Lushoto, mara anafuga yale madubwana ambayo nikiyaona lazima nipige Astakafuli! Mara anakusanya mahindi na kuuza. Yaani alikuwa na jitihada na vurugu za kutafuta! Alithubutu!

Leo mwalimu Soka ni miongoni mwa matajiri wakubwa pale Lushoto! Kwa taarifa yenu nilikutana naye miaka kama 3 iliyopita bado alikuwa anapigisha chaki kama kawaida! Kumbukeni, hakuwa akifundisha sekondari na wala hakuwa na elimu kubwa ya kiwango cha shahada kama chenu Elli na zumbemkuu).

Mwingine yuko Handeni maarufu sana kwa jina la TEACHER, nilikutana naye Mkuzi akitokea Kwemakame nilikuwa nasubiria gari hadi Lushoto mjini kisha nikamate zangu Coaster hadi Mkoa (Tanga), nikapiga mkono gari yake akasimama. Akuliza "Ndio kaka nikusaidie nini ndugu yangu"? Nikamuambia "Samahani Bro, naenda Lushoto naomba unisaidie lift nimesubiria gari muda mrefu hapa naona haziji" akaniambia "Usijali panda twende ndugu yangu". Ndani ya gari (Pajero short chases) alikuwa yeye na jamaa mwingine lakini nyuma kulikuwa na mifuko kama 4 ya unga kilo 20.

Nilikuwa kimya kwenye gari kwa muda kidogo nikiwaza jinsi mama alivyo nihadisia kabla sijaondoka kuhusu kuhusu kumlipia karo mtoto wa dada yangu mmoja ambaye baba yake aliapa kuto kumsaidia, na alikuwa kafaulu shule ya UKATA (kata).
Ghafla jamaa akaniiuliza, huku ndio kwenu? Nikamjibu ndio, unaishi huku? Nikamuambia hapana niko Tanga, oh! Unakwenda Tanga?... Mimi naenda Handeni unaonaje nikikuacha Korogwe?! Nikamuambia haitakuwa vibaya.

Akaiambia itabidi uvumilie maana itakuwa na mazungumzo na watu fulani Lushoto mjini, Soni, na Mombo.

Tulipo fika Magamba akanunua Matunda ghafla ikaja Fuso moja akaitwa na jamaa mmoja "Teacher, teacher" kumbe yule bwana ni mwalimu. Baadae nikawa interested kuumuliza.

Kumbe Bro wewe ni Mwalimu?!

" Mimi ni mwalimu kaka mwaka takribani wa kumi na tisa huu, niko Handeni" Nikaendelea kumdadisi, "mbali na ualimu najishughulisha sana na kilimo na biashara, kwa sasa nalima sana nina hekari kama 1500 na nina mashine za kusaga".

Kumbe jamaa alikuwa anatokea Kwemakame na Mlola kutafuta wateja wa jumlajumla awe ana wauzia unga wa sembe, unao sagwa na mashine zake na offcourse unao tokana na mahindi anayo vuna mwenyewe.

Elli na zumbemkuu, siku moja niko Korogwe nikamuona tena Teacher tukasalimiana. Kuna jamaa akaniambia "Oyaa unajuana na huyo fogo?!... Jamaa ana vyuma (hela) hapo Handeni huwa anaikopesha mpaka Halmashauri" Nikaona jamaa ananipiga fix tu! Nikajiuliza akopeshe Halmashauri?!

Ukweli ni kwamba jamaa ana vyuma vya kufa mtu!

Kwa maelezo na mifano hiyo michache hapo juu! Nimejifunza kuwa juhudi ndio zinaweza kukutoa! Kuwa na kazi nzuri sio kipimo pekee cha kukutoa kimaisha!

Nani alikuwa na vyuma kama Salimu Matagi?! Nani walikuwa na vyuma kama kina Kusaga?!

Jamaa yangu mmoja, ni mwalimu, ana hekari 15 za michungwa Muheza, kwa wastani kila mwaka anakunja Milioni 10. Life goes on!

Wakati mwingine hata House gal anaweza kutoka kimaisha kuliko baba mwenye nyumba, what matters ni mindset. Hahahaha.
 
Last edited by a moderator:
Mohamedi Mtoi shiiiii!
eka kuongesha osie, said matagi hasomie, hata ali bucha hana shule, eka matei mwena mbaruku na abasi ya shambali, bado simtajizie alphani kagogo wa umba.
osie walimu enzi za mwalimu mwenyewe na enzi za mwinyi na mkapa ndo mafogo, aliyekuja kuharibu sifa ya ualimu ni JK, Mohamedi Mtoi pia mimi nimefundisha shule ya BAKWATA Jitengeni ipo Kihurio same (wakati huo nasubiri matokeo ya chuo,nalipwa elfu 40), najua ugumu wa hiyo kazi, ila usiombe kukutana na walimu wa shule za UKATA (kata) waliopangwa huko kwenye vijiji vyetu tunavyovijua Singida au Shinyanga, acha kuuliza habari za Lushoto, popote na kijiji chochote utakachopangwa ni kama umepelekwa Ulaya,
hapa tunaongelea majority ya walimu waliotelekezwa huko kwenye vijiji vileeeeeeeee, huko hata uwe na juhudi binafsi vipi hutoki NG'OOOOOOO, osie eka kabisa kuonga.
 
Last edited by a moderator:
Chabebi ulichosema ni ukwelio mtupu but kuna ukweli mwingine tuuuweke sawa japo kwa ufupi, ukiangali watu kama hawa Ualimu kwao hua kama kivuli tu, Huyu Soka namfahamu vyema maana si tulikua wote Kaka, kumbuka kwamba alikua anauza vipindi kw Walimu na kama utakumbuka alikumbwa hadi na kashfa na Mwalimu Mkuu Mama Chalamila kua jamaa alikau hafundishi na muda mwingi yuko kwenye biashara zake, the same kwa huyu Fogo wa handeni, kama muda huo yuko Mkuzi (nakufahamu vizuri sana) hebu nambie atafundisha saa ngapi na andaliao ataliandaa sa ngapi? mimi hichoi ndio ambacho sijakipenda kuwadanganya watoto ili nije kubeba laana zao baada ya wao kufeli NO NO siwezi kubeba laana ya mtu ial kama ni usaniii ningeweza kuufanya sana sana mohamed mtoi

Unamkumbuka Mwalimu Kanyawana ambaye wewe mwenyewe wakati tuko form Two pale Shambalai ulimpa jina la Bab Langu hebu nambie na yeye alikua na ualimu gani? si baada ya kuingia SACCOSS ya walimu ndio alikoibukia? Mwalimu Kiangi je? mmmhhh no no teeka niishie hahahaaaaa but ukweli ni kwamba ukitaka kuwa mwalimu mkweli basi kwa Bongo sahau
 
Elli nami ni mhanga wa udhalilishaji wa taaluma ya Ualimu inaofanyiwa. Nasikitika sana leo hii sifundishi, hata baada ya kusoma Ualimu 7yrs. Ni kati ya swala linaloniumiza sana kila siku, kwani taaluma hii naipenda, na ninajua thamani yake. Tatizo ni changamoto ulizoeleza hapo juu.
 
Kwani umeambiwa mtu kujua chuo ndo kufanikiwa katika maisha?
Mkuu Saudari hii ndiyo sababu huwa napenda sana kupitia mada zako. Ni mtu unayechambua vitu kwa undani sana pasipo kukurupuka kiushabiki kama wengine humu ndani wanavyofanya.

Naunga mkono swali lako zaidi ya 100%.
 
Tumekusanyika wote, tumependeza kweli, ni kozi mbalimbali na tumetengwa vivyo hivyo!! Mimi nahitimu kozi ya Elimu ya Watu wazima (Bachelor of Education in Adult Education) ni furaha kweli. Ila kuna kitu kinaniumiza sana kila nikikumbuka shule niliyopangiwa.

Kweli hii si shule bali ni majengo tu, hayana madirisha mazuri, sakafu chafu, imetoboka toboka! Nashindwa kufundisha kutoka na vumbi lile, ubao wa kufundishia haueleweki, ofisini sina hata rula, inabidi nijinunulie kalamu! Lakini mbaya zaidi ni hawa wafuatao; wanafunzi wawili wenye ulemavu wa viungo, inabidi wakae chini pale mbele maana hawawezi kukaa kwene madawati na pia baskeli zao hazipiti kwene milango ya madarasa. La pili, wanafunzi wangu wanaonekana kukata tamaa ya maisha kabisa na kila ninavyojaribu kuwaelimisha hawaonekani kabisa kunielewa. Wanauliza maswali magumu kuliko uwezo wa kuyajibu, hawana maabara hata moja, kuna gunia moja na box ambalo tumehifadhia mifano ya test tube, spatula na n.k

Walimu wenzangu nao wanaonekana wamefika mwisho wa maisha yao, ni walevi wa kutupwa (si walaumu) na nguo zao zinaonyesha fadhaiko kubwa na kukata tamaa kwa hali ya juu, ni kilio kikubwa. Niko kwene nyumba ya kupanga, naonekana kama ndio mungu wao, mwenyewe nimepigika!

Siku moja niakenda Halmashauri kufuatilia madai yangu, nilichokikuta ilikua ni pigo jingine, kauli za wahasibu wale zilinikatisha tamaa sana sana, ni kauli zilizojaa jeuri na kiburi, mbaya zaidi namuona kijana mmoja ambae tulimaliza mwaka mmoja kwa kozi tofauti (Accounts) ni mmoja wa wahasibu/cashier wa pale, yeye anapendeza jamani si haba hakuna ulinganisho wa mimi na yeye kwa namna yoyote ile. Naelekea kwene ofisi za TSD huko nako nakuta kituko majibu ya hovyo sana, roho inauma sana.

Ninaporudi jioni nimechoka sana maana hata basi la kurudia kwangu nililikosa na hivyo kupanda Landrover, nimejaa vumbi sana, nimechoka na kesho natakiwa tena niwepo darasani nifundishe wanafunzi wangu!!! Usiku ule unakuwa usiku wa maumivu makali sana kwangu, nikijiuliza kuwa kwanini nilifanya chaguo baya? Maana nilifaulu kwa kiwango cha Division One point Seven kwa form six.

Asubuhi naamua kuongea na wanafunzi wangu badala ya kufundisha tu kila siku, tunabadilishana mawazo, maana si mwalimu wala si wanafunzi wanaoneka wana ari ya kusoma tena!!!!! Nawauliza, ni wapi alipo Asha Amiri? wanacheka na mmoja anasimama na kuongea kwa kejeli, "ameshaolewa, yaani mwalimu huna habari?"

Ni jioni sasa, nipo nje pale nyumbani, wanakijiji wanaendelea na shughuli zao, huyu anachota maji hawa wanarudi machungani, nina kiredio kidogo nasikiliza nisichokielewa! Maana hakika mawazo yangu yako mbali sana, ile degree haina maana tena, sina wa kumfundish maarifa yale! Naonekana kituko pale kijijini kwa kutaka kuwafundisha watoto wale!!! Ghafla, napata ujasiri wa ajabu, yes ujasiri wa ajabu sana. NIMEAMUA KUACHA KAZI. Kesho ni ijumaa kwahio nitaomba neinde mjini mara moja lakini hapo ndipo mwisho wa kukaa hapa.

Narudi mjini na kuamua kaunza maisha ya tofauti sana na kujaribu kuisahau ndoto ile kwamba ningekuwa Mwalimu mzuri, nimeachana na vituko vya kukatwa pesa ya MWENGE kwa ajili ya kufungua miradi ya watu binafsi, nimeachana na maumivu yale ya kudharauliwa na watumishi wenzangu walioko halmashauri, sijawahi pia kukaa nikafahamu mshahara wangu ni shilingi ngapi hasa, maana kila siku unabadilika kwene payslip.

Walimu wana haki sawa na watumishi wengine, tuwapende, tuwajali na tuwatunze!!!

Mwalimu Elli

Kama kamati ya Pinda ina peruzi mtandao kidogo, nadhani wasomapo ujumbe huu, wahitimishe task waliyopewa kubaini chanzo cha wadogo wetu kufeli. Wafanyie kazi hili.
Story yako inagusa hisia kwa kiwango cha juu.
 
Maskini wa Mungu hawana huo muda....watakaaa mahali watajiandikia wanachokfahamu wao wenyewe
Kama kamati ya Pinda ina peruzi mtandao kidogo, nadhani wasomapo ujumbe huu, wahitimishe task waliyopewa kubaini chanzo cha wadogo wetu kufeli. Wafanyie kazi hili.
Story yako inagusa hisia kwa kiwango cha juu.
 
Mpwa wangu...huu unaoitwa Ukweli Unaouma....tuukubali au tuukatae japo unauma but unabakia kuwa ukweli mchungu kwetu sote pamoja na vionjo na vidokezo vyovyote vile tutakavyoviweka ukweli utabaki kuwa Taalluma ya Ualimu inadhalilishwa sana sana
Elli nami ni mhanga wa udhalilishaji wa taaluma ya Ualimu inaofanyiwa. Nasikitika sana leo hii sifundishi, hata baada ya kusoma Ualimu 7yrs. Ni kati ya swala linaloniumiza sana kila siku, kwani taaluma hii naipenda, na ninajua thamani yake. Tatizo ni changamoto ulizoeleza hapo juu.
 
Back
Top Bottom