Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 59,040
- 103,461
Mkuu uko wapi?
We mdada na wewe unaweza kufuga!!!? Mimi nadhani wewe ni wale wanaovaa viatu virefu na jeans huku wakiwa na kucha za kubandikiza. Karibu kwenye ujasiriamali.
Mkuu uko wapi?
Looh hisia zako zinakudanganya jamani.... Santeee ntakaribia muda si mrefuWe mdada na wewe unaweza kufuga!!!? Mimi nadhani wewe ni wale wanaovaa viatu virefu na jeans huku wakiwa na kucha za kubandikiza. Karibu kwenye ujasiriamali.
Umenitoa matongo-tongo katika hii industry. NitakutafutaKumekuwa na upotoshaji kwa baadhi wa watu wanaojiita wataalamu wa ujasiriamali, hasa wanaofanya shughuli za ufugaji kwa maandiko ya whatsapp bila kuwa na hata kuku mmoja bandani.
Nimesukumwa kuandika bandiko hili hapa kutokana na jumbe mbali mbali za uufugaji wa kimtandao unaoshawishi vijana kuwa watatajirika mapema kwa shughuli za ufugaji kwa kuanza na kuku wa kienyeji kumi na moja na kuweza kupata Zaidi ya kuku miatatu ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wa uzalishaji. Hoja yao inaweza kuwa sahihi, ila ningependa kusisitiza mafanikio katika ufugaji hayapo katika idadi ya kuku unayomiki, bali ni namna ulivyoweza kumanage biashara ya ufugaji.
Hoja yangu leo hapa ni kwamba, Biashara ya kuku wa kienyeji hailipi na nikupoteza muda wako. Na nitatetea hoja yangu kwa mifano hai na uzoefu wangu katika ufugaji.
Biashara ya Mayai. (idadi isiyo na tija kibiashara)
Kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji wa mayai 7-10 na mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga - siku 50-60. Hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka kwani anapoteza muda mwingi kwa shughuli za utamiaji na malezi ya vifaranga badala ya kutaga. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.
Changamoto kwenye soko la mayai ya kienyeji. (Uhifadhi wa mayai)
Mayai ya kienyeji ni kati ya bidhaa ngumu Zaidi kuhifadhika. Ikumbukwe kuwa tofauti na mayai ya kisasa, mayai ya kienyeji huwa yamerutubishwa na majogoo. Hivyo kuharibika ndani ya muda ya week moja au pungufu kama hayatatuzwa katika mazingira salama kwaajili ya utunzaji. Kipindi cha joto kali, mayai haya huanza kujitenenezea kifaranga au mishipa ya damu ambayo baada ya muda mfupi hugeuka viza na kutofaa kwa matumizi tena.
Kwa uzoefu wangu binafsi, nilianza kusambaza mayai ya kienyeji kwenye supermarkets miaka mitatu iliyopita. Nilipata changamoto kubwa sana ya kubadilisha mayai mara kwa mara kwani mteja akichukua yai viza ni kumpoteza kabisa. Hii ni changamoto ya kwanza ambayo mpaka sasa bado inasumbua wafugaji wengi.
Bei juu kwa mayai ya kienyeji
Gharama za mayai husika, bei ya mayai ya kienyeji iko juu ukilinganisha na gharama za mayai ya kuku wa kisasa. Soko kubwa la mayai ni pamoja na vibanda vya chips, migahawa na hoteli. hawa wanauhitaji mkubwa sana wa mayai na soko liko juu muda wote wa mwaka.
Soko la mayai ya kienyeji lipo Zaidi kwenye households(soko la familia) hasa kwa vigezo vya kuzingatia afya zaidi. Soko hili la familia sio kubwa, ni soko dogo na mara nyingi hutumia tray moja kwa kipindi cha wiki mbili au Zaidi. Kwa mzalishaji mkubwa wa mayai ya kienyeji ni lazma awe na soko la familia pana Zaidi kuweza kupata faida ndogo, nasema faida ndogo maana ili kuzalisha mayai tray kumi (mayai 300) kwa siku, utahitaji Zaidi ya matetea 700 mpaka 1000 ya kienyeji pure. idadi ambayo ni kubwa kuliko idadi ya mayai yanayopatikana.
Biashara ya Nyama
Na declare interest, mimi pia ni msambazaji wa nyama ya kuku wa kienyeji, hivyo naongea kwa uzoefu, na niko tayari kukosolewa. Pamoja na kufugwa katika misingi ya kijani (organic rearing), iyo pekee haitoshi kumpa thamani inayostahili huyu kuku sokoni.
Thamani ya kuku sokoni ni uzito alio nao, organic component ni jambo la ziada lililo muhimu pia. tunavyo jadili bei ya soko ya kuku huyu ni lazma tumliganishe na gharama za bidhaa pinzani zilizoko sokoni. Haitawezekana kumuuza kuku mwenye kilo moja au pungufu kwa bei ambayo tunashawishiana humu ya 15,000-20,000 wakati bidhaa pinzani (nyama nyeupe) kama samaki sato toka mwanza wanauzwakwa 7,500 kwa kilo, au kitimoto, nyama ya ngombe ambazo nazo kilo ni 7,500-8,000.
Hivyo basi, hoja yangu hapa ni uzito wa kuku husika. Ukiachana na jamii chache za kuku wa kienyeji (kuchi etc) wenye uzito mzuri, majority ya kuku pure wa asili/kienyeji kwa majogoo huwa na pungufu ya kilo moja na nusu. Kumbuka uzito wa kuku hawa sio kwasababu ya malisho duni, laah hasha, bali ni kutokana na vinasaba (genes) vyao kuwafanya kuwa na maumbo madogo madogo. kwa kuku wa aina hii, sitegemei mfugaji kama atafanikiwa kuwapeleka sokoni na kuweza kupata bei nzuri toka kwa mlaji wa mwisho.
Nini kifanyike?
Ili ufugaji uwe wenye tija kibiashara ufanyike, ni lazma wafugaji tuamke na kuachana na ufugaji wa kuku hawa asilia kwani hawana tija. Nikisema hivi simaanishi watu waache kufuga, hapana, ila wafuge aina /breeds za kuku zenye tija kibiashara. Kuku pekee unaoweza kuwafuga kwa mbinu za kienyeji na bado wakakuletea mfugaji faida nzuri kibiashara, ni kuku aina ya chotara (cross breeds). Hii ni aina ya kuku wenye sifa zote za ukienyeji kwa misingi ya mbinu zao za kuwafuga pamoja na namna walivyo nauwezo wa kuhimili mazingira hasa ya vijijini.
Kuna aina mbalimbali ya kuku hawa ikiwamo Black/ white australorps, kroiller, Rhodes island red, red hamshire, Sussex etc. Hawa ni kuku ambao wanaserve purpose zote za mayai na za nyama. Mfano kuku aina ya black/white australorps wao wanauwezo wa kutaga mpaka mayai 250 kwa mwaka, tofauti na wa kienyeji, mayai ya kuku hawa huwa makubwa na yenye kasha jeupe na kiini cha njano kama utawafuga kwenye mazingira na mbinu asilia (za kienyeji).
Ukilinganisha uwezo wa utagaji wa kuku hawa utagundua utagaji wao ni Zaidi ya asilimia 500% ukilinganisha na ule wa kienyeji pure. Idadi hii ya mayai toka kwa kuku mmoja kwa mwaka, anaweza kumwezesha mfugaji kuzalisha mayai kwa wingi na kushusha Zaidi bei ya mazao yake (mayai) kuwa chini kuweza kuliteka soko kwa urahisi Zaidi. Kumbuka, bei ya juu ya mayai ya kienyeji ni kwaajili ya kulipia gharama kubwa za utunzaji wa kuku huyu ilihali utagaji wake ni hafifu.
Pili, kuku hawa wana nyama nyingi Zaidi kuliko hawa wa kienyeji kwa majogoo hufikia mpaka uzito wa kilo 3-3.5. huku matetea hufikia kilo 2-2.5 na huwa na nyama nzuri, iliyokomaa vyema na yenye ladha. kwa uzito huu kwa majogoo, kuku hawa uuzwa kwa bei ya 20,000 - 25,000 wakiwa hai. bei ambayoni kwa mujibu wa bei ya soko kwa makadirio ya shilingi 8,000 kwa kilo kwa nyama nyeupe.
Mapungufu
Pamoja na ubora wa kuku hawa katika ufugaji wa kibiashara, kuku hawa pia wanachangamoto mbali mbali ikiwemo kutokuwa na uwezo wa kutamia. Pamoja na hii kuwa changamoto pia ni fursa kwani kwa yeye kutotamia kunamwongezea nafasi ya yeye kuendelea kutaga mara nyingi Zaidi bila kupumzika. Hivyo changamoto hii ni faida kwa mfugaji anaelenga kufuga kwa tija. Kwa vile mayai haya huwa yamerutubishwa na majogoo, nirahisi kwa mfugaji kuongeza idadi ya kuku kwa kupitia kutotolesha kwa mshine za kuangulia vifaranga au kumpa kuku mwingine ayatamie kwa niaba.
Neno la kufungia:
“ I think I touched a raw nerve when I said farming is NOT cool! I believe farming takes a lot of HARD work and dedication. Lets not lie to the youth that they'll become instant millionaires when they get into farming. It becomes "cool" once you master the trade......” caleb
Ufugaji unalipa ukiweza kuibudu biashara ya ufugaji,
Kwa ushauri Zaidi kuhusu shughuli za ufugaji, tuwasiliane kwa namba 0755815174. pia pata fursa kusoma ya Makala mbali na utaalamu kutoka kwenye mtandao wetu www.backyard.co.tz
Nimejaribu kuattach picha za baadhi ya kuku bora wanaofaakufugwa kienyeji na wakaleta tija kibiashara hapa chini. Neno langu si sharia, nakaribisha Michango
View attachment 385750
View attachment 385751
View attachment 385752
View attachment 385753
View attachment 385754
Mkuu shukrani kwa maelezo mazuri, yanatia Moyo kwa ambao tunataka kuanzisha miradi ya kuku wa Kienyeji. Tunaweza kujifunza mengi kupitia watu kama nyie wenye uzoefu kama wewe na GinnerNimesoma makala yako kwa undani but mengine si kweli.n imegundua pia unavutia biashara yako pia!
Kwa mfano mm nilianza na kuku 3,majike 2 na dume 1 wa kienyeji.ilikua mwisho wa mwezi wa 12 mwaka jana 2015. But mpaka mwez wa sita mwaka huu nilikuwa nimepata kuku zaid ya 60. Kuku wangu wanataga wastan wa mayai 15-18. Na kila baada ya miezi miwili ni lazima watoto.ninachokifanya vifaranga nilikua nabitunza mwenyewe toka siku ya kwanza kutotolewa .
Kuku wangu wanataga kila baada ya wiki 2 baada ya kutotoa.
Tena nimegundua njia nzuri ya kuku wa kienyeji kutotoa vifaranga kuanzia 20-24. Kwa wakati mmoja na kwa kuku mmoja.
Kuku wa kienyeji wanalipa kama itaamua kukomaa na kufuata maelekezo.
Ufugaji wa kuku wa kienyeji una changamoto zake japo zinaweza tatulika pia.
Picha ya kuku alolalia mayai 23.Kuku wangu mmoja ameanza tena kulalia mayai tena nimempa mayai 23 nategemea atotoe yote. Nitawatumia picha ya namna ya kumwekea mayai kwa beseni la kunawia.
Nitakutafuta ndg nimekuelewa. Huyo jamaa kachemka lkn nae niuelewa wake..Nashukuru kwa kukubali kupokea challenge,
kwa ufupi andiko lako limejaa upotoshaji mkubwa na linalenga kuwakatisha tamaa, wajasiriamali wadogo wadogo ambao wanapendelea kufuga kuku wa kienyeji.
Pia nimegundua mambo makubwa mawili,
1. Bila shaka utakuwa unauza hiyo aina ya kuku amabayo unadai kuwa ni wazuri.
2. Bado hujajua mbinu mbali mbali za ufugaji wenye tija.
Hebu tazama hapa, ulichoandika.
Kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji wa mayai 7-10 na mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga - siku 50-60. Hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka kwani anapoteza muda mwingi kwa shughuli za utamiaji na malezi ya vifaranga badala ya kutaga. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.
kuku wa kienyeji wanataga mayai 15 hadi 20 na sio kwa siku za mfululizo kuna siku nyingine huwa hatagi na hii inatokana na kutokushiba vizuri, nakubali kuhusu muda wa kulea kuwa ni siku 50 hadi 60. unachotakiwa kufanya siku tatu baada ya kuku kutotoa vifaranga, mnyang'anye vifaranga na uviweke mbali nae huko vipatie chakula cha kukuzia stater, maji ya kunywa changanya na glucose, pia weka na chanzo cha joto kama ile mtungi wenye mkaa wa moto ndani yake.
ukifanya hivyo itamchukua kuku huyo uliemnyang'anya vifaranga wiki mbili na kuanza tena utagaji.
kwa mwaka atatoa kati ya mayai 100 hadi 160 kwa uhakika.
Tizama na hapa.
'Mayai ya kienyeji ni kati ya bidhaa ngumu Zaidi kuhifadhika. Ikumbukwe kuwa tofauti na mayai ya kisasa, mayai ya kienyeji huwa yamerutubishwa na majogoo. Hivyo kuharibika ndani ya muda ya week moja au pungufu kama hayatatuzwa katika mazingira salama kwaajili ya utunzaji. Kipindi cha joto kali, mayai haya huanza kujitenenezea kifaranga au mishipa ya damu ambayo baada ya muda mfupi hugeuka viza na kutofaa kwa matumizi tena.
uhifadhi wa mayai ya kienyeji sio mgumu, yanakaa bila ya kuharibika kwa muda wa mwezi mmoja, unachotakiwa kufanya, hifadhi mayai yako ktk trey ya mayai, pia chunguza kama yai lina ufa hilo usilihifadhi litumie kwa kula mwenyewe na familia, pia weka mayai yako sehemu ya wazi ambayo ina mwangaza wa kutosha, kuyaweka mayai sehemu isiyo na mwangaza kutapelekea mayai kuanza kutunga kifaranga ndani yake (hiyo ni kwa mayai ya kuuza kwa matumizi ya lishe)
kama unahifadhi yai la kutotolesha hilo halitakiwi lizidi siku 14 uwe tayari ushampa kuku kwa ajili ya kuatamia.
kwa faida yako na wengine si lazima kuku wa kienyeji apandwe na jogoo ndio atage, umri wake wa kutaga ukifika tu ataanza kutaga, ambao ni miezi sita hadi saba.
Pia bei ya kuku wa kienyeji zaidi kutokana na ladha yake na wala sio kilo zake.
Mwisho.
Ningefarijika sana kama unge declare interest kuwa wewe ni mfanya biashara wa hao kuku uliowapigia debe, hata ukaweka na picha zao na namba yako, kuliko kuwakatisha tamaa wafugaji waliojikita ktk ufugaji mdogo mdogo wa kuku wa kienyeji.
Pia nawatia moyo wafugaji wote wasikatishwe tamaa na maandiko kama hayo bali yawe chachu ya wao kujua zaidi mbinu mbali mbali za kupata kuku wengi ndani ya muda mfupi na wasichoke kujifunza.
kama utanataka kujua chochote kuhusu kuku wa kienyeji njoo in box nitakusaidia bila ya malipo yoyote, mimi sio mfanya biashara, nami nakaribisha kukosolewa.
Asante kwa mchango wako mkuu.kiukweli kama unataka kua mfugaji usiogope wala kusikia maneno yenye kukatisha tamaa.mm nilipata maelezo mengi na maandiko mengi tena humu jf hasa jamaa mmoja aitwae Gazeti ana uzi wake humu.nilisoma makala yote bila kuacha hata coment moja.nikaanza kufuga.kiukweli mwanzo nilipata changamoto saana nakumbuka mara ya kwanza nilianza na kuku wawili baada ya kama miezi minne nikawa na kuku zaid ya 40. Kilichotokea ni malaika wako ndo wanajua maana wooooote walikufa baada ya kupata ugonjwa.nilikula kuku mpaka wakanikina moja leo mm hua Sili firigisi maana zilinikifu kabisaaa!mama yoyo akapata hasira akaniambia hakuna kufuga tena mpka tuhamie kwetu coz nilikua nimepanga! Nami ckua na ubishi maana yy ndo mhudumiaj mkuu hapa hom.nikawa nasoma makala mblmbl kujiongezea maujuzi.nikshamia hom kwangu nikaanza na kuku wawili tena baada ya miezi 4 nikapata kama 60 pamoja na makinda nao pia nikapata mtikisiko wakapata ugonjwa nikabak na mmoj nikaanza tena. Sasa nimeanza kutulia maana nimejifunZa mengi.hakuna kukata tamaa.Mkuu shukrani kwa maelezo mazuri, yanatia Moyo kwa ambao tunataka kuanzisha miradi ya kuku wa Kienyeji. Tunaweza kujifunza mengi kupitia watu kama nyie wenye uzoefu kama wewe na Ginner
Uko wapJamani nahitaji mayai ya kanga, please
Safi Sana Mkuu, Tunashukuru kwa kututia moyo, Miaka mi3 inatosha kabisa kukupa ujuzi na uzoefu kuhusu huu mradi, Ni dhahiri tutajifunza mengiGinner
Mimi ni mfugaji wa kuku wa kienyeji pure. Nimeanza miaka mi3 iliyo pita na nimepata faida sana hata kuku wa kizungu sitamani
1 wana soko hasa katika mahoteli makubwa
2 kuku wa kienyeji anafundishika tabia. Na ukitaka faida usisubiri kuku akulele vifaranga
3 kuku wa kienyeji ni wavumilivu na hawahitaji mlolongo saana wa chakula ( kila siku madini n.k)
Mimi naweza nikakukosoa saaaana na kukuomba uombe radhi kwa wana jamvi
Kiwango cha kuku nilicho nacho. Kila mwezi lazima nipate zaidi ya 90( trey 3 hizo). Soko langu liko kwenye mahoteli na mayai yanakaa wiki 2 hadi kuharibika na kuharibika kwakwe si kwamba ushindwe kula.
12
Utengenezaji wa vyakula vya Kuku
Namba moja hadi nne katika jedwali hili ni michanganyiko wa vyakula aina 4 tofauti
kwa ajili ya kuku wenye umri uliotajwa hapa juu. Ukihitaji kuandaa chakula cha kuku
hao, chagua mchanganyiko mmoja (kwa safu wima) wenye malighafi zinazopatikana
kwenye eneo lako kwa urahisi na utakazozimudu kifedha.
UTAYARISHAJI CHAKULA CHA KUKU WANAOTAGA (MIEZI 5 HADI MIEZI
18) PAMOJA NA KUKU WAZAZI
Aina ya vyakula
Kiasi (kilo)
Chenga za Mahindi
31.5kg
Mtama
15.0kg
Pumba ya mahindi
13.0kg
Mashudu ya Alizeti
20.0kg
Dagaa
12.0kg
Chokaa
3.0kg
Premix
0.25gm
Chumvi
5.0gm
Jumla
100kg
-------------------------------------------------------------------------------
Aina ya vyakula
Kiasi (kilo)
Dagaa kilo
12.0kg
Chenga za mahindi
30.0kg
Mtama
6.75kg
Mashudu
20.0kg
Pumba ya mahindi
23.0kg
Chumvi
0.25gm
Chokaa
3.0kg
Mifupa
5.0kg
Jumla
100kg
AU
Vyakula hivi vyote vinafaa kwa kuku watagaji na kuku wazazi. Tofauti kwenye kuku
wazazi ni kuwa wanalishwa kiasi pungufu ili wasinenepe na kushindwa uzalishaji.
Mwongozo uliotolewa, hapa juu ni kwa ajili ya kuandaa kilo 100 za chakula cha kuku,
endapo unataka kutengeneza kilo 500 itabidi kila kilichopo kwenye mchanganyiko
kizidishwe, mara tano ndipo kupata hizo kilo 500....HAKIKA KINAFANYA KAZI JARIBU HIYO 4MLA END INGATIA HAWAUMWI UTAPATA MATOKEO
Hongera mkuu! Huna hiyana Mungu atakuongezea! Mm sio mfugaji wa kuku, na wala sitegemei kufuga kuku kwa maengo ya biashara, ila nimeukubari mchango Wako!Kuna jamaa yangu mmoja alinielekeza namna nzuri ya kuku kutotoa mayai yote bila kuacha. Ni kwamba aliniambia ninunue vile vibeseni vidogo vya kunawia then ndan unaweka mchanga kiasi halafu weka mayai yako tayari kwa kuliwa na kuku. kiukweli njia hii nilitumia na imefanikiwa. kwa wafugaji wenzangu jaribuni muone maajabu yake.
Kitu kingine ni utunzaji wa vifaranga baada ya kutotolewa napo hapa kuna changamoto wakati wa usiku kutokana na barid kwa vifaranga hasa kwa wafugaji wa hali ya chini,mm mwanzo nilihangaika but nikapata njia nyingine bora ya kutunza vifaranga wakati wa usiku,nilitenga sehm ya kuwalaza. Hapa unaweza chukua hata box kubwakubwa la kuwatisha vifaranga then nikatafuta chungu!! Nikaweka majivu ndani kwa hio kila usiku nilikua unaweka mkaa wa moto mle ndani ya chungu na kufunika na majivu!! Nakwambieni ndugu zangu wafugaji vifaranga hawapati barid kabisaaa! Na huo moto ulioko ktk hilo jivu utaukuta mpka asubuhi na utatumia kwa kuwashia moto hapo kwa nyumba yako. jaribuni na njia hii muone mafanikio yake na si kukaa ohhh nitanunua vifaranga 500 nianze hapana anza hata na kuku 2 au 3 baada ya mda utakuja nambia. Yangu ni hayo labda hujaelewa uliza tupeane maujuzi.
Nashukuru kwa kukubali kupokea challenge,
kwa ufupi andiko lako limejaa upotoshaji mkubwa na linalenga kuwakatisha tamaa, wajasiriamali wadogo wadogo ambao wanapendelea kufuga kuku wa kienyeji.
Pia nimegundua mambo makubwa mawili,
1. Bila shaka utakuwa unauza hiyo aina ya kuku amabayo unadai kuwa ni wazuri.
2. Bado hujajua mbinu mbali mbali za ufugaji wenye tija.
Hebu tazama hapa, ulichoandika.
Kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji wa mayai 7-10 na mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga - siku 50-60. Hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka kwani anapoteza muda mwingi kwa shughuli za utamiaji na malezi ya vifaranga badala ya kutaga. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.
kuku wa kienyeji wanataga mayai 15 hadi 20 na sio kwa siku za mfululizo kuna siku nyingine huwa hatagi na hii inatokana na kutokushiba vizuri, nakubali kuhusu muda wa kulea kuwa ni siku 50 hadi 60. unachotakiwa kufanya siku tatu baada ya kuku kutotoa vifaranga, mnyang'anye vifaranga na uviweke mbali nae huko vipatie chakula cha kukuzia stater, maji ya kunywa changanya na glucose, pia weka na chanzo cha joto kama ile mtungi wenye mkaa wa moto ndani yake.
ukifanya hivyo itamchukua kuku huyo uliemnyang'anya vifaranga wiki mbili na kuanza tena utagaji.
kwa mwaka atatoa kati ya mayai 100 hadi 160 kwa uhakika.
Tizama na hapa.
'Mayai ya kienyeji ni kati ya bidhaa ngumu Zaidi kuhifadhika. Ikumbukwe kuwa tofauti na mayai ya kisasa, mayai ya kienyeji huwa yamerutubishwa na majogoo. Hivyo kuharibika ndani ya muda ya week moja au pungufu kama hayatatuzwa katika mazingira salama kwaajili ya utunzaji. Kipindi cha joto kali, mayai haya huanza kujitenenezea kifaranga au mishipa ya damu ambayo baada ya muda mfupi hugeuka viza na kutofaa kwa matumizi tena.
uhifadhi wa mayai ya kienyeji sio mgumu, yanakaa bila ya kuharibika kwa muda wa mwezi mmoja, unachotakiwa kufanya, hifadhi mayai yako ktk trey ya mayai, pia chunguza kama yai lina ufa hilo usilihifadhi litumie kwa kula mwenyewe na familia, pia weka mayai yako sehemu ya wazi ambayo ina mwangaza wa kutosha, kuyaweka mayai sehemu isiyo na mwangaza kutapelekea mayai kuanza kutunga kifaranga ndani yake (hiyo ni kwa mayai ya kuuza kwa matumizi ya lishe)
kama unahifadhi yai la kutotolesha hilo halitakiwi lizidi siku 14 uwe tayari ushampa kuku kwa ajili ya kuatamia.
kwa faida yako na wengine si lazima kuku wa kienyeji apandwe na jogoo ndio atage, umri wake wa kutaga ukifika tu ataanza kutaga, ambao ni miezi sita hadi saba.
Pia bei ya kuku wa kienyeji zaidi kutokana na ladha yake na wala sio kilo zake.
Mwisho.
Ningefarijika sana kama unge declare interest kuwa wewe ni mfanya biashara wa hao kuku uliowapigia debe, hata ukaweka na picha zao na namba yako, kuliko kuwakatisha tamaa wafugaji waliojikita ktk ufugaji mdogo mdogo wa kuku wa kienyeji.
Pia nawatia moyo wafugaji wote wasikatishwe tamaa na maandiko kama hayo bali yawe chachu ya wao kujua zaidi mbinu mbali mbali za kupata kuku wengi ndani ya muda mfupi na wasichoke kujifunza.
kama utanataka kujua chochote kuhusu kuku wa kienyeji njoo in box nitakusaidia bila ya malipo yoyote, mimi sio mfanya biashara, nami nakaribisha kukosolewa.
Mkuu kwanza nikupingeze kwa makala yako nzuri.
Ila mimi niko katika kufanya utafiti na hawa kuku wa kienyeji na nimechagua kuku 7Majike na jogoo mmoja. Nimefanikiwa kwa mwezi wa nne sasa kupata mayai 5 kila siku yakishuka ni 4 kuku hupunzika kidogo na kuendelea siwalazishii naweka mayai kwenye mashine.
Tunachotakiwa ni kubuni mbinu za kuwafuka kuku wa kienyeji kwa maslahi na sio kuwaacha.
Pia ninao wengine nafuga ila nitatoa taarifa kamili baada ya utafiti kufika kikomo.
Kwa hiyo hutawafuga?Uko sahihi boss, nimekupendaje